JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha iliyokuwa ikisikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 27/2021 imepanga kwa mara ya pili kutoa hukumu hiyo.
Awali, Mei 31, 2022. Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Patricia Kisinda aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo, alipanga kutoa hukumu lakini ilishindikana kutokana na kudaiwa kuwa nje ya kituo cha kazi kwa majukumu mengine.
Sabaya na wenzake walikuwa wakisubiri hukumu hiyo endapo wangeachiwa huru au la, kabla ya kufunguliwa kesi nyingine na wenzake watano ya uhujumu uchumi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi, Juni Mosi, 2022
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Fadhil Mbelwa akiahirisha kesi hiyo Mei 31, 2022 alisema hakimu aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo amepangiwa majukumu mengine nje ya kituo cha kazi hivyo hukumu hiyo itatolewa leo.
Hukumu hiyo inatarajiwa kutolewa baada ya kesi hiyo kusikilizwa kwa miezi saba tangu ilipoanza Julai, 2021.
Sabaya alikamatwa Mei 27, 2022, Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam na kufikishwa mahakamani Juni 4, 2021 na kufunguliwa kesi mbili tofauti.
Katika kesi ya kwanza walihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, hukumu ambayo Mei 6, 2022 ilitenguliwa na Mahakama Kuu na kuwaachia huru baada ya kubaini dosari.
============================
SABAYA NA WENZAKE WAACHIWA HURU
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha imewaachia huru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya pamoja na wenzake sita waliokuwa wanakabiliwa na Kesi ya Uhujumu Uchumi.
Mahakama imesema ushahidi uliotolewa na Mashahidi wa upande wa Jamhuri ulikuwa na utata. Pia imeelezwa kuwa Hati ya Mashtaka ilikuwa na mapungufu ya Kisheria.
Hata hivyo, Sabaya na wenzake Sylvester Nyegu, John Aweyo na Nathan Msuya wataendelea kubaki Mahabusu kutokana na Kesi nyingine ya Uhujumu Uchumi waliyonayo Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi.