Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ukweli tunapaswa kuombea taifa letu ,mambo ni mengi mno ,mahali hapa tunaweza kuungana pamoja kuomba na kuona ukuu wa Mungu katika kila jambo

YAKOBO 5

16.b...kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana,akiomba kwa bidii.

17.Eliya alikua mwanadamu mwenye tabia moja nasisi,akaomba kwa bidii mvua isinyeshe,na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18.Akaomba tena,mbingu zikatoa mvua,nayo nchi ikazaa matunda yake.

Shalom
Shalom mama mchungaji
 
3/Bang Na Expressway
fab2c1cf763370dd02e7532bdccf81b9.jpg
4e1fea6c511dcf33dff95b0de484c3f2.jpg

Ndo lilikuwa likishikilia rekodi ya dunia hadi hapo mwaka 2010 lilipoondolewa kwenye orodha kwa sababu tu halikatizi sehemu yoyote majini(Flyover}
Ni flyover ya njia 6 huko nchini Thailand
Lina urefu wa Km 55
.......
Usipokuwa makini unarudi ulikotoka
 
2/Tanjin Grand Bridge
d9c5c6e686ea09a64ed9015f3fec1560.jpg
8a5e6a1b94ee1b1fbd8fbf2f16a9bb40.jpg

Ni daraja la reli linaloziunganisha Langfang na Qingxian
Ni njia ya treni ya spidi kutoka Beijing hadi Shanghai....Sisi huku huita SGR
Lina urefu wa Km 113.7
.......
Aisee refu sana hilo
 
Jambo lingine la kujifunza kule China
Ni kwamba serikali yao hawataki pesa yao iwe na thamani kubwa ili tu kuvutia kibiashara yaani export trade ndiyo maana wametawala soko la dunia

Chukua mfano dola ya Marekani ina thamani kubwa sasa mbongo ukanunue TV huko kwa SHIMBA dola 500 sijui ikija huku Bongo utamuuzia Nyagei Tsh ngapi

.........
Lazima atataka aniuzie zaidi ya 900k dollars

Na hapo ndipo atakapobaki nayo
 
Asante sana mdau Shimba, kuandika ni 'hobby' na ninafurahi na kujiskia vizuri kuwa sehemu ya familia hii, Makapuku ambako kumejaa member wanaojitambua na kujali masiha yao na ya wengine bila kukereka wala kukereketwa.
Nikiingia humu huwa najifunza mengi sana tena ya msingi na yananifanya niwe na wakati mzuri nikaa kusaka mkate wangu na wa wapwa zako.

Hapo nilipopabold, ndo wanapokosea, ni kweli wapo watoto wa shule humu, JF ni kama kokoro... na unajua kokoro linaleta si samaki tu. Humu makapuku kuna watu wa fani zote na mada humu huwa zinaongelewa japo kiurahisi rahisi lakini ndo zinaeleweka vizuri sana.

Nikupe mfano mdogo tu, enzi hizo gazeti la Daily News lilikuwa linaandikwa kwa kiingereza kigumu hadi unajiuliza hawa waandishi ni maAnglo Saxon ama vipi? Yalipokuja mengine kama The Express, Guardian na mengine nikaona kumbe huna haja sana ya kuandika mabombastic ili uonekane unajenga hoja.

Hoja ni hoja pale inapoeleweka, na hili ndilo linalofanywa na Makapuku
Sina la kuongeza mkuu
 
Siyo kutega nimeongea ukweli toka moyoni Mkuu.

Pia natumai siyo kosa wala nini!
Huyo binti nampenda sana.

Sitojali kapendwa na wangapi wala na nani!

"I will fight and win"

Nakuelewa na nakupenda sana Sakayo
Habari yako lakini.....

Tumewahi kuonana wapi mkuu, maana Unaongea kwa kujiamini halafu mie ndo kwaaanza nakuona leo
 
Usipokuwa makini unarudi ulikotoka
Ni kweli. Siku moja nakwenda kumchukua mtu airport nikakosea exit zote mbili kutokana na labyrinth ya mi-flyover yao hii. Nikajikuta nimeingia kwenye mzinga wa daraja reefu tena juu ya bahari halafu traffic ni bumper to bumper. Kulivuka tu karibia lisaa lizima ndiyo sasa nikaanze kuangalia utaratibu wa kurudi. Mgeni nikamwambia achukue taxi tutakutana nyumbani jioni. Mashikolomageni baba!
 
Hii ni kwa mpendwa wangu wa dhati kabisa pasi na kupepesa macho mnamjua kama hamumtambui basi nami sitambuliki.
Jorowe amesema kwake kuandika ni hobby na huwa anafarijika anapoandika hasa kutuandikia sisi Makapuku wengine, naheshimu mchango wako Obe.
Leo katika kusikiliza nyimbo zilizopo kwenye flash niliyoletewa na shemeji yenu kuna wimbo umeimbwa na George Benson unaitwa Nothings gonna change my love for you, Jorowe utakuja kuongezea nyama hapa ili tujue original version ya wimbo huu.
Baada ya kusikiliza nikapata wazo la kusikiliza ikiwa katika guitar version na hii imekuwa nzuri zaidi maana unajikuta kama upo studio unaingiza sauti.



Leo nimejitahidi kuandika sababu kuna vitu vimenisukuma kufanya
Cc Linamo
Cc Obe (Jorowe)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom