Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mambo Muhimu usiyo yajua kuhusu Twiga

Twiga ana miguu mirefu,shingo ndefu sana,ulimi mrefu na pembe fupi zilizo butu.Mwili wake una mabaka yenye rangi ya kikahawia(njano )na kuzungukwa na rangi ya maziwa.

Mnyama huyu anapatikana katika nyika hususan sehemu zenye migunga pamoja na mikakaya,miti ambayo huifurahia sana na ni chakula chake kikuu.


Twiga hana ushindani mkubwa wa chakula na wanyama wengine kwa vile yeye hula majani ya juu nchani wakati wanyama wengine hawafikii majani hayo.

Twiga ana urefu wa kati ya mita 4.8 na 5.5 Uzito wake ni kati ya kilo 700 na 1500.Twiga jike ana rangi ng'avu zaidi kuliko dume.Hii inaweza kuwa ni maumbile ya kuwavutia Twiga dume.Dume ni mkubwa na mzito kuliko jike.View attachment 521248

Urefu wa ulimi wake ni kati ya sentimeta 46 hadi 50 wakati ambapo urefu wa moyo ni meta 0.6 Ana uwezo wa kukimbia kilometeta 55 kwa saa.Mkia wake ambao ni meta 2.4 ni mrefu kuliko mikia ya wanyama wote duniani.

Twiga huzaa mtoto mmoja kwa mara moja na huweza kuishi kati ya miaka 20 hadi 30.Huchukua mimba kwa muda wa miezi 14.15 hadi 15.mtoto anapozaliwa huwa na uzito wa kati ya kilo 45 hadi 70 na urefu wa mita1.8

Shingo yake ndefu hufanya mwendo wake kuwa wa madaha na kuwavutia watu wengi.View attachment 521247
Vipi kuhusu sexual organs za twiga. Ni kama za punda kihongwe?
 
MATHAYO 7

7. Ombeni nanyi mtapewa,tafuteni nanyi mtapata,bisheni nanyi mtafunguliwa.

Mungu ulisema niombe nami nitapewa.Na nitafute nami nitapata.Nibishe nami nitafunguliwa.

MPENDWA
USIACHE KUOMBA,KANUNI HII INATUHAKIKISHIA KUPATA TUTAKACHOOMBA KWA IMANI
NAWATAKIA MCHANA MWEMA
Kila aombae hupewa. Ni kweli hii Mama mchungaji?
 
+Twiga ndiye mnyama ambaye ni nembo ya Taifa la Tanzania
Duniani kote wanyama ni utambulisho wa Taifa Fulani
Mfano
Uganda ni korongo(flamingo) wakati USA ni tai(Eagle)
........
Asante

Umenikumbusha Uganda ...huyo mnyama anaheshimika kinomaaaa

Enzi hizo nahis mpaka sasa walikuwa wanatishiwa ukimuua na wewe unakufaa

Wanamlinda sana
 
Ni uchaguzi binafsi wa nchi
Kwani hajawahi kuona hata bendera hufanana

Hutumika kwa ajili ya utalii na pia kutambulisha nguvu/tabia ya Taifa husika
Mfano
USA wanatumia Eagle na ni taifa babe kijeshi na kiuchumi wakati Tz tunatumia Twiga ni Taifa lenye ukarimu na upole/unyonge karibia kila kitu kuanzia uchumi hadi michezo

......
Umenishinda tabia madenge
 
b743ecc77d68475267a53056e64b3631.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom