Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Kauli hii ya "Hakuna mchezaji atakubali kucheza second fiddle kwa Salah Bobby au Firmino" ikimaanisha kwamba hawa ndiyo wachezaji bora Duniani hakuna wa kuwazidi uwezo, nimegundua kuwa hayakuwa mawazo ya wanayoisema bali ni Watu waliokuwa Brainwashed na wale MosDef anaowaita Top Reds.

Top Reds walioanzisha kauli hii kwa lengo la kuwalinda FSG na Wachezaji wao vipenzi ili wasijekusajiliwa wachezaji wazuri wakachukua namba zao.
Hivyo washabiki wa Liverpool waliokuwa fooled na hii kauli wakawa wanaitumia kila sehemu.

Baadae wakataka kumtoa Kafara Salah juu ya kufungwa kwetu, sasa wanataka kumtoa Kafara Thiago kwa kufungwa kwetu.
Top Reds my foot... Hatuna depth kwenye squad yaani unatoa Salah anaingia headless Ox, unatoa Mane anaingia Blunt Origi.. Yaani hatuna like for like subs hivyo ikitokea wachezaji wa 1st 11 wameshuka kiwango ama majeruhi basi tumekwisha kama hali ilivyo sasa almost kikosi kizima kimechuja na hatuna plan B kwani waliopo bench ni uozo mtupu... Ki ufupi Klopp hana benchi la kumtoa alipo sasa ndio manaa anakomaa nao mwanzo mwisho.. Tazama hata kwenye media anasema yeye ndio apewe blame kwa kushindwa kupata winning mentality na sio vijana anajua fika hata akiwalaumu hana benchi la kumsapoti hapo hapo...mpaka pale Jota atarejea na ukali ule angalau atakua na new e dimension pale mbele na pale nyuma kwa sasa ni ku test waliopo combination ipi itamsaidia.. Pale kati wamekua pedestrians yaaani hakuna cha Gini wala nani bila Fabinho playing DM wote tutawaona hovyo maana wanajikuta na majukumu ambayo sio yao.

Kama kuna wachezaji hua ni ngumu kua replaced kwenye timu ni DMs yaani hawa hua pengo lao halizibiki kirahisi tazama Makelele pale Real Madrid, Maschereno Liverpool, Kante Leicester, Fabinho Liverpool, Keane MNU, Viera Arsenal, nk. Kwa sasa hatuna DM to slow down attacks na pia wa dictate play allowing fellow MFs kupeleka support forward.

Husikii Top Reds wakisema pengo la Fabinho lilivyo kubwa kiasi hata ulete Thiago na Gini hawawezi kulizimba. Hao Top Reds wanakomaa na Hendo arudi MF eti tumepoteana kwa vile hayumo pale kati like serious.

Fabinho is the unsung HERO yaani sasa ndio kazi yake inaonekana ya DM.

YNWA
 
Namuheshimu Sana Klopp.Infact Kwangu ndiye kocha ambae ameleta mafanikio makubwa zaidi Liverpool katika kipindi cha miaka 20 iliyopita.Ndiye kocha ambae amerudisha ukubwa wa Liverpool,heshima ya Liverpool na ametuletea mvuto ambao unawafanya wachezaji nyota kabisa kutaka kucheza Liverpool.Makampuni makubwa kama Nike sasa yanafanya kazi na Liverpool..Hauwezi kutenganisha hivi vitu na Klopp...

Lakini Klopp huyu nae kuna muda anazingua Sana.Kitu kimoja cha uhakika ambacho Klopp anazingua ni kuendelea kutumia 4 3 3 wakati anazo sababu za msingi za kubadili mfumo.Injuries za mabeki, kushuka viwango kwa full backs na hata front three na kuwa na wachezaji ambao ni wazuri kwenye mifumo mingine kuliko 4 3 3.Hizi zilitakiwa kuwa sababu za kufanya mabadiliko ya shape ya timu kulingana na opponent.Takumi,Thiago,Keita,Gini,Origi etc ni wachezaji ambao wanaweza kuonekana flops kwenye mfumo wa 4 3 3 lakini wakawa wazuri zaidi kwenye 4 2 3 1 au hata 4 4 2.Sasa kwa nini usitumie huo mfumo ambao utakufanya upate asilimia zaidi ya 80 za ubora wa mchezaji na badala yake unaamua kukomaa na mfumo ambao unaupata ubora wa mchezaji yule yule kwa asilimia 20?Unafanya makusudi Ili aonekane ni flop?

Hata hao akina Mane ,Salah sometimes tunawaonea tu kuwakosoa.Wamecheza Sana mfululizo bila break na kocha hataki kutumia wachezaji wengine kwenye mifumo inayowasuit zaidi.Rotation ilitakiwa kuhusika Sana baada ya majeruhi huku mfumo ukiwa unabadilika mara kwa mara Tusingekuwa ambapo tupo sasa hivi..

Bado Hizi lawama zangu kwake haziondoi heshima kwake kama nilivyoeleza para ya kwanza...
Mkuu tutasema mengi na tutasema sana hata Klopp anakumbali kukoselewa kwa hayo yanayoedelea uwanjani sasa.. Upande mmoja yanamhusu kua muumini wa kikosi kindogo hili ni yeye maana kama kikosi kiwe kiduchu basi kiwe quality nk.. Depth iliyopo pengine kwa kukumbali kulipwa bei chee na FSG ni dead woods wote ukimtoa Jota. Zimepita dirisha nyingi tu na alikua ana uwezo wa kuwatoa akina Origi nk yeye aliona wanafaa sasa anayaona.

Kingine tunacheza high intensity hivyo wear and tear will catch up na wa madogo one way or the other.

Kingine uzoefu tazama goli la pili dogo Phillips alivyopitwa kurahisi naamini pale VVD asingepitwa vile kwa vile ange anticipate nini kinafuata.. Hata goli la kwanza Kabak was caught with a clear cut pass ya James pia pale kwa VVD na Fabinho akiwa DM sidhani kama ingekua that easy to pass and score..

Kingine losing is addictive haha just like winning is addictive.. Yaani Klopp ana kazi sana kibarua haswa kuwajenga upya vijana wacheze as unit na wawe na subira kushambulia only when they are sure kuliko sasa we are losing many useless passes kutoka kwa Robbo na Trent.

Mpaka sasa ishajulikana bila VVD Gomez pale nyuma ni ngumu kua challengers hivyo kwa sasa tukomae tubakie kwenye BIG 4 if we are lucky na tujipange kwa ajili ya next season maana next season itakua ngumu zaidi Manchester City Pep anapewa £200m kuingia sokoni ana mpango wa kuwaleta Lukaku na Martinez kutoka Inter au Hallad kutoka Dortmond, pia Grealish na Traore wote wanatajwa huku pia Messi akitajwa tajwa.. Hivyo Juni Edwards inafanya clear out ya nguvu uza Gini, Matip, Philips, Milner, Hendo, Shaqir, Chamberlain, Keita na mmoja ama wawili katia ya Firmino, Mane au Salah. Kama kweli lazima kuuza ili kununua basi we have to sell our worthy players pale mbele tupate ela kujenga kwingine design kama ya Coutinho.. Zipo tetesi FSG wanapeleka Salah na ela kumpata Mbappe haha come June tuone niaje.

YNWA
 
Adjustments.jpg
 
Aaa kumbe upo.
Hivi kuwa tapeli na uongo unakusaidia nini?Hiyo pesa ni ndogo sana kwa aina ya mtu uliyemfanyia.

Halafu ulikuwa unataka namba yake ya nini sasa?Na wewe awe anakupa hela kama mie?


.
Mkuu mlivyopeana sisi hatukujua inakuaje unakuja kupost Mambo binafsi kwenye jukwaa Kama hili.... Ustaarabu kitu Cha bure.

Sent from my M1 Lite using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Ollachuga Oc wakati msimu unaanza ulikua hakauki humu na sifa wewe ndio bingwa mtarajiwa 2020-2021 lakini baadae hayo maneno ukanywea wala hukusema tena... Hayo ndio maisha ya soka unakua na wakati mwema kipindi fulani na wakati mbaya nyakati zingine. Tupo vimbaya kwa sasa wala hatuna cha kusingizia.. Pamoja na yote wote ni BIg 4 contenders hivyo tuchekani sasa ila mpaka mwisho wa msimu tutaona nani atacheka mwisho.

He who laughs last is the winner.

Surez ana jambo na Les Blue na kwa vile ana historia na nyinyi itakua powa sana awazime.

YNWA
Kabisa

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom