Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Duh, na bado mvua inaendelea kunyesha! Hatari sana.
 
Na kati kati ya mji kunakokuwa na mafuriko yale maghorofa yalijengwa kiholela na Wananchi? Acheni kutetea hoja uzembe na ukosefu wa sera? Kule msasani kwenye mafuriko mbona zile nyumba zimejengwa kwa kibali cha Serikali na bado kuna mafuriko? Ni aje?

Yaani nyinyi wananchi mjenge holela na kuziba mitaro, mjenge sehemu za maji kupita, mvua ije maji yashindwe kupita, muilalamikie Serikali? Seriously?
 
Ha ha ha ha mkuuu mvua hii unataka wasilale? ila asante umenipa taarifa binafsi sikua najua na kumbuka hii ndio Tz ileile kwahiyo usishangae sana bana
 
Huku mikocheni inamwagika mida hii
 
Kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha usiku kucha nimepita baadhi ya mitaa alfajiri hii na kukuta wananchi wakikimbia nyumba zao sababu ya kujaa maji ndani. Inatia huruma kwa kweli, awa watu wanahitaji msaada wa haraka kutoka kwa jamii inayowazunguka sababu Serikali imeshashindwa kuwa msaada kwa Wananchi.

Nimepita maeneo ya Tabata, Buguruni, Vingunguti nimekuja kuiona tena hali hiyo Kigogo na sasa nipo magomeni sijajua kwa ndugu zangu pale Kinondoni kutakuwaje.


View attachment 249781


View attachment 249777View attachment 249778View attachment 249779View attachment 249780

muda huu jangwani daraja limefunikwa na maji, barabara ya morogoro imefungwa kuanzia magomeni, hakuna gari linaloruhusiwa kuingia mjini kupitia morogoro road.
 
Channel ten mida ya saa nne hadi tano wameonyesha habari kuhusuiana na mafuriko yalivyotokea sehemu mbalimbali dar ikiwemo pia eneo la jangwani na kufungwa kwa barabara pia walifanya mahojiano na kova etc.
 
Ya jana ilikuwa kali, nimetoka mjini posta na private car saa kumi na moja jioni, nimeingia mataa ya fire saa sita na dakika 12 usiku mbezi mwisho nikafika saa saba, saa nane kasoro ndo nilikuwa nakula chakula cha jioni. Leo sijakanyaga mjini, kama ndo na Leo itakuwa kama jana nawapa pole kwa watakao kutwa na mafoleni
 
Tuwekee picha ikiwezekana

DSC_1097.jpg
 
wa mjini tokeni mapema mtalala njiani kama mimi jana

ya jana ilikuwa balaaa, huko kariakoo ilikuwa ni full kukanyaga vinyesi vya wahindi!! mi nilitembea kwa mguu toka posta hadi mbagara!! na huku unapigwa bonge la mvua, leo nimeona isiwe tabu sitoki mengine tutajua huko huko kesho!! mzee mzima unapigwa mvua unakuwa kama kuku wa mdondo!!
 
Back
Top Bottom