Makapuku Forum

Makapuku Forum

82ae30c69ff838bf000c9295a1712379.jpg
Yuck! ‍♂️‍♂️‍♂️
 
Nasikia hata Marekani mwanzo hawakuwa wakiruhusu wanawake kupiga kura! Walikuja kuruhusu baada ya kujihakikishia kuwa kiwango chao cha elimu kimekuwa sawa na wanaume
Marekani wanawake waliruhusiwa kupiga kura majuzi juzi hapa tu (mwaka 1920) na mpaka leo bado wanabaguliwa hasa katika mishahara. Kwa wastani mwanamke wa Marekani leo hulipwa senti 79 kwa kila dola ambayo mwanaume hulipwa. Yaani kama mwanaume analipwa dola 1 kila saa hata kama ni kwa kazi ile ile, elimu ile ile... mwanamke yeye atalipwa senti 79.
 
Huku Uswaz kwetu tumelala giza km bundi jana na tumeamka gizani km kuku bandani na hadi sasa umeme haujarudi
Jovyo hata simu chaji imekata ila IPTL/Dowans nasikia hata umeme usipokiwepo wanalipwa tu mamilioni yao kila siku
.....
...Watu walishachukua chao...and guess what? Hao hao waliochukua chao mapema na kujitajirisha kupindukia jamii inawaheshimu sana na kuwaona wajanja. Mtemi Chenge Joka Makengeza lililoshindikana alipofukuzwa uwaziri kwa ile ishu ya rada alipata mapokezi huku Usukumani ambayo hayajawahi kutokea. Magari na watu walijipanga kutokea Mwanza mpaka Bariadi (mwendo wa karibia masaa sita kwa gari). Watu wanaabudu wenye pesa na wewe ukiwa mwadilifu ukapewa ulaji usiibe ukistaafu hujatajirika jamii inakucheka. Kwa Falsafa kama hii ufisadi utaisha lini? Ndiyo maana, pamoja na matatizo yake yote mengineyo, namheshimu sana Mwl. Nyerere japo naye anachekwa kwa kufa masikini na kutowaachia utajiri wanae. Na nadhani masikini alimwamini kabisa kabisa mwanafunzi wake Mkapa kuwa ni mwadilifu mpaka kuzunguka nchi nzima kumpigia kampeni. Jamaa akageuka na kuwa mpigaji wa kutisha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom