15 December 2023
Mahakama Kuu ya Tanzania imeagiza kusitishwa kwa mkutano mkuu wa dharura wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika TLS uliopangwa kufanyika kesho jumamosi tarehe 16 December 2023.
Amri hiyo imeyolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania masijala ya Dar es Salaam kwenye maombi madogo no. 27673 ya mwaka 2023 ktk shauri la Baltazary Bosco Mahai dhidi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Rais wa TLS mwanasheria msomi Harold Sungusia awaomba wanachama kuwa watulivu.
Picha: Rais wa TLS wakili Harold Sungusia
Rais wakili msomi Harold Sungusia asema shauri la Baltazary Bosco Mahai dhidi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali likisikikizwa upande mmoja bila TLS kuhusishwa ijumaa 15 December 2023.
Na kuwa ofisi na uongozi wa TLS ulipata taarifa ya zuio hilo saa 12 jioni ijumaa tarehe 15 December 2023 .
===
Rais wa TLS alisema kuwa kikao hicho kilipanga kujadili mabadiliko ya Sheria ya Mawakili ili kuongeza wigo wa mawakili kujisimamia wenyewe na kufanya kazi pasipo kushurutishwa.
Pia walitaka kujadili suala la Kamati ya Maadili ya Mawakili, ambayo amesema imekuwa ikifanya maamuzi ambayo yanautata wa kisheria.
Mahakama Kuu ya Tanzania imeagiza kusitishwa kwa mkutano mkuu wa dharura wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika TLS uliopangwa kufanyika kesho jumamosi tarehe 16 December 2023.
Amri hiyo imeyolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania masijala ya Dar es Salaam kwenye maombi madogo no. 27673 ya mwaka 2023 ktk shauri la Baltazary Bosco Mahai dhidi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Rais wa TLS mwanasheria msomi Harold Sungusia awaomba wanachama kuwa watulivu.
Picha: Rais wa TLS wakili Harold Sungusia
Rais wakili msomi Harold Sungusia asema shauri la Baltazary Bosco Mahai dhidi ya TLS na Mwanasheria Mkuu wa Serikali likisikikizwa upande mmoja bila TLS kuhusishwa ijumaa 15 December 2023.
Na kuwa ofisi na uongozi wa TLS ulipata taarifa ya zuio hilo saa 12 jioni ijumaa tarehe 15 December 2023 .
===
Rais wa TLS alisema kuwa kikao hicho kilipanga kujadili mabadiliko ya Sheria ya Mawakili ili kuongeza wigo wa mawakili kujisimamia wenyewe na kufanya kazi pasipo kushurutishwa.
Pia walitaka kujadili suala la Kamati ya Maadili ya Mawakili, ambayo amesema imekuwa ikifanya maamuzi ambayo yanautata wa kisheria.