Makapuku Forum

Makapuku Forum

Interesting!

Yaani hapo ndo sisi tumeshindwa kabisa, yaani tunafurahia kujaza mapesa mfukoni bil kuyazungusha. Yaani mtu kuanzia jtatu hadi jpili anakula kwake tu, hajui kama kuna mamantilie wametoa ajira.

Na trend inayoendelea sasa badala ya kuifanya private sector iajiri watu wengi kwa kuipa tender za serikali serikali inachofanya ni kutoa pesa kwenye mfuko wa suruali na kuziweka kwenye mfuko wa shati utasema kadi nyekundu. Huwezi kujenga uchumi kwa kukalia mapesa huku bank zikishindwa kukopesha.

Kwa serikali kutoonesha kutaka kushirikiana na sekta binafsi (kana kwamba yenyewe ndo muajiri mkuu) linaundwa kundi kubwa la watu wasio na ajira na hii ni hatari kwa afya.

wenzetu wanazipa sekta binafsi ushirikiano ili zitoe ajira na uchumi usimame sawasawa sisi tunakazana (kazana) kujadili jaza ujazwe, lipa ukatiwe yaani akili za kijinga kabisa.

Kwa kusikiliza mijadala ya kuanzia kwa rais hadi bunge, utagundua kuwa, mosi wabunge wetu wengi wako hai kuanzia kiunoni kushuka chini ( ndo mana utasikia, kikalishe, jazwa ujaze) na pale feri kwetu tunapofurahia harufu ya shombo pameoza kuanzia shingoni kwenda juu. Shingoni kushuka chini pako makini sana kama makanikia.

Asante sana mdau, yaani ulichoandika hapo juu wallah tena nasikitika kwanini bia zinazidi kuongezewa kodi ilhali kuna watu serikalini hawalipi kodi kwenye mishahara yao mikubwamikubwa
Maneno kuntu
 
Napenda uwasilishaji wako. Una uwezo wa kuandika (kumzidi hata bwana yuleeee!) na inaonekana uko siriazi. Mtu akisoma ni lazima tu ajifunze kitu kipya. Ni mambo kama haya yanayoifanya Makapuku izidi kuheshimika na kuondoa ile dhana potofu kwamba sote tulioko huku ni watoto wa shule wapiga porojo tu tusio na mbele wala nyuma.


Asante sana mdau Shimba, kuandika ni 'hobby' na ninafurahi na kujiskia vizuri kuwa sehemu ya familia hii, Makapuku ambako kumejaa member wanaojitambua na kujali masiha yao na ya wengine bila kukereka wala kukereketwa.
Nikiingia humu huwa najifunza mengi sana tena ya msingi na yananifanya niwe na wakati mzuri nikaa kusaka mkate wangu na wa wapwa zako.

Hapo nilipopabold, ndo wanapokosea, ni kweli wapo watoto wa shule humu, JF ni kama kokoro... na unajua kokoro linaleta si samaki tu. Humu makapuku kuna watu wa fani zote na mada humu huwa zinaongelewa japo kiurahisi rahisi lakini ndo zinaeleweka vizuri sana.

Nikupe mfano mdogo tu, enzi hizo gazeti la Daily News lilikuwa linaandikwa kwa kiingereza kigumu hadi unajiuliza hawa waandishi ni maAnglo Saxon ama vipi? Yalipokuja mengine kama The Express, Guardian na mengine nikaona kumbe huna haja sana ya kuandika mabombastic ili uonekane unajenga hoja.

Hoja ni hoja pale inapoeleweka, na hili ndilo linalofanywa na Makapuku
 
Interesting!

Yaani hapo ndo sisi tumeshindwa kabisa, yaani tunafurahia kujaza mapesa mfukoni bil kuyazungusha. Yaani mtu kuanzia jtatu hadi jpili anakula kwake tu, hajui kama kuna mamantilie wametoa ajira.

Na trend inayoendelea sasa badala ya kuifanya private sector iajiri watu wengi kwa kuipa tender za serikali serikali inachofanya ni kutoa pesa kwenye mfuko wa suruali na kuziweka kwenye mfuko wa shati utasema kadi nyekundu. Huwezi kujenga uchumi kwa kukalia mapesa huku bank zikishindwa kukopesha.

Kwa serikali kutoonesha kutaka kushirikiana na sekta binafsi (kana kwamba yenyewe ndo muajiri mkuu) linaundwa kundi kubwa la watu wasio na ajira na hii ni hatari kwa afya.

wenzetu wanazipa sekta binafsi ushirikiano ili zitoe ajira na uchumi usimame sawasawa sisi tunakazana (kazana) kujadili jaza ujazwe, lipa ukatiwe yaani akili za kijinga kabisa.

Kwa kusikiliza mijadala ya kuanzia kwa rais hadi bunge, utagundua kuwa, mosi wabunge wetu wengi wako hai kuanzia kiunoni kushuka chini ( ndo mana utasikia, kikalishe, jazwa ujaze) na pale feri kwetu tunapofurahia harufu ya shombo pameoza kuanzia shingoni kwenda juu. Shingoni kushuka chini pako makini sana kama makanikia.

Asante sana mdau, yaani ulichoandika hapo juu wallah tena nasikitika kwanini bia zinazidi kuongezewa kodi ilhali kuna watu serikalini hawalipi kodi kwenye mishahara yao mikubwamikubwa
Jambo lingine la kujifunza kule China
Ni kwamba serikali yao hawataki pesa yao iwe na thamani kubwa ili tu kuvutia kibiashara yaani export trade ndiyo maana wametawala soko la dunia

Chukua mfano dola ya Marekani ina thamani kubwa sasa mbongo ukanunue TV huko kwa SHIMBA dola 500 sijui ikija huku Bongo utamuuzia Nyagei Tsh ngapi

.........
 
Jambo lingine la kujifunza kule China
Ni kwamba serikali yao hawataki pesa yao iwe na thamani kubwa ili tu kuvutia kibiashara yaani export trade ndiyo maana wametawala soko la dunia

Chukua mfano dola ya Marekani ina thamani kubwa sasa mbongo ukanunue TV huko kwa SHIMBA dola 500 sijui ikija huku Bongo utamuuzia Nyagei Tsh ngapi

.........
Karibu Koromije mkuu. Huku TV ni laki tatu tu unapata. Unachosema hata hivyo ni kweli. Ndiyo maana Marekani huwa wanamlaumu sana Mchina kuwa huwa anafanya currency manipulation - mbinu za makusudi ili kuifanya pesa yake ibakie chini ikilinganishwa na dola hata kama uchumi wake unakua kwa kasi. Vita vya wakubwa!
 
Wakati najisomeasomea elimu za darasani, nilivutiwa naye sana.
Hakujikita katika mambo hasi yanayomfanya mtu asifanikiwe, yeye aliamini kila mmoja wetu ana uwezo wa kufanikiwa kwa kuwa tu tuna vipawa tofauti, na hasa tukitia jitihada kuboresha maisha yetu. Aliandaa hii inayoitwa 'hierarchy of needs'.

Ili ufanikiwe, kuna ngazi lazima uzipande, na ngazi moja hufanya hamu ya kupanda zaidi.
Ngazi ya kwanza; Mahitaji ya kimwili na kiasili: Unahitaji kula , kunywa , malazi, kulala na kulalana. Physiological and biological needs

Ngazi II: Mahitaji ya kuwa salama, hapa anasema ili ufanikishe ndoto zako baada ya kuwa umeshiba kimwili na kiafya basi ni lazima uwe na uhakika wa usalama wako pindi unatekeleza majukumu ya kujitafutia kipato iwe shambani (kule kibiti /Rufiji ni ngumu), usiwe na hofu.

Ngazi ya III: Mahitaji ya mapenzi na kujinasibisha, hapa kila mmoja ana haki ya kupendwa, ukaribu (intimacy), kuaminiwa na kukubalika (love and belongingness)

Ngazi ya IV: Esteem needs , weee Mondray hebu njoo uweke link hapa ili kujua kwamba kuna hitaji la kujithamini, kutojiweka chini
Na ngazi ya tano ni kujitambua wewe ni nani na unajukumu gani. Hii utaifikia baada ya kuwa umepitia ngazi zote hizo.

Labda tu kwa kuongezea hapa, kuna hitaji/motisha ya utambuzi. Ukiweza kutambua na kuelewa kupitia maarifa tofauti uhakika wa kufanikiwa ni mkubwa tofauti na ukiwa bwege mtozeni, utatoswa hata na wanasiasa wajinga wa mwisho. Soma soma, angalia news, pitia Makapuku nk

Pia kuna motisha ya kujiweka smart, ndo maana watu hawakauki gym kujenga mwili , kujipodoa ukapodoka (aesthetic needs), kutafuta kakitambi kaheshima kama nilikonako.

Na pia kuna motisha ya kuwasaidia wengine kufanikisha ndoto zao (transcendence needs) hapa ndo unakutana na waombeaji wote, walimu na wewe Kapuku unayesoma hapa.
Well, nimeandika sana eeh. Pole na asante kwa kumsoma Mussolin5 na leo katika historia
Ukiunganisha nguvu na SHIMBA YA BUYENZE mtafanikiwa kumrudisha Shedebe na hadithi yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom