Mafanikio ya Rais Samia yanawatesa waliokuwa wanaomba ashindwe kuongoza nchi

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,305
9,734
Ndugu zangu Watanzania,

Mafanikio makubwa kiuongozi aliyoyapata mh Rais ndani ya muda mfupi wa uongozi wake yanawaumiza na yamekuwa mateso makubwa sana kwa Baadhi ya watu. Yameleta mateso ya moyo ,presha ,hofu,chuki,vinyongo na Dua mbaya kila uchwao. Usione watu wakiropoka ropoka na kuongea maneno utafikiri wamekatika mishipa ya fahamu ukafikiri kuna kosa amelitenda Rais Samia. jibu ni hapana bali ni URAIS Tu,Ni chuki na sumu wanayolishwa na baadhi ya watu wenye ajenda zao za siri huko mbeleni,Hivyo huwatumia wale wanaoonekana kutokuwa na breki za midomo yao kuimba nyimbo zao kama Makasuku.

Ndugu zangu Watanzania,kuna watu wangekuwa na uwezo na wakapata wa kuwaunga mkono, kwa hakika wangetamani wao ndio wawe kitini alipo Keti mama yetu mpendwa kipenzi cha watanzania. Hao watu japo unaweza usiwaone hadharani ndio baadhi yao huwatumia wale wanaoweza imba ngonjera kama makasuku kwa kutaka kupandikiza chuki na sumu katika mioyo ya watanzania kwa kutaka kuchomekea masuala ya ubaguzi kwa misingi ya Udini,ukabila ,ukanda na jinsia kama kichaka tu ili tu waone watanzania wakianza kumchukia Rais samia.

Watu hao ambao tunapaswa kuwaogopa kama ukoma na kutowaunga mkono wao na vipaza sauti vyao au vibaraka wao,wanakesha wakiomba ili Rais Samia aonekane mbaya na aliyeshindwa kuongoza nchi yetu,wanataka kumdhoofisha Rais samia kiutendaji ,wanataka aache kujikita katika kuwatumikia watanzania na kuanza kuingia katika ajenda zao,wanataka kumtengenezea ajenda wanayojuwa wapi atakwama na kumkwamisha.

Ndio maana wameinua silaha zote kuanzia silaha ya Udini,ukanda,jinsia n.k. na kwa bahati mbaya wameishia kuvunjika moyo baada ya kuona hakuna silaha yao iliyofanikiwa wala kuinuka, kwa kuwa Mungu yupo upande wa Rais samia na Amekataa kuwapa Ushindi waovu na mashetani kwa Taifa letu. Sasa wamemaliza Silaha zao na mbinu zao zote wamezimaliza na bado Rais samia anaendelea kusonga mbele kwa kishindo cha mafanikio kinachoendelea kulitetemesha Taifa letu.

Wabaya wa Rais Samia Wataungana lakini hawatashinda,watasema lugha moja lakini hawataelewana,wataongozana lakini hawatafika pamoja, watakaa vikao lakini hawatafika mwisho,watapanga mipango lakini hawatapanga ushindi,watakaa meza moja lakini hawataondoka pamoja,watashikana mikono lakini hawatagusana mioyo. Rais Samia Ni mpango Wa Mungu na mwenye kibali cha mwenyezi Mungu mkononi mwake. Vita ni ya Mungu na Mungu yupo Upande wa Rais Samia.

Uwezo mkubwa wa kiuongozi wa Rais samia, upeo mkubwa alio nao pamoja na maono makubwa aliyo nayo yanayoendelea kulipa mafanikio Taifa letu ndio maana kuna baadhi ya watu wanaishia kutukana tu matusi,kupandikiza mbegu ya ubaguzi kwa misingi ya Udini ,ukanda na jinsia.wameishiwa hoja na kubaki kutapa tapa. Wenye chuki binafsi na Rais Samia utawaona hata humu jukwaani ikianzishwa hoja au mada ya kumkashifu Rais samia unaona namna wanavyojitokeza haraka kuunga mkono na kutolea hasira zao,kwa kuwa hawana hoja zaidi ya kubakiwa na mimatusi pamoja na Ramli chonganishi na kujifanya waganga wa kienyeji wa kutabiri ya mbele Baada ya kuwa wapweke na wakiwa hasa baada ya kuona watanzania kwa mamilioni wapo bega kwa bega na Rais Samia.

Uongozi unatoka kwa Mungu,huyo ndiye amuinuaye mtu kwa sababu maalumu katika uumbaji wake katika ulimwengu wa kiroho. Kama huna kibali cha mwenyezi Mungu cha kuja kuwa Rais wa Taifa letu utahangaika mpaka uchoke,utahujumu mpaka ukoome,utaroga mpaka utatoa kafara watoto wako hadi mke na Bado utaendelea kuusikia Urais Redioni Tu mpaka unaingia kaburini.., utapanga mipango ambayo haitafanikiwa kamwe kamwe. Mungu ndiye muweza wa yote. Kama kuna mwanadamu anafikiria atamshusha Rais samia kwa chuki zake binafsi,kwa kumhujumu,kwa mipango yake ovu na michafu na ya kishetani kwa hakika atashindwa vibaya sana. Kwa kuwa kamwe na katu Shetani hajawahi kumshinda Mungu wala Giza haliwezi ishinda Nuru.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Kwa vyovyote vile wewe kuna namna uko kwenye payroll kwa kazi hii maalum ya UCHAWA, haiwezekani haya magazeti uwe unayaandika burebure tuu!!.
Siyo kila mtu yupo hapa jukwaani kwa malipo kama ulipwayo wewe kwa ajili ya kuja kutukana hapa kila siku utafikiri kichaa
 
Naona umejaza shombi na mipasho tu!!

Hembu weka hata mafanikio matatu tu aliyofanikiwa ukiacha kujenga uchumi wa kijijini kwake alipozaliwa Kizimkazi ikiwemo kupeleka mbuga ya wanyama,hotel ya kifahari na tamasha la mabilion kila mwaka.

Mafanikio mengine labda kumpa uwaziri mtoto wake(Mchengerwa)

Mfumuko wa bei wa kila kitu umefumuka,mgao wa ajabu wa umeme. Ukosefu wa ajira.

Miradi inayotekelezwa karibu yote Ni ya Magufuli,mradi mkubwa wake Ni wa kuwahamisha wamasai lloliondo na kubadiri baraza la mawaziri kila baada ya miezi kadhaa!
 
Ficha ujinga wako basi hata kwa heshima ya familia au hata wazazi wako. Ni mafanikio gani hayo ndugu chawa?
Ni mafanikio kila eneo ni ushindi kila sehemu kuanzia afya ,Elimu, miundombinu,maji,kilimo, Biashara, uwekezaji,utalii,Ajira,mapato, Demokrasia, Diplomasia n.k. nikitaka nidadavue kimoja baada ya kingine kwa hakika hapatatosha hapa jukwaani
 
Mama kashituka huyu Lucas Muoshambwa kazidi kusifia hata ambayo mama hafanya ye ni makofi na maandishi mengi yasiyoendana na mama!

Swala la teuzi sahau!
 
yeah...hata kipofu anayaona

kuwapa kesi za uhaini wanaompinga
kugawa bandari kwa wapwa wake
kuwafurusha masai kutoka ngorongoro
kufuga chawa
katiba kuwa kitabu cha kawaida
umeme wa kutosha masaa 24
kujaza wazanzibari nafasi wasizostahili bara
kumpa mkwe wake Tamisemi

wenye wivu wajinyonge.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Mafanikio makubwa kiuongozi aliyoyapata mh Rais ndani ya muda mfupi wa uongozi wake yanawaumiza na yamekuwa mateso makubwa sana kwa Baadhi ya watu. Yameleta mateso ya moyo ,presha ,hofu,chuki,vinyongo na Dua mbaya kila uchwao. Usione watu wakiropoka ropoka na kuongea maneno utafikiri wamekatika mishipa ya fahamu ukafikiri kuna kosa amelitenda Rais Samia. jibu ni hapana bali ni URAIS Tu,Ni chuki na sumu wanayolishwa na baadhi ya watu wenye ajenda zao za siri huko mbeleni,Hivyo huwatumia wale wanaoonekana kutokuwa na breki za midomo yao kuimba nyimbo zao kama Makasuku.

Ndugu zangu Watanzania,kuna watu wangekuwa na uwezo na wakapata wa kuwaunga mkono, kwa hakika wangetamani wao ndio wawe kitini alipo Keti mama yetu mpendwa kipenzi cha watanzania. Hao watu japo unaweza usiwaone hadharani ndio baadhi yao huwatumia wale wanaoweza imba ngonjera kama makasuku kwa kutaka kupandikiza chuki na sumu katika mioyo ya watanzania kwa kutaka kuchomekea masuala ya ubaguzi kwa misingi ya Udini,ukabila ,ukanda na jinsia kama kichaka tu ili tu waone watanzania wakianza kumchukia Rais samia.

Watu hao ambao tunapaswa kuwaogopa kama ukoma na kutowaunga mkono wao na vipaza sauti vyao au vibaraka wao,wanakesha wakiomba ili Rais Samia aonekane mbaya na aliyeshindwa kuongoza nchi yetu,wanataka kumdhoofisha Rais samia kiutendaji ,wanataka aache kujikita katika kuwatumikia watanzania na kuanza kuingia katika ajenda zao,wanataka kumtengenezea ajenda wanayojuwa wapi atakwama na kumkwamisha.

Ndio maana wameinua silaha zote kuanzia silaha ya Udini,ukanda,jinsia n.k. na kwa bahati mbaya wameishia kuvunjika moyo baada ya kuona hakuna silaha yao iliyofanikiwa wala kuinuka, kwa kuwa Mungu yupo upande wa Rais samia na Amekataa kuwapa Ushindi waovu na mashetani kwa Taifa letu. Sasa wamemaliza Silaha zao na mbinu zao zote wamezimaliza na bado Rais samia anaendelea kusonga mbele kwa kishindo cha mafanikio kinachoendelea kulitetemesha Taifa letu.

Wabaya wa Rais Samia Wataungana lakini hawatashinda,watasema lugha moja lakini hawataelewana,wataongozana lakini hawatafika pamoja, watakaa vikao lakini hawatafika mwisho,watapanga mipango lakini hawatapanga ushindi,watakaa meza moja lakini hawataondoka pamoja,watashikana mikono lakini hawatagusana mioyo. Rais Samia Ni mpango Wa Mungu na mwenye kibali cha mwenyezi Mungu mkononi mwake. Vita ni ya Mungu na Mungu yupo Upande wa Rais Samia.

Uwezo mkubwa wa kiuongozi wa Rais samia, upeo mkubwa alio nao pamoja na maono makubwa aliyo nayo yanayoendelea kulipa mafanikio Taifa letu ndio maana kuna baadhi ya watu wanaishia kutukana tu matusi,kupandikiza mbegu ya ubaguzi kwa misingi ya Udini ,ukanda na jinsia.wameishiwa hoja na kubaki kutapa tapa. Wenye chuki binafsi na Rais Samia utawaona hata humu jukwaani ikianzishwa hoja au mada ya kumkashifu Rais samia unaona namna wanavyojitokeza haraka kuunga mkono na kutolea hasira zao,kwa kuwa hawana hoja zaidi ya kubakiwa na mimatusi pamoja na Ramli chonganishi na kujifanya waganga wa kienyeji wa kutabiri ya mbele Baada ya kuwa wapweke na wakiwa hasa baada ya kuona watanzania kwa mamilioni wapo bega kwa bega na Rais Samia.

Uongozi unatoka kwa Mungu,huyo ndiye amuinuaye mtu kwa sababu maalumu katika uumbaji wake katika ulimwengu wa kiroho. Kama huna kibali cha mwenyezi Mungu cha kuja kuwa Rais wa Taifa letu utahangaika mpaka uchoke,utahujumu mpaka ukoome,utaroga mpaka utatoa kafara watoto wako hadi mke na Bado utaendelea kuusikia Urais Redioni Tu mpaka unaingia kaburini.., utapanga mipango ambayo haitafanikiwa kamwe kamwe. Mungu ndiye muweza wa yote. Kama kuna mwanadamu anafikiria atamshusha Rais samia kwa chuki zake binafsi,kwa kumhujumu,kwa mipango yake ovu na michafu na ya kishetani kwa hakika atashindwa vibaya sana. Kwa kuwa kamwe na katu Shetani hajawahi kumshinda Mungu wala Giza haliwezi ishinda Nuru.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Another Musiba.
Yaani humu jf ukiona mtu anaweka namba ya simu huyo lazima ni chawa.
 
Back
Top Bottom