Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Mafuriko makubwa yaikumba Dar es Salaam

Bamaga.jpg Bamaga, leo asubuhi!
 
Tatizo kujenga ovyo bila mpangilio, kujenga mabondeni na ukosefu wa miundo mbinu ya kutolea maji wakati wa mvua,,,

Idara ya ardhi na mipango miji wanajinufaisha tu kwa kwenda kuwapimia matajiri viwanja. Eg kama wapo serious mbona hawapimi maeneo mapya na kuwasaidia raia wema kuhusu makazi bora na kuepusha haya majanga. Wanasibiri posho ya world bank ndo wanajikosha kupimapima mifereji ya maji taka na 70percent
 
Laiti ungefikiria kidogo tu ungejua serikali yako inahusika vipi na mipango miji. Lazima kuwe na master plan ya mji, lazima kabla hujaamza kujenga uwe na ramani na approval ya wizara, lazima kabla ya kujenga eneo lako lipimwe na kuonekana linafaa na kukidhi ujenzi, lazima wizara ijidhihirishe kuwa drainage system pale unapokenga inakubaliana na system ya mji, lazima sewage system ya nyumba yako iendane na sewage system ya jiji.
Unaposema sisiem isilaimiwe sijui unaangalia vigezo gani.

ndugu yangu Eli79. Huyo mwehu anayetetea serikali anamaanisha kuwa raia mwenyewe afanye hizo hesabu zoote, achore mchoro, aprove mwenyewe, mwenye kiwanja adesign sewage system ya jiji zima drainage system ya mtaa, jiji, nk......
 
kutokana na hali ya hewa ilivyobadilika katika jiji la dar-es-salaam mvua zinazoendelea kunyesha zimeathiri makazi ya wengi na kusababisha mafuriko kwenye baadhi ya mitaa.
 
Ifike wakati watu waende nje ya mji, kwani lazima kuonekana unakaa mjini ili hali unaishi kwenye bwawa la maji ya chooni???????? nyumba nyingine ni kinyaa lakini mtu anang'ang'ania hapo hapo kisa yupo karibu na kariakoo ni ujinga huo sasa. hapo serikali ya ccm haihusiki.

Samahani dada, umemaliza darasa la ngapi? Nata nikufowardie jinsi mipango miji inavyotengenezwa na mafuriko ni ya kawaida wala yasingetokea.
By the way. Kwa kifupi ukishindwa kuelekeza maji pa kupita maji yenyewe yanakulazimisha kupita na fidia juu. Sasa dada hilo siyo jukumu la mtu mmoja mwenye kaploti ya mita 60 kwa mita 40. Kuna mamlaka husika inayoitwa mipango miji na wizara yenye waziri, naibu waziri, katibu mkuu, wakurugenzi, wataalam wa kupima na kuratibu miundo mbinu za miji na majiji....nk...nk....sasa hawa ndo tunawatupia lawama ambao ndo inaitwa "serikali"
 
Samahani dada, umemaliza darasa la ngapi? Nata nikufowardie jinsi mipango miji inavyotengenezwa na mafuriko ni ya kawaida wala yasingetokea.
By the way. Kwa kifupi ukishindwa kuelekeza maji pa kupita maji yenyewe yanakulazimisha kupita na fidia juu. Sasa dada hilo siyo jukumu la mtu mmoja mwenye kaploti ya mita 60 kwa mita 40. Kuna mamlaka husika inayoitwa mipango miji na wizara yenye waziri, naibu waziri, katibu mkuu, wakurugenzi, wataalam wa kupima na kuratibu miundo mbinu za miji na majiji....nk...nk....sasa hawa ndo tunawatupia lawama ambao ndo inaitwa "serikali"

Nimemaliza darasa la 3, endeleeni kuwatupia lawama muone kama lawama ni mzigo wataota kibyongo, au mnapoteza muda tu, badala yakutafuta plan B yakuepukana na mafuriko, mtapiga sana kelele tena sana lakini hakuna mtaKACHOAMBULIA.
 
Hali ni mbaya sana, tuombe dua mambo yasizidi kua mabaya.
 
Leo asubuhi nimepita Kibasila Sec. hali ni mbaya sana na wakazi wa jirani wote hali ni mbaya, sijui itakuaje endapo mvua zitanyesha na leo. Sijui serikali tuliyonayo ipo kwaajiri ya nani?
 
Leo asubuhi nimepita Kibasila Sec. hali ni mbaya sana na wakazi wa jirani wote hali ni mbaya, sijui itakuaje endapo mvua zitanyesha na leo. Sijui serikali tuliyonayo ipo kwaajiri ya nani?

Serikali ipo kwa ajili yetu sote ila haiwajibiki kwetu. Kwa mujibu wa katiba pendekezwa.
 
Wadau mvua kubwa imeanza kunyesha tena maeneo mbalimbali.Kama Kinondoni, Posta, Temeke n.k.

Hali ni mbaya sana.

Tupeane taarifa wadau.
 
Back
Top Bottom