Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Adjustments.jpg
 
Kuna siku Don Clericuzio alihoji kuhusu usajili wa hawa KABAK na DEVIES kuwa Je, ndiyo wachezaji wa kutupa Makombe EPL na CL?
Dah! Wanazi walimuona anamkosoa Klopp ambaye anajua zaidi kuliko Don.

Naamini wameshaanza kuelewa

Hahaha, acha mzee.

Niliambiwa habari za kina Robertson, Gini, Robbo nk. Kwamba na wao walikuwa hivyo.
 
Watu tunajisahau sana
Hivi teams kama Man City au Man U au LC mwaka jana zilifanya nn la maana wkt Liva anachukua ubingwa mechi 8 mkononi?
Hii ni soka ina ups and downs
Livapool HALISI tuendelee kuwa nyuma ya Klopp,kila team ina mapito EPL hamna jipya ambalo Liva anapitia leo hazijapitia teams zingine
 
Hahaha, acha mzee.

Niliambiwa habari za kina Robertson, Gini, Robbo nk. Kwamba na wao walikuwa hivyo.
Aaa kumbe upo.
Hivi kuwa tapeli na uongo unakusaidia nini?Hiyo pesa ni ndogo sana kwa aina ya mtu uliyemfanyia.

Halafu ulikuwa unataka namba yake ya nini sasa?Na wewe awe anakupa hela kama mie?


.
 
Hahahahahahahahah........umeanza kutafuta Excuse sasa kama ilivyokuwa kwa Adrián ,Origi ,Gini ,Henderson umehamia kwa Kabak na Davies ......... Alcantara yeye ameongeza nini kwenye timu mpaka sasa mnawapotezea kama hamuwaoni vile kwa sababu ni Favourite sio.

Kaka kama ninaielewa vizuri definition ya excuse basi wanaotafuta excuses ni wale wanaosema tunafungwa kwasababu hatuna VVD, Hendo anachezeshwa nje ya Sehemu yake, na blah blah nyingi! Lakini mimi nilishaweka wazi kuwa hakuna kisingizio bali hili Timu ni bovu.

Kuhusu Thiago nilishaweka wazi kuwa niliacha Tabia ya kulaumu mchezaji mmoja mmoja kwani Timu nzima ni mbovu mpaka mbinu za kocha zisizobadilika pia ni mbovu.

Kwasasa mimi nimejikita kwenye kukosoa usajili tu, hivyo kwa Thiago mimi sina sababu ya kulaumu usajili wake kama nilivyokuwa silaumu usajili wa Keita na OX ingawa ni Failed projects. Unajua kwanini?

Ni kwamba sikuwa na Uchawi wowote wa kuniwezesha kujua kuwa wachezaji hawa wakija Liverpool watafeli.

Hata kama unamchukia vipi lakini huwezi kubisha kuwa Thiago wakati yupo Bayern alikuwa ni WC na best Midfield, kufeli Liverpool sio kipimo cha kulaumu alikotoka. Lakini sajili ya Mtu kama Mfano Ben Devies hii ni Wazi kuwa tumeokota tu huku tukijua hawezi kutusaidia chchote.
 
Mkuu Ollachuga Oc wakati msimu unaanza ulikua hakauki humu na sifa wewe ndio bingwa mtarajiwa 2020-2021 lakini baadae hayo maneno ukanywea wala hukusema tena... Hayo ndio maisha ya soka unakua na wakati mwema kipindi fulani na wakati mbaya nyakati zingine. Tupo vimbaya kwa sasa wala hatuna cha kusingizia.. Pamoja na yote wote ni BIg 4 contenders hivyo tuchekani sasa ila mpaka mwisho wa msimu tutaona nani atacheka mwisho.

He who laughs last is the winner.

Surez ana jambo na Les Blue na kwa vile ana historia na nyinyi itakua powa sana awazime.

YNWA
Mkuu bado point chache tu tumtoe city pale juu ..hilo liko wazi kabisa mkuu ..hiyo kazi tuachieni sisi kwa kuwa nyie mumeshindwa, basi hawa city boys hawafiki popote ..kufikia april kila kitu kitakuwa katika mstari unaotakiwa ..maneno yangu bado yapo pale pale .."sisi ndio mabingwa wa EPL msimu huu wa 20/21" tutawashangaza kweli kweli.
#CFC

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Sasa bila kificho nadiriki kusema wazi kabisa usajili wa THIAGO AĹCANTARA ni usajili ambao hauna faida kwa Liverpool.

Tumepigwa za uso Mchana kweupe.

Eheeee! Hivi ndiyo inavyotakiwa na ndiyo maana sahihi ya kuwasilisha mawazo yako. Usisubiri mawazo yako akuwasilishie Mtu mwengine.
Hapa umefanya la maana sana kukosoa kile unachohisi hakikua sawa! In case tukijafukua makaburi unakuwa wewe kama wewe.

Chamsingi ukikosoa mawazo yako yawe huru, usikosoe tu kwasababu kuna Mtu kamkosoa mchezaji ambaye unahisi hakupaswa kukosolewa ndio ukaamua kujibu mapigo na wewe kukosoa ambaye yeye hajamkosoa! Huko si kukosoa kimpira bali ni visasi.
Mfano Mtu aonapo tu anakosolewa Origi ndiyo nayeye anakuja na makala ya kukosoa wengine. That's not a football.
 
Sasa bila kificho nadiriki kusema wazi kabisa usajili wa THIAGO AĹCANTARA ni usajili ambao hauna faida kwa Liverpool.

Tumepigwa za uso Mchana kweupe.
Thiago tumepigwa boss.
Jota naona wazi wazi tulipigwa.
Minamino nako hivo hivo ila bado kuna namna ya kufidia hasara
Kwa ufupi huu msimu tumepigwa hahahahahahahahahahaha..

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Tena ilikua inasemwa hakuna mchezaji atakumbali kucheza second fiddle kwa Salah Bobby au Firmino na maneno mengi mengi.

FSG mpaka sasa hua ni ngumu kuelewa kama kweli wanaelewa uwekezaji wa kujenga kikosi cha ushindi endelevu. Hawa jaama mara ya mwisho kutoa mkopo wa kununua mchezaji hata sikumbuki ni lini. Wao wametoa mkopo ama kudhamini mikopo kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa Anfield na mkopo pia kwa ajili ya New Training ground AxA. Huu wa kujenga Anfield nadhani wanaanza kulipwa Mwaka huu.

Ukitazama wanavyosajili hawa watoto utaona ni dhahiri hawa wanafuata mbinu za uwezekazaji wa Red Bull teams. Na taarifa wamefanikiwa kwa mfano kwa Solanke walimnunua bei chee wakaja uza bei kubwa, na pia Hoever vile vile design kama hio. Kwa sasa zipo tetesi wanatafuta timu nyingine Ulaya wanunue ili iwe kama feeder club ya Liverpool. Haha hii yote wanakimbia kutoa mamilioni kama vile wanavyofanya Chelsea na Manchester City. Ukitazama tangu 2015 mpaka sasa kwenye usajili Manchester City wametumia zaidi ya £800m kununua wachezaji. Tazama table hapo chini.
View attachment 1707922

Liverpool wamenunua wachezaji wa £470.9m na wameuza wachezaji wa £378.5m ina maana ela iliyotoka klabuni kwenye akiba ni £92.4m., sasa tazama kwa Manchester City £505.6m ilitoka klabuni maana mauzo yao ya wachezaji sio makubwa. Hii ni balaa kwani wao kununua mchezaji wanaemtaka sio lazima kuuza ndio kununua kama Liverpool wanavyofanya na hii inawapa consistency ya ku challenge top honours kwani kikosi kimesheheni super talent.

Ukitazama net spent per season ni £18.5m yaani hawa FSG wao ni kuvuna tu.

Imagine Origi ndio tegemeo letu kuturudisha BIG 4 jamani like serious. Ki ukweli wachezaji wazuri hujulikana pale timu ipo vimbaya lakini wao wana shine kuokoa jahazi tuliona sana hayo kwa Steve G, Messi, Ronado, Bruno nk.

Liverpool kwa sasa wachezaji wote wamepoteana hata zile instinct za pasi hazipo kabisa.

Tunabitaji Edward awe na Juni bizy kweli kweli kuturudisha kwenye ukali. Hii shinda ya ku unlock deep playing teams lazima watafute jawabu kama Thaigo ndio jawabu basi mfumo uwe flexible kwake ili tuone kazi yake.

Yajayo yanatisha.

YNWA

Kauli hii ya "Hakuna mchezaji atakubali kucheza second fiddle kwa Salah, Mane au Firmino" ikimaanisha kwamba hawa ndiyo wachezaji bora Duniani hakuna wa kuwazidi uwezo, nimegundua kuwa hayakuwa mawazo ya wanayoisema bali ni Watu waliokuwa Brainwashed na wale MosDef anaowaita Top Reds.

Top Reds walioanzisha kauli hii kwa lengo la kuwalinda FSG na Wachezaji wao vipenzi ili wasijekusajiliwa wachezaji wazuri wakachukua namba zao.
Hivyo washabiki wa Liverpool waliokuwa fooled na hii kauli wakawa wanaitumia kila sehemu.

Baadae wakataka kumtoa Kafara Salah juu ya kufungwa kwetu, sasa wanataka kumtoa Kafara Thiago kwa kufungwa kwetu.
 
Mkuu bado point chache tu tumtoe city pale juu ..hilo liko wazi kabisa mkuu ..hiyo kazi tuachieni sisi kwa kuwa nyie mumeshindwa, basi hawa city boys hawafiki popote ..kufikia april kila kitu kitakuwa katika mstari unaotakiwa ..maneno yangu bado yapo pale pale .."sisi ndio mabingwa wa EPL msimu huu wa 20/21" tutawashangaza kweli kweli.
#CFC

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Mkuu upo siriazi kabisa unamtoa Manchester City pale alipo hivi ni kwenye play station ama hii ligi hii unayogombania kuingia Big 4.

Huo uwezo hamna ndugu sio wakati huu.

YNWA
 
Hahaha, acha mzee.

Niliambiwa habari za kina Robertson, Gini, Robbo nk. Kwamba na wao walikuwa hivyo.

Kauli kama hizi ndiyo zinazofanya sote Washabiki wa Liverpool tuonekane ni wa kukariri tu! Kwasababu tu Watu wamekariri Gini na Robbo walitoka Timu zilizoshuka Daraja basi imehalalisha kila tunayeokota kwa Vibonde ndiyo atakuwa kama Gini na Robbo.

Hivi kwasababu tu Suarez tulimnunua Ajax ndiyo kila tutakayemnunua Ajax atakuwa kama Suarez?

Watu tuache kukariri haimaanishi Relegators wote ndiyo wanawamiliki kina Gini na Robbo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom