Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

msimu wa mimba sisizotarajiwa...kwa wenye ndoa na wasio na ndoa aaaa
 
Znz tangia kumekucha hadi saa hizi mvua. Ya juzi hata hayajakauka bado. Shidaaa
 
DSC_0574.JPG
 
Yap best nakubaliana na wewe, lakini ukweli ni kwamba viwanja watu wanauziana kyenyeji kwa bei nafuu, na wengi hukwepa gharama za upimaji, ni watu wangapi wanaishi kwenye nyumba hata miaka 10 nyumba kiwaja hakija pimwa wala haijui hati???????????? mbona oysterbay, masaki hakuna mafuriko?????????

AL hilo la kuuziana viwanja kienyeji na ujenzi holela unadhani nani anatakiwa kulisimamia? Ni wananchi au wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi? Swala la kupimwa viwanja ni jukumu la nani? mwananchi au serikali? Anayehusika na mipango miji ni nani kati yangu mwananchi na wizara? Hebu niambie katika majiji yote Tanzania, ni jiji lipi limepangika? Ni vitongoji vingapi vimepangika? Hapo unapoishi kuna "defined dranage and sewage system?" Ni jukumu la nani kuweka city plan ? Hayo ya oysterbay na Masaki wadhani yamefanikiwa kwa sababu gani na kwa nini kwingine ishindikane?
 
Yanuhu yalianza hivihivi, watu walikuwa wakinywa na kupiga story za hapa na pale, baadaye ilivyozidi wakapanda juu ya nyumba zao, baadaye wakapanda juu ya miti, hata wajuzi wa kuogolea hawakuweza...

Tumrudie Mungu.

BACK TANGANYIKA
 
Dar Tambararee - Serikali sikivu.


Alafu wanakuambia serikali haihusiki na majanga haya. Wakati wanaacha watu wanajenga kiholela, wanaruhusu nyumba zijengwe mabondeni...hakuna master plan ya jiji..sewage and drainage system tunazisoma tu kwenye mitandao...serikali sikivu imekufa mpwa!!
 
Huku maeneo ya Kimara/Mbezi imeanza tena muda huu kunyesha mvua ya nguvu.
 
Samahani dada, umemaliza darasa la ngapi? Nata nikufowardie jinsi mipango miji inavyotengenezwa na mafuriko ni ya kawaida wala yasingetokea.
By the way. Kwa kifupi ukishindwa kuelekeza maji pa kupita maji yenyewe yanakulazimisha kupita na fidia juu. Sasa dada hilo siyo jukumu la mtu mmoja mwenye kaploti ya mita 60 kwa mita 40. Kuna mamlaka husika inayoitwa mipango miji na wizara yenye waziri, naibu waziri, katibu mkuu, wakurugenzi, wataalam wa kupima na kuratibu miundo mbinu za miji na majiji....nk...nk....sasa hawa ndo tunawatupia lawama ambao ndo inaitwa "serikali"

mmh!! kama tatizo ni mipango miji mbona kwangu mafuriko ya hivyo hakuna ila yapo zile sehemu maarufu kwa mafuriko?? jangwani kigogo kila siku wanafurikwa lakini wapo tu
 
Serikali lazima ilaumiwe kwani hata ile sheria ya kujenga mita sitini kutoka baharini haaifuati. Kutokujenga sehemu za wazi hawazifuati (huko ndiko maji yanapumulia). Kuna sheria ya kutokujenga mabondeni watendaji wanaruhusu! Mikondo ya maji haitakiwi kuzibwa lakini wananchi wanaziba na serikali inaangalia tu!
Tunahitaji serikali ya kisayansi na kama ni kuhamisha watu wahamishwe kwa gharama, waliojenga sehemu za wazi wavunjiwe mifereji ijengwe sehemu husika nchi nzima.
Ukiwa na miundo mbinu mizuri hata mafuriko yakija huwa yanaondoka baada ya muda mfupi.

NAKUPINGA KABISA % 100! Dar haijawahi na wala haitawahi kuwa ama kukumbwa na mafuriko ya maji ya mvua.
ILA Miaka yote Dar imeshuhudia MAFURIKO ya nyumba kwenye mikondo na njia za maji.
 
ndugu yangu Eli79. Huyo mwehu anayetetea serikali anamaanisha kuwa raia mwenyewe afanye hizo hesabu zoote, achore mchoro, aprove mwenyewe, mwenye kiwanja adesign sewage system ya jiji zima drainage system ya mtaa, jiji, nk......
Ni nani anayejenga au kupanga Jangwani huku akiwa hafahamu kwamba pale Jangwani kila mwaka ni mafuriko? Serikali inaweza kulaumiwa lakini wananchi wenyewe ni wapumbavu tena wapumbavu kweli kweli! Kwa wanaoishi Dar es salaama wanafahamu ugomvi usioisha kati ya serikali na wananchi wa mabondeni hususani Jangwani! Lakini leo hii ukipita mkong'oto pale na kuwalazimisha watu kuhama, baadae ni nyinyi ndio mtarudi tena hapa na kuja na hoja za haki za binadamu!!

Mistake ilishafanyika tangu enzi na enzi kwa kuwaacha watu wajenge pale and that can never reverted. The only thing serikali hivi sasa kinaweza kufanya ni kuwaambia wananchi wahame! Wakiambiwa wanajifanya kuidindia serikali na zikitumika nguvu pale, kama nilivyosema hapo awali, mtarudi tena hapa kuilaumu serikali! I am very very sorry kwa watoto wadogo wanaoathirika na maamuzi ya kipumbavu ya wazazi wao otherwise, nisingemuonea huruma mtu wa Jangwani hata siku moja anapokumbwa na hadha ya mafuriko. Visingizio vya kila siku kwamba watu hawana uwezo wa kupata viwanja vizuri. This's stupid claims coz' Dar es salaama hii kuna maeneo kibao ambayo ni very cheap lakini tatizo ni kwamba hawataki kuwa mbali na mji.

Fika pale Mto Msimbazi... yaani hata kama ni mgeni na ni kiangazi lazima utajua tu kwamba huu ni mkondo wa maji lakini watu na akili zao wanajenga humo humo! Jaribu kuwagusa uone balaha lake. Hawaoni taabu hata kwenda mahakamani kuweka pingamizi. Hii tabia yetu ya kupenda kusukumiza kwa wengine matatizo yanayotokana na upumbavu wetu wenyewe kuna siku tutakuja kuona matokeo yake!
 
NAKUPINGA KABISA % 100! Dar haijawahi na wala haitawahi kuwa ama kukumbwa na mafuriko ya maji ya mvua.
ILA Miaka yote Dar imeshuhudia MAFURIKO ya nyumba kwenye mikondo na njia za maji.

Umeona hiyo mkuu? Mvua za dar za kawaida sana tu. sasa raia wa dar watafikia hatua watalalamika nyumba zao chafu sababu serikali haiwagawii mifagio na maji ya kudekia
 
Back
Top Bottom