Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Watu wenye fikra kama hizi ndio wapo kwenye vikao muhimu kama hivyo unategemea nini? Wanasema ili wasikiwe na upande wenye makali, waendelee kuwepo. Kama aliingia hapo kwa milioni 10 za Rostam hana la zaidi la kufanya zaidi ya yale aliyoelekezwa au anadhani wafadhili wa njaa zake watafurahia.
Napata shaka na upambanuaji wa mambo wa huyo mwenyekiti aliyekuwa akicheka tu,anachoweza yeye ni kucheka tu.
Nimesoma thread moja humu jamvini kwamba JK alishatonywa mapeeema kwamba kuna washenzi wamepanga dili ya kummwanga spika kupitia NEC na kiasi cha sh 50m kilipangwa kutumika kwa shughuli hiyo. Kwa hiyo mzee alikuwa anataka kuthibitisha kwa kuwaruhusu wajumbe kuropoka wawezavyo. Kama taarifa hiyo ni sahihi yawezekana kicheko cha JK katika mazingira haya (maana ana kawaida ya kucheka) kilikuwa ni sanifu tu!
 
Mkuu Filed, thanks man for the important infos, hii sasa sio siasa ni vita, mtu akifanya kitu kizuri kwa wananchi anaonekana msaliti kwenye chama cha mapinduzi, yaani hii ni mpya saaana, lakini one time light is gonna overcome the darkness, wote hao watahukumiwa kutokana na walichafanaya, the coming generation am sure itakuja kuwahukumu
 
Mimi nsipati picha hiki chama kinachotutawala kinaelekea wapi kwa kweli, ila kwa upande mwengine nina furaha tele maana naanza kuliona anguko lao takatifu likiwa linawanyemelea kwa kasi kama waliyoihaidi wakati wanataka kuendelea kututawala..... Kweli maisha bora kwa kila mtanzania ndo haya walahi vile doh....
 
lakini mimi huwa najiuliza every day, hivi wakati CCM inaanzishwa hili neno walilitoa wapi, make Tanzania kulikuwa hakuna mapinduzi ukiachilia mbali Zanzibar, sasa th majority were from the mainland (Tanganyika), where this name coming from, make ukifikiria zaidi mapinduzi yapo mengi na wao walikuwa wakifikiria mapinduzi ya aina gani? we need to storm our brains.


Lazima kuna back door iliyo na real meaning ya hili neno CCM, kifikira you may not think these guys were not serious when launching the part's name and this takes the whole scerio happening around today, someone should tell us, what does CCM means, kifalsafa naona kwa Tanzania hatukutakiwa kuwa na chama cha siasa chenye jina kama hili, lakini ni kama utakuwa unaona mbele, make mpaka sasa sijaona hayo mapinduzi kiuchumi, kijamii, nk.
 
Nahisi kosa la awali linataka kurudiwa. Kujitoa sisiemu ni kuwapa fursa vibaraka hawa na wahalifu kujitanua. Napinga kwa nguvu zote kujitoa humo. Mkakati uwe ni kubanana nao mpaka kieleweke. Sijali watakuwa wangapi lakini ingetokea wajumbe wawili au watatu wakakosoa mwenendo wa kikao kile nafikiri pangechimbika kweli. Ujasiri unahitajika kwa hili. HivI? iwapo wakiamua kuuza nchi tutanza kuhama!!!!! Tufikiri mara mbili jamani hao wamezaliwa kama sisi jitihada zao ni kujidanganya. Na zaidi hapa Bongo ndo kwetu hatuna pa kukimbilia! tusiache wapachafue kisha waondoke kwenda Canada. Sina ubaguzi lakini nafikiri kuna haja ya kukataa hizi ngozi nyeupe, zipo kibiashara zaidi na tuende mbali mpaka kwa vibaraka wao HAWANA UZALENDO kabisa
 
Hivi huyo KUSILA ni mbunge wa jimbo gani vile? Nawaonea huruma sana wapiga kura wa jimbo hilo. Hapo hamna mbunge. Kweli mtu unaweza kuuza utu wako kirahisi namna hiyo! Siamini!
 
kweli ukombozi unakaribia sana, nikizingatia maneno na msimamo wa Kada Mpinzani, FMES na sasa Gembe ninaambini hata Kibunango, Nnauye, Mwawando nk hawa ni CCM wa hapa JF, au kwa maneno mengine ni watetezi wa CCM. Sasa tutafakari kwa pamoja je kunauwezekano wa kuisafisha CCM? bora tuunge mkono chama mbadala.

Natoa wito kwenu akina Sikonge, Mtanzania na CCM wote hapa JF, ni vigumu almost impossible kutenganisha CCM na ufisadi. Come on guys, tuikomboe nchi yetu. Tambua kuwa CC na NEC wameshatoa azimio kwamba Kinana na wenzake wakutane na wabunge wote na kuwaambia shhhh!!! so, nothing will come from either Mwakyembe or Kilango which is critic to our dictatorship like government.

Mkuu,

Mie nililazimishwa kuwa na kadi ya CCM kule Msange JKT na hasa sababu ilikuwa kwamba kama huna kadi ya CCM wanaweza kukukatalia usiende nje kusoma. Kwa kuangalia mazuri na mabaya, niliamua kuinunua hiyo kadi na kuilipia mwaka mmoja yaani mwaka 1990. Hadi leo ninayo ila sijailipia. Nimeiweka kama UKUMBUSHO wangu. Sijui kama bado mie ni mwana CCM. Kwa sasa sina chama ila nikiamua basi naweza kutokea CHADEMA au kama CCM ikimeguka na kuanzishwa CCM safi.
 
Kwenye hili la Sitta's sagga na NEC, nimejifunza two important lessons, kwamba:-

1. Tanzania tutaendelea kulipia laana ya dhambi ya kumkataa Mrema, kwenye urais kwa sababu so far ana-stand tall kwa kuwa kiongozi pekee wa juu wa bara, aliyeweza kurudisha kadi ya CCM bila kufikiria mara mbili.

2. Utawala wa sasa umeanza kukubali kushindwa, kwa sababu Diria na Mwinyi walipoingia Ikulu, walijaribu sana mwanzoni kumrushia vijembe Mwalimu, lakini within time wakakwama kwa sababu hawakuwa na uwezo wa kuongoza, ndipo Mwalimu akaanza kuwachapa bakora akianzia kwenye sikuu ya wakulima Mbeya,

- Hawa Membe na Muungwana, walipoingia na wao walianza na zile zile za kumrushia vijembe Mkapa, lakini recently wamenza kunyoosha taulo la kushindwa, now Mkapa is on his way back sio siri soon na yeye ataanza kuwachapa bakora kama zile zile za Mwalimu,

Masikini ya Mungu wananchi wa Tanzania, tutawachagua tena anyways!

Respect.

Field Marshall Es

...Mrema ndio Kiongozi ingawaje ana mapungufu yake,nina uhakika tungekuwa much better kuliko hawa wa sasa hivi,tatizo la umaskini wetu ni moja tuu..CCM!
 
Kwanini unampa lawama JK wakati hao wenyeviti wa mikoa wamechaguliwa na wanachama mikoani?

Katiba ya CCM ibara 108(8) inasema wazi kuwa NEC ina kazi ya kuchunguza lawama kuhusu viongozi na inaweza kuwafukuza uanachama au kurudishia uanachama mtu. Na kama kulikuwa na watu waliotoa malalamiko kuhusu spika, NEC ilikuwa ni chombo muhimu na mwenyekiti anachotakiwa ni kuendesha tu mikutano.


Mimi naamini tangu enzi za kuchagua kilanja mkuu wa shule ya msingi, tulikuwa tukitafuta awezaye kutuongoza wooote wenye mawazo potofu na wema.

Nina maana kwamba kama Mwenyekiti wa CCM aliendelea kuvumilia matusi na yooote yasiyoendana na utawala wa sheria eti tu kwa sababu wanaosema ni wenyeviti, alishindwa kujua kazi yake ya uenyekiti.

Ukiongoza bila kujua njia na taratibu ni aibu na ndiyo maana nasema Lawama ni za mwenyekiti.
 
Field Marshall Es,
Habari zaidi kutoka kwa watu walio karibu na Rais Kikwete zilidai kwamba Kiongozi huyo wa CCM alipata taarifa zote za maandalizi ya genge hilo la kifisaidi na kwamba katika kikao chao kilichofanyika mjini hapa ndicho kilichoandaa hoja ya kumng'oa Bw. Sitta na kwamba baada ya kupata taarifa hizo, aliwatega kwa kuwaacha wafanye kila wanachotaka kwanza ili awabaini na kujiridhisha na ushahidi aliopewa.
Mkuu wangu si nilisema haya!....sikiliza sasa yote niliyosema yanakuja..nipe mji mkuu wangu!
Inawezekana alofanya JK ni upumbavu mkubwa lakini wahenga wanasema ni vizuri sana kumjua adui yako ana silaha gani badala ya kumfahamu kwa sura na umbo lake..
 
Kama mmefuaitilia saana hii, kuanzia mahojiano ya Kingunge kabla ya kikao. Alikaririwa akisema kuna mtu alikosa kupitishwa na chama kwenye kinyang'anyiro cha kuwa mgombea wa kiti cha uraisi kupitia CCM na amekuwa akileta vurugu. Sasa ukijiuliza majina ya waliogombea na ukafuatilia hii kauli ya Kusila tuliyoletewa hapa. Actually utaona mtu wanayemsema ni Tinga Tinga ( Malichela). Swali je Mzee alikimbia mawe akaenda kujificha UK?
 
Huyu Kusila asisumbue watu. NEC ya CCM siyo organ ya kisheria inayoweza kuingilia mijadala ya Bunge. Kwa kitendo chake cha kudai wabunge wakamatwe, ndiye mhanini.

Vile vile nimesikitishwa sana na kitendo cha Spika Sita kunyamazia kitendo hicho cha kudhalilishwa kwa Bunge tukufu na mtu ambaye hana mamlaka yoyote ya kisheria. Kusila kama Mwenyekeiti wa CCM wa mkoa wa Dodoma anabaki hivyo tu, hana mamlaka yoyote ya kisheria ya kuingilia maamuzi ya chombo chochote cjha kiserikali kama serikali Bunge. Ningekuwa spika ningeamuru Kusila aitwe Bungeni kuja kujieleza kwa nini asichukuliwe hatua za kisheria kwa kulidhalilisha Bunge huko NEC.
 
Kichuguu,
Mkuu wangu pale sio mahala pake.. subiri Sitta akisha vaa joho lake na amekaa ktk kiti cha Uspika.. hapo ndio utatambua Sitta nani hasa baada ya kuwa na baraka za JK!.. yaani kazi imeanza, vyama vya Upinzani vijiweke sawa maanake CCM wanaanza na kujisafisha Kisiasa kuvunja kabisa hoja kubwa ya Wapinzani -UFISADI.
Leo hii ndio the major issue ya Utawala, na CCM sii wajinga kupuuza hilo kwani umaskini wa nchi yetu unashika nafasi ya pili. Na JK ili apate ushindi mkubwa ni lazima ajikite ktk kusafisha chama hata kama iwe changa la macho!
 
Nakumbuka Kusila alipokuwa Waziri wa Mawasiliano aliwahi kupanda "chai maharage" enzi hizo ili kujua shida wanazopata wananchi kwenye daladala hizo. Nilifikiri ni mchapakazi sana.
 
wote waliokaa hicho kikao ni mafisadi tu, hakuna cha spika wala RA wote wako level moja.
 
"Kila mtanzania, kila mtu kijijini, kila mjumbe wa halmashauri ya wilaya, kila mbunge n.k lazima aweze kusema kwa uhuru bila hofu ya vitisho ama katika mkutano ama nje ya mkutano" J. K. Nyerere (1974) kwenye Binadamu na Maendeleo




"Watu wenye mawazo tofauti, hata kama wakiwa wachache, lazima wawe na haki ya kutoa mawazo yao katika majadiliano bila ya hofu ya kusumbuliwa; mawazo yao na yashindwe katika hoja za majadiliano, siyo kwa vitisho au mabavu." J. K. Nyerere (1974) kwenye Binadamu na Maendeleo
 
Hapa ndio nakupaga tano mzee wa masauti ya umeme....
 
Back
Top Bottom