- More dataz ni kwamba, baada ya Kusila kumaliza aliyepewa nafasi kuzungumza next alikuwa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar, kwa hasira kali sana Guninita alikuwa ndiye fisadi wa kwanza kudai Spika arudishe kadi yake mara moja, akiendela zaidi alisema:-
- ".......CCM tumewahi kuwalazimisha Seif na Jumbe, kurudisha kadi zao kwa kukiuka maadili ya chama chetu, sasa kwa nini tushindwe kumnyanga'anya huyu Spika na hao wenziwe kumi na moja?...."
-"........ Wakati wanatafuta hizo nafasi za uongozi kitaifa walizonazo sasa, walipitia hapa hapa NEC, tukawachuja kwamba wanafaa sasa toka wapate hizo nafasi wamekuwa wakikidhalilisha sana chama wakiongozwa na huyu Spika, huku wakivisaidia hoja vyama vya upinzani, sasa ni wakati muafaka wakarudisha kadi za chama chetu........" ".....ninasema Spika arudishe kadi sasa na wenzake kumi na moja, waende waanzishe chama chao........hatuwahitaji tena ndani ya CCM", alisema kwa hasira kali sana.
Hapa ilibidi Mzee Mwinyi, kuingilia kati ili kupunguza tention ndani ya ukumbi, lakini wakati wote huu Mwenyekiti wa CCM aliendelea kuangua kicheko chake cha awali, akionyesha kuwa very much amused na hii Cinema.
Tutaendelea tena na more dataz as soon as possible!
Respect.
Field Marshall Es!