Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

Maamuzi ya NEC ya CCM na Hatima ya Spika Sitta

CCM rasmi imeitumbikiza Tanzania kwenye mgogoro wa kikatiba na haya shime watz hasa wana JF tusikubali hali hii dhalili iendelee,na ikiwezekana na sisi tutoe"waraka wetu wenye miongozo mingi" kupinga kutishwa kwa Spika na wabunge wengine wapambanaji wa CCM.

Katiba ya Tanzania inaeleza kwa uwazi kabisa mipaka na mamlaka ya Bunge na kiongozi wake yaani Spika;HAMNA sehemu kwenye katiba inayosema kuwa "Spika akiruhusu wabunge wa chama tawala waeleze ukweli kuhusu MADHARA ya ufisadi basi ashtakiwe ama kwa uhaini au akihurumiwa basi afukuzwe uanachama",hii ni kejeli kubwa kwa demokrasia,na nakiri sijawahi ishuhudia ktk nchi yeyote ile yenye utawala BORA zaidi ya hapa Tanzania!

Sheria mama ya Bunge inaeleza wazi kuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kulishambulia bunge na mamlaka yake akiwa nje ya bunge,sheria inasema kuwa hata mbunge anatakiwa alishambulie bunge akiwa bungeni tu;na ni mwiko kwa mtu yeyote pia kupinga,kujadili na kudharau jambo ambalo tayari bunge limekwisha lipitisha na kulitolea ufafanuzi,na ukifanya hivyo unaweza fungwa jela kwenye mahakama halali za kikatiba;sasa huyu Mwenyekiti wa CCM-Shinyanga mzee Mgeja yeye sio mbunge,hii nguvu ya kulitolea ufafanuzi hata kumsimanga Spika kwa jambo lililojadiliwa na kupitishwa kihalali na wabunge kama hili la ufisadi wa Richmond amepata wapi?

Kauli ya Mzee William Kusila,ambaye ni Mwenyekiti wa CCM-Dodoma na mbunge wa jimbo la Bahi ndiyo limenishangaza zaidi!William Kusila kwa nguvu alizonazo za ubunge alipaswa kulisemea jambo hili kwenye vikao halali vya bunge,lkn akakaa kimywa na hata akakubali Richmond ijadiliwe tena mwezi Novemba,iweje sasa amshambulie Spika?

JF as a great thinker institution;we need to react as soon as possibe on this senseless mayhem,na ikiwezekana na sisi tutoe tamko rasmi na kulipeleka kwenye jumuiya za kimataifa hasa mabalozi wa nchi za Ulaya-Magharibi,Canada na USA; sehemu ambazo kwa utafiti wangu wa haraka haraka CCM huwa wanaogopa sana!

Wamefanya mambo mengi sana mabaya kwa watz,lkn hili la kulishambulia,kulitukana,kulikejeli na kulidhalilisha bunge na Spika wake tusiache lipite hivi hivi,Naam wanazuoni wote wa JF tujipange kwa hili jambo lisilo la kidemokrasia na tukichanganya nguvu na sauti zetu ni dhahili kilio hiki kitasikia nje ya mipaka ya tz na watatetemeka hawa MAFISADI!
 
Siri ya kumng'oa Sitta yafichuka https://www.jamiiforums.com/index.p...huka-&format=pdf&option=com_content&Itemid=57 https://www.jamiiforums.com/index.p...nt&print=1&page=&option=com_content&Itemid=57 https://www.jamiiforums.com/index.p...odWthLSZvcHRpb249Y29tX2NvbnRlbnQmSXRlbWlkPTU3 Majira

(Picha) Spika wa Bunge la Tanzania Bw. Samuel Sitta
*Shilingi milioni 50 zilimwagwa kummaliza
*Mrithi wake aliandaliwa kabla ya kikao
*Kikwete adaiwa kuweka mtego kubaini ukweli

Na John Daniel, Dodoma


SIKU mbili baada ya mkakati wa kumng'oa Spika wa Bunge la Tanzania Bw. Samuel Sitta, kukwama ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), siri nzito zimeendelea kubainika.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Kikao NEC kilichomalizika Jumatatu iliyopita zilidai kwamba zaidi ya sh. milioni 50 zilitumika kugawa kwa baadhi ya wajumbe kuhakisha kwamba wanasimama kidete kuhakikisha wanamng'oa Bw. Sitta na kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete aliwatega ili ajiridhishe na tuhuma hizo.

“Unajua ni wazi kwamba hawa jamaa walitumia zaidi ya sh. milioni 50 kuwagawia baadhi ya wajumbe waliowaandaa ili wahakikishe wanaibua hoja dhidi ya Sitta kwenye kiti chake, lakini bahati nzuri Mwenyekiti alidokezwa na huenda hata vielelezo kadhaa alipewa,”kilidai chanzo chetu ndani ya NEC

Ilielezwa kwamba kama mpango wa kumng'oa Bw. Sitta ungefanikiwa zingefanyika kampeni za papo kwa papo kumpata mtu wa kumrithi ambapo mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini alikwishaandaliwa kugombea na kuchukua nafasi hiyo kwa gharama yoyote ile.

“Tayari timu ya kampeni ilikwishaandaliwa kutembea nchi nzima kwa wabunge ili aliyeandaliwa apate Uspika na kazi yake ya kwanza ilikuwa ni kutangaza kwamba tuhuma zote zinazotikisa Serikali ndani ya Bunge zitajadiliwa upya au kufungwa kwa kuwa zimeleta mgawanyiko, huo ndio ungekuwa mwisho wa CCM kuongoza nchi,”kilisema chanzo chetu bila kutoa ufafanuzi wa kina wa kauli hiyo.

Habari zaidi kutoka kwa watu walio karibu na Rais Kikwete zilidai kwamba Kiongozi huyo wa CCM alipata taarifa zote za maandalizi ya genge hilo la kifisaidi na kwamba katika kikao chao kilichofanyika mjini hapa ndicho kilichoandaa hoja ya kumng'oa Bw. Sitta na kwamba baada ya kupata taarifa hizo, aliwatega kwa kuwaacha wafanye kila wanachotaka kwanza ili awabaini na kujiridhisha na ushahidi aliopewa.

Ilielezwa kwamba katika siku ya kwanza ambapo baadhi ya Wajumbe walifika mbali kwa kutoa lugha zinazoweza kutafsiriwa kuwa ni matusi kwa Bw. Sitta ndani ya NEC, siku ya pili Rais Kikwete aliwaacha wajumbe hao kujieleza kwa kina wakidhani wanatumia uhuru wao kama wajumbe kumbe alikuwa amewatega ajiridhishe na yale aliyopewa na vyombo husika vinavyofuatilia nyendo za mafisadi.

“Unajua hata hawa jamaa hawamtambui vizuri Kikwete (Rais), wanadhani ukimya wake hawaujui, jamaa anawatega tena safari hii amewapatia kweli kweli, anajua fika mipango yao yote lakini kama tunavyomjua ni mtu asiyekurupuka katika maamuzi na anafanya kwa upole, alipojiridhisha dakika za mwisho alimaliza mzizi wa fitna kwa kuunda Kamati ya kurejesha umoja na kumaliza mgongano ndani ya chama,”kilisema chanzo chetu na kuongeza;

“Ni wazi kwamba CCM sasa inataka kwenda kinyume na matakwa ya Watanzania, lakini bahati nzuri Mwenyekiti ni mwerevu sana, amekiokoa chama kufuata mkumbo wa KANU, lakini kama asipokuwa makini zaidi wanaweza kumweka pabaya mwakani, hawa wana mbinu nyingi na kila siku wanakuja na jipya.”

Habari zaidi zilieleza kwamba Kamati hiyo inayojumuisha Rais mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Bw. Pius Msekwa na Spika mstaafu wa Bunge la Afrika Mashariki Bw. Abdulrahman Kinana imepewa jukumu la kukutana na wabunge wote wa CCM na kuzungumza nao kwa undani na kuhakikisha vikao vya wabunge wa chama hicho vinafanyika vizuri na kuweka msimamo mpya wa jinsi ya kumaliza mambo mzito yenye maslahi kwa chama kupitia vikao hivyo kabla ya Bunge.

Kwa kumjibu wa taratibu za Bunge ni wazi kwamba Kamati hiyo ambayo ina watu wenye sifa za ushawishi itakutana na wabunge katika Kikao cha 17 cha Bunge Oktoba mwaka huu mjini hapa.

Majira lilipomtafuta Bw. Sitta ili kujua msimamo wake kuhusu uendeshaji Bunge kwa kasi na viwango kutokana na mashambuzi yaliyoelekezwa kwake kwenye NEC hakupatikana mara moja.

Hata hivyo habari za uhakika kutoka kwa watu waliokaribu na kundi linalopinga ufisadi zilisema hivi sasa wabunge hao wanaendelea na mikakati mizito ya kuendeleza vita hivyo kwa mbinu za kisasa.

Taarifa hizo zilidai kwamba huenda Bw. Sitta akaongeza kasi na viwango zaidi vya kusimamia Bunge na kuwabana zaidi mafisadi pamoja na mawaziri wazembe jambo ambalo litaibua hasira za kundi hilo kwa kiongozi huyo wa Bunge.
 
Rais ana sauti kubwa mno kwa tanzania kuzidi hata mahakama ya rufaa.Kama kweli angekuwa anapigana na ufisadi hili neno ufisadi lingekuwa historia.

Lakini ukirudi nyuma atamfunga je? Lowasa ama RA wakati pesa zilizochukuliwa ni yeye ndiye kanufaika nazo kuliko RA na Lowasa? yani ya kwamba yeye ni prezda.

Sema waafrika hatutaki kuwa wawazi, kwanini JK asisimame siku moja akasema jamani pesa za EPA nilizitumia kwenye uchaguzi?? Mbona watu wataelewa!!kuliko anavyopata wakati mgumu kuficha haya??
 
Magazeti yetu bwana! Yanafanana kabisa na wale waliomfungulia mashtaka ya MAUAJI ACP Zombe na wenzake huku hawana ushahidi. Hizo milioni 50 aligawiwa nani?
 
Kuna watu wengi walioko madarakani ambao kwa vitendo vyao, wamethibitisha kama hawastahili kuongoza watu. Kutetea uovu kwa nia ya kulinda maslahi binafsi haitaisadia nchi yetu.
Uovu huu tukiendelea kuulea utatudhuru sisi na kizazi chetu.Nawashangaa viongozi ambao wanapigana kufa na kupona kuona hatufanyi marekebisho ya makosa yetu ili kujenga future endelevu.
katika misingi ya uongo, nchi yetu haitosimama kamwe.
 
Salama ya watanzania imebaki ktk mambo yafuatayo:- 1, umakini wa wapiga kura, 2, tume huru ya uchaguzi, 3, kuingia mitaani kupinga udhalimu, la 1 litakuwa na maana iwapo la 2 litakuwa limefanyika, ili la 2 lifanyike vyama vya upinzani vikatae uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi, kushiri uchaguzi chini ya tume hii, ni kuwasaliti wapiga kura. La mwisho, kiongozi yoyote wa dini atakaekubali kukutana na CCM huyo atakuwa anaisaliti dini yake na Mungu wake na atakuwa ameamua kuwa mfuasi wa dini mpya inayoitwa CCM. MUNGU atawalaaani CCM na viongozi wake.
 
Kuna watu wengi walioko madarakani ambao kwa vitendo vyao, wamethibitisha kama hawastahili kuongoza watu. Kutetea uovu kwa nia ya kulinda maslahi binafsi haitaisadia nchi yetu.
Uovu huu tukiendelea kuulea utatudhuru sisi na kizazi chetu.Nawashangaa viongozi ambao wanapigana kufa na kupona kuona hatufanyi marekebisho ya makosa yetu ili kujenga future endelevu.
katika misingi ya uongo, nchi yetu haitosimama kamwe.

Nafikiri Nyerere alipoyasema haya wengi hatukumuelewa (Ukimuona mtu anakimbilia kwenda Ikulu tena kwa kutumia vijipesa kidogo, huyo ni wa kumuogopa kama ukoma-J.K. Nyerere). Wengi walijua iliishia kwa JM peke yake.....sasa leo iko live hadharani.....!
 
tunaililia mnoo CCM na sijuii tatizoo liko wapi..huenda hatujiamini na kuamini kuna mbadala wa chama hichi kwa sasa katika kuongoza taifa letuu..pili wale wote wanaopingana na itikadi za ccm hawajawa tayari kuwa wawazi kwa mioyo na nafsi zao na kujiondoaa ili kuendeleza mapambanoo huru ya kujikomboaa kutoka katika mafisadi walioshikilia hatamu za CCM.sitta na kundi lake ni sehemu ya wanasiasa wababaishaji katika kutaka tuu kujijengeaa uhalisia wasiokuwa nao wa kupambana na ufisadii kwa kuendeleaa kuogopa maisha baada ya kujitoa CCM..Sitta amepewa fursa nzuri na NEC ya kuamua vema kwa kuiweka mbele nafsi yake na masilahi ya umma kwa kujimbanua zaidi kama mpiganaji wa kweli katika vita hii ya kuikomboaa nchi yetuuu..namshauri tena yeye kama kiongozi ya wale walioitwa kundi la zecomedy katika kuwasilisha hoja zao bungeni atambue kuwa CCM sio mama yakeeeee......na hakuna dhambi yeyote kuachana nao na kuja katika uwanja wa mapambano kwa ufunuo mpyaa wa kusonga mbelee...
 
2009-08-20 09:25:00​

MOVE TO SILENCE MPs: CCM under fire
14519.jpg

Chadema secretary-general and outspoken opposition politician Dr Willibrod Slaa


Critics say party's move to rein in outspoken politicians 'unconstitutional'

By The Citizen Team

The ruling Chama Cha Mapinduzi yesterday came under severe criticism for its apparent bid to gag its MPs, who have been publicly critical of the Government and the party leadership.

Politicians, lawyers, and university lecturers accused CCM of undermining democratic institutions, including Parliament, warning that it was a serious breach of the Constitution, for which the party could be sued.

In separate interviews, they said they were surprised to learn that CCM's National Executive Committee (NEC) meeting in Dodoma last Sunday had picked a team to come up with guidelines for the conduct of its MPs, but which, they felt, amounted to measures to silence dissenting voices.

The critics cited the reported abortive bid to expel the Speaker of the National Assembly, Mr Samuel Sitta, and condemnation of other independent MPs for their vociferous criticism of corruption within the party and government on the floor of Parliament and at public forums.
The decision drew fire, with Pentecostal Church coming out in defence of Speaker Sitta. The church leadership criticised the NEC for attempting to muzzle leaders who have won public trust for their relentless fight against corruption.

Though the NEC did not name names, some of MPs who have been highly critical of their party over corruption allegations, include Ms Anne Kilango- Malecela, of Same East. She is on record as having declared that she will not let only the opposition MPs get undue credit for criticising the Government and the party on graft.

Others who have been kept Cabinet ministers on their toes over the mismangement of their portfolios, include Dr Harrison Mwakyembe (Kyela), Mr Lucas Selelii (Nzega), Ms Christopher Ole Sendeka (Simanjiro), Mr Aloyce Kimaro (Vunjo) and Mr Fred Mpendazoe (Kishapu).

Yesterday, outspoken opposition politician Willibrod Slaa, lawyers Tundu Lissu and Alex Mgongolwa, and University of Dar es Salaam lecturer Azaveri Lwaitama, were among those who censured CCM, cautioning that it could be accused of breach of the Constitution and interference in the independence of Parliament.

The party's NEC meeting chaired by President Jakaya Kikwete in Dodoma, appointed retired President Ali Hassan Mwinyi, vice-chairman (Mainland) Pius Msekwa and former East African Legislative Assembly Speaker Abdulrahman Kinana to review the role of its caucus and advise on better ways for its MPs to air their views on various issues.

The move was prompted by talk that the party and government have recently been humiliated through acts by members, including the MPs, whose condemnation of corruption was perceived to have soiled CCM's image and could undermine its chances in the national civic elections this and the General Election expected to be held in October next year.

But in response, the critics said that just like other leaders, CCM lawmakers should be free to exercise their right of freedom of speech and expression, as stipulated in Article 18 of the Constitution.

The Leader of the Official Opposition in Parliament, Mr Hamad Rashid, said the move by the ruling party was "proof that it does not respect democracy and good governance".

NCCR-Mageuzi secretary-general Samwel Ruhuza challenged the CCM politicians who felt they could not fit in the ruling party, and wanted to continue speaking and working freely for the country to decamp to the opposition.

Dr Slaa, who is the Chadema secretary-general, said:"CCM has no powers to stop its MPs from expressing their views regardless of whether they are harmful to the party or not so long as this is for the larger national interest and development."

The Karatu MP said by that questioning the conduct of Parliament, the ruling party's NEC had assumed "a role that is not theirs and infringed on the power and privileges of Parliament".

Chapter 100 of the House Powers and Privileges says: "There shall be freedom of opinion, debate in the National Assembly, and that freedom shall not be breached or questioned by any organ in the United Republic or in any court or elsewhere outside the National Assembly."

Section two of the states: "Subject to this Constitution or to the provisions of any other relevant law, a Member of Parliament shall not be prosecuted and no civil proceedings may be instituted against him in a court in relation to any thing which he has said or done in the National Assembly or has submitted to the National Assembly by way of a petition, bill, motion or otherwise."

Dr Slaa added:"I think (John) Chiligati (CCM Ideology and Publicity Secretary, who announced the NEC decision at a press conference) failed to think clearly before addressing the public about such decisions. But again it is clear that it was not by accident. Chiligati was presenting what he had been asked to say,"

But contacted yesterday, Mr Chiligati, who is also the minister for Land, Housing and Settlement Development, denied that the CCM decision amounted to a breach of the Constitution and abuse of the privileges of Parliament.

"It's not true that we have abused any part of the Constitution or interfered with the running of Parliament. Those saying so have only got us wrong because what we are doing is purely an internal party affair to clean up our own house," Mr Chiligati told The Citizen in a telephone interview.

He said they had only discussed the party's leadership ethics and conduct of its members, as "a father would do with his family to avoid washing their dirty linen in public".

He added:"Our MPs have been told that they are absolutely free to criticise the Government and air any views in Parliament. The team that we picked is only meant to help the party members understand clearly the workings of its internal caucus,"he said.

The minister said the party should not be condemned for trying to establish better working relations between the different arms of the State.

"When you see friction intensify between say Parliament and the Government, something is definitely wrong. We are not saying that either should be controlled but each of their orbits should be observed. We are saying that one should know when and how to raise issues without injuring the interests of others," Mr Chiligati said.

However, Dr Slaa charged that CCM had shown that it was unable to continue leading the country and urged voters to think seriously about whether they are gaining anything from the party.

"Speaker Sitta should relinquish his party posts to void the conflicting roles," he suggested.

Tanzania Labour Party (TLP) national chairman Augustine Mrema, who defected from CCM as a top government leader more than a decade ago, had a word of advice for aggrieved ruling party members. "Summon the courage and defect for the good of the country."

He said it would be difficult for the MPs to challenge the Government because they were adhering to the principles and rules of the ruling party.

If the MPs wanted to talk about corruption and misuse of public funds by government and CCM officers, they should quit the party.

"You cannot attack CCM while in CCM. You cannot pretend to talk about corruption while taking orders from corrupt leaders. They need to do what I did in 1992, when I accused the Government of smuggling minerals abroad and quit from the party," said Mr Mrema.

A senior lecturer at the University of Dar es Salaam, Dr Azaveli Lwaitama, said CCM was worried about its chances of winning next year's General Election if its prominent leaders continued to speak their minds about issues of national importance.

"It is quite clear that there are groups in the party that think those fighting tirelessly against corruption are putting the party in a dangerous zone in the coming elections. But as a political analyst, I know this decision will cost CCM dearly."
Dr Lwaitama, a political analyst of repute, said:"Telling people to remain silent means CCM is full of people who are intolerant to criticism, and under such conditions the party is sowing seeds of its own destruction."

Dar es Salaam-based lawyer Alex Mgongolwa said MPs did not represent any party in parliamentary proceedings and should, therefore, not be bound by their principles or rules, while in the National Assembly.

"They are there to serve people and they are under the principles and rules of the parliament, therefore CCM has no right to stop MPs from speaking in Parliament," said Mr Mgongolwa.

He said any disciplinary action within the Parliament ought to be taken according to the principles that guide the proceedings in the National Assembly.

Dar advocated and human rights activist Lissu took issue with the criticism of Speaker Sitta by his party's top organs. Said he:"I can only ask fellow wananchi to rally behind Speaker Sitta, who has stood firm against grand corruption. IIt is during his tenure that Richmond, Kiwira and EPA scandals were exposed.

One of the ruling party's MPs, who has declared he will challenge Mr Kikwete in the CCM presidential nomination, Mr John Shibuda (Maswa), declined to comment, saying he was not sure of the announcement made by Chiligati.

Reported by Tom Mosoba, Florence Mugarula and Elias Muhegera
 
Mhhhhh! ntaendelea kukamua hiyo mada,maana 'MWENGE UNAKUNYWA CHAI HAPA KARIBU NA OFISI,NA NIMEONA UNASINDIKIZWA NA MAGARI KAMA 51 HIVI.

Natanguliza heshima.
 
Nafikiri Nyerere alipoyasema haya wengi hatukumuelewa (Ukimuona mtu anakimbilia kwenda Ikulu tena kwa kutumia vijipesa kidogo, huyo ni wa kumuogopa kama ukoma-J.K. Nyerere). Wengi walijua iliishia kwa JM peke yake.....sasa leo iko live hadharani.....!

Tuna mengi ya kujifunza toka kwa Mwalimu Nyerere kwa kuwa yeye aliweza kuona mbali.Lakini mbali na hayo Watanzania tumekuwa tikihadaiwa na CCM kwamba wana sera safi na nia ya kweli ya kuwasaidia watanzania.Hilo sio jambo la kweli.

Ukweli wa CCM sasa ndio unawekwa bayana kwamba ubadhirifu, wizi na ufisadi ni sera yao na wale wote wanaojaribu kupambana nao wakiwa ndani hawafai na wanaitwa wahaini.

Isitoshe mpango walio nao ni kutufanya sisi watanzania kuendelea kuwa watwana kwenye nchi yetu wenyewe.Rasilimali za nchi hii wanagawana wao kwa wao tena kwa kutumia nguvu na sii kwa makubaliano.Isitoshe wako tayari kutumia nguvu zozote kuendelea kubaki madarakani ili waweze kuendeleza utumwa wa watanzania kwenye nchi yao.

Hii ni changamoto kwetu sote hapa JF kuwaelimisha watanzania tena kwa wingi unaowezekana ili waweze kujua kuwa wanahadaiwa na CCM.Usanii huu wa kisiasa usiposhughulikiwa sasa hakika utaendelea kuongeza mzigo mziti kwa watanzania walio wengi tena kwa vizazi vingi vijavyo.Wakati wa ukombozi na saa ya ukombozi wa dhati ndio sasa.Hatuna viongozi nchi hii tunamajambazi tuu.Kilichojiri Dodoma kwenye Mkutano wa Halmashauri kuu ya CCM kinadhibitisha haya niliyoyaweka hapa,inasikitisha.
 
Mtikila, hili nalo ni la kwenda MAHAKAMANI.
Wanasheria wetu mko wapi? Au ni kwa kuwa mnaendesha biashara ya u-advocate kinyemela, hamlipi kodi za Nchi hii?
 
Najua katiba inawalinda wabunge kwa matamshi yao bungeni, je matamshi ya hawa wahuni kwenye kikao cha chama chao yanalindwa na nani - serikali ? Kama nakumbuka Spika Sitta aliwahi kuwaonya wale wote wanaothubutu kuhoji maamuzi ya bunge mitaani - kama sikosei nadhani alikuwa anavishambulia vyama vya upinzani. Akiendelea kuonya, alisema bunge litachukua hatua kali kwa yeyote yule atakayerfanya hivyo kwa sababu huko ni kuvunja katiba.

Hivi itakuwaje kama hoja ikitolewa bungeni ya kuwawajibisha wahuni hawa waliokutana Dodoma, ama bunge halina ubavu huo. Watanzania tumepata nafasi nzuri ya kuwapima na kuwatolea hukumu inayostahili hawa wawakilishi wetu walioapa kuilinda na kuitetea katiba. Ja wataongozwa na matumbo yao kama siku zote au kama wanaume watahakikisha heshima ya bunge kama mhimili muhimu wa dola inalindwa. Wanaojiita wapiganaji, kazi kwenu.

Kwa ujinga wao hawajatambua kuwa wamevunja katiba. Natamani SS na wapiganaji wengine wapate ujasiri wa kuwashughulikia bungeni. Liwalo na liwe hata kama ni kuvunjwa kwa bunge.
 
how do they silence them?...........
unless they kill them,NO WAY FOR NOW
 
Siri ya kumng'oa Sitta yafichuka Majira

(Picha) Spika wa Bunge la Tanzania Bw. Samuel Sitta
*Shilingi milioni 50 zilimwagwa kummaliza
*Mrithi wake aliandaliwa kabla ya kikao
*Kikwete adaiwa kuweka mtego kubaini ukweli

Na John Daniel, Dodoma

SIKU mbili baada ya mkakati wa kumng'oa Spika wa Bunge la Tanzania Bw. Samuel Sitta, kukwama ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi(CCM), siri nzito zimeendelea kubainika.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Kikao NEC kilichomalizika Jumatatu iliyopita zilidai kwamba zaidi ya sh. milioni 50 zilitumika kugawa kwa baadhi ya wajumbe kuhakisha kwamba wanasimama kidete kuhakikisha wanamng'oa Bw. Sitta na kwamba Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete aliwatega ili ajiridhishe na tuhuma hizo.

“Unajua ni wazi kwamba hawa jamaa walitumia zaidi ya sh. milioni 50 kuwagawia baadhi ya wajumbe waliowaandaa ili wahakikishe wanaibua hoja dhidi ya Sitta kwenye kiti chake, lakini bahati nzuri Mwenyekiti alidokezwa na huenda hata vielelezo kadhaa alipewa,”kilidai chanzo chetu ndani ya NEC

Ilielezwa kwamba kama mpango wa kumng'oa Bw. Sitta ungefanikiwa zingefanyika kampeni za papo kwa papo kumpata mtu wa kumrithi ambapo mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini alikwishaandaliwa kugombea na kuchukua nafasi hiyo kwa gharama yoyote ile.

“Tayari timu ya kampeni ilikwishaandaliwa kutembea nchi nzima kwa wabunge ili aliyeandaliwa apate Uspika na kazi yake ya kwanza ilikuwa ni kutangaza kwamba tuhuma zote zinazotikisa Serikali ndani ya Bunge zitajadiliwa upya au kufungwa kwa kuwa zimeleta mgawanyiko, huo ndio ungekuwa mwisho wa CCM kuongoza nchi,”kilisema chanzo chetu bila kutoa ufafanuzi wa kina wa kauli hiyo.

Habari zaidi kutoka kwa watu walio karibu na Rais Kikwete zilidai kwamba Kiongozi huyo wa CCM alipata taarifa zote za maandalizi ya genge hilo la kifisaidi na kwamba katika kikao chao kilichofanyika mjini hapa ndicho kilichoandaa hoja ya kumng'oa Bw. Sitta na kwamba baada ya kupata taarifa hizo, aliwatega kwa kuwaacha wafanye kila wanachotaka kwanza ili awabaini na kujiridhisha na ushahidi aliopewa.

Ilielezwa kwamba katika siku ya kwanza ambapo baadhi ya Wajumbe walifika mbali kwa kutoa lugha zinazoweza kutafsiriwa kuwa ni matusi kwa Bw. Sitta ndani ya NEC, siku ya pili Rais Kikwete aliwaacha wajumbe hao kujieleza kwa kina wakidhani wanatumia uhuru wao kama wajumbe kumbe alikuwa amewatega ajiridhishe na yale aliyopewa na vyombo husika vinavyofuatilia nyendo za mafisadi.

“Unajua hata hawa jamaa hawamtambui vizuri Kikwete (Rais), wanadhani ukimya wake hawaujui, jamaa anawatega tena safari hii amewapatia kweli kweli, anajua fika mipango yao yote lakini kama tunavyomjua ni mtu asiyekurupuka katika maamuzi na anafanya kwa upole, alipojiridhisha dakika za mwisho alimaliza mzizi wa fitna kwa kuunda Kamati ya kurejesha umoja na kumaliza mgongano ndani ya chama,”kilisema chanzo chetu na kuongeza;

“Ni wazi kwamba CCM sasa inataka kwenda kinyume na matakwa ya Watanzania, lakini bahati nzuri Mwenyekiti ni mwerevu sana, amekiokoa chama kufuata mkumbo wa KANU, lakini kama asipokuwa makini zaidi wanaweza kumweka pabaya mwakani, hawa wana mbinu nyingi na kila siku wanakuja na jipya.”

Habari zaidi zilieleza kwamba Kamati hiyo inayojumuisha Rais mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Bw. Pius Msekwa na Spika mstaafu wa Bunge la Afrika Mashariki Bw. Abdulrahman Kinana imepewa jukumu la kukutana na wabunge wote wa CCM na kuzungumza nao kwa undani na kuhakikisha vikao vya wabunge wa chama hicho vinafanyika vizuri na kuweka msimamo mpya wa jinsi ya kumaliza mambo mzito yenye maslahi kwa chama kupitia vikao hivyo kabla ya Bunge.

Kwa kumjibu wa taratibu za Bunge ni wazi kwamba Kamati hiyo ambayo ina watu wenye sifa za ushawishi itakutana na wabunge katika Kikao cha 17 cha Bunge Oktoba mwaka huu mjini hapa.

Majira lilipomtafuta Bw. Sitta ili kujua msimamo wake kuhusu uendeshaji Bunge kwa kasi na viwango kutokana na mashambuzi yaliyoelekezwa kwake kwenye NEC hakupatikana mara moja.

Hata hivyo habari za uhakika kutoka kwa watu waliokaribu na kundi linalopinga ufisadi zilisema hivi sasa wabunge hao wanaendelea na mikakati mizito ya kuendeleza vita hivyo kwa mbinu za kisasa.

Taarifa hizo zilidai kwamba huenda Bw. Sitta akaongeza kasi na viwango zaidi vya kusimamia Bunge na kuwabana zaidi mafisadi pamoja na mawaziri wazembe jambo ambalo litaibua hasira za kundi hilo kwa kiongozi huyo wa Bunge.

Hapa ninaweza kusema, hizi ni propaganda za kumjenga Muungwana. Hakuna lolote la kuwatega. Ana Ways na Means za kupata habari ambazo nina uhakika anazo za nchi inavyokwenda.
 
CCM inapaswa kupelekwa mahakamani kwa kukiuka katiba ibara ya 100.Wananchi wa Tanzania kwa upande wao watakuwa wamefanya la mbolea sana kama wataandamana kumwunga mkono Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupeleka very clear message kwa chama cha mafisadi.
 
Hahahahahhahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa Tanzanniaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa UnafikiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiLindeni masilahi ya mafisadiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii mpaka mfe, lakini kisu chenu kipo kinanolewaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Ninawapongeza sana wabunge wote walio amua kuwawakilisaha wananchi wao ndani ya Bunge na nje ya bunge.kwa maana kwamba hawa wana mapenzi mema na chi yao.nawaomba wasikate tamaa waendelee tu kuwafichua hao mafisadi hatima ya hawa watu ipo japo ina chelewa utaratibu wetu kwa sasa ni kujarabu kuchukua takwimu ya hao wanao dhani ufisadi hauna mwisho na wanayafanya haya kwakuwa tu inchi hii ina amani kidogo wao bila kujielewa kuwa watavuruga amani hii dakika yeyote ile.Vijana tume choka.na tunakoelekea hatuta chachua viongozi kwa sera ya vyama vyao isipokuwa kwa ujasiri wao wa kusimamia maamuzi katika jamii hasa yale yanayo itakia mema taifa hiri,pia suala zima la ubunifu wa kuleta maaendeleo.sasa tuifanye mikutano iwe elekezi na wala siyo ya kutishana waacheni watu wema walitetee taifa kwa vizazi vijavyo.

Kesi inayomkabili Mbunge wa Simanjiro (CCM), Christopher ole Sendeka, ya kumshambulia James Millya jana ilianza kusikilizwa huku mlalamikaji akielezwa kwamba anaishi nyumba ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Millya ambaye ni shahidi wa kwanza kwa upande wa Jamhuri alijikuta katika swali gumu la kueleza nyumba anayoishi ni ya nani baada ya upande wa utetezi kuanza kumhoji baada ya kutoa ushahidi wake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Wakili wa upande wa utetezi kutoka kampuni ya The Professional Center, Kamara Mpaya, alimtaka Millya aeleze pamoja na mambo mengine anakioishi na ni nyumba ya nani. Mahojiaono hayo yalikuwa kama ifuatavyo:

Wakili: Nyumba unayoishi ni ya nani?
Shahidi: Sijui.

Wakili: Nikikuambia ni ya Lowassa utakataa?
Shahidi: Siwezi kukubali wala kukataa. Kutokana na jibu hilo watu waliokuwa wamefurika mahakamani wakifuatilia kesi hiyo, waliangua kicheko.

Mafisadi hawataki waguswe hata kidogo na hii ni upuuzi mtupu, tutaendelea kuwafuatilia popote walipo na kuanika uchafu wao wote.
 
Nadhani Ole sendeka na Selelii wanasakamwa sana hii ni kutokana na Serikali Ya CCM kushindwa kuendesha nchi. Wizi umezidi mno kila idara ni ufisadi tu. Hii nchi inatisha kwa afrika jamani pia SPIKA WA BUNGE njoo chadema na wanaCCM mashuhuri mje CHADEMA jamani tuiondoe CCM maana tumechoka na kutishwa pia Hivi CCM hawaoni kama Watz tunauelewa sasa na si enzi za Mwl Nyerere na MKapa. Internet, SIMU ZA MKONONI na MAgazetu zitasaiidia kuikomboa hii nchi!!

NI Mtazamo na maoni wenzangu mnasemaje na haya mambo ya wana CCM kutishia watu wanaojalibu kufichua maovu hata Kingunge kutisha kuhusu waraka wa katoliki hana jipya maana hata kipindi kile DR Slaa na Tindu Lisu wanataja mafisadi alidai wanatafuta umarufu, Bora Acha na ale ugali tu.

mimi sikuungi mkono kabisa kuwa Bw Sitta na wabunge wote wanaotetea wananchi waingie upinzani kwa sasa, kwa kweli ni bado sana kwa vyama vya upinzani havijasimama vizuri japo kunauelewa mkubwa wa wanachi kuhusu upinzani kwa sasa,
dawa ya hawa wakina Sitta ni kukimaliza chama wakati bado wakiwa ndani ya chama, mchwa hawezi kumaliza mbao kama hakiwa nje , bali akiwa ndani ya mbao, inatakiwa wakiyumbishe chama wakiwa ndani mpaka mpasuko wa maana uonekane kabisa, na hapo ndio ule upinzani wa kweli utakapoonekana
 
Back
Top Bottom