Captain Marvelous
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 15,313
- 32,605
Duuh kweli tulikotoka panatisha mno wachezaji enzi kuja team ya nafasi ya 7 mpaka 10 ilikua ishu sana kuwavuta wengi walitugomea kwa vile hatukua na UCL lakini leo hii mpaka wachezaji kama Mbappe tunatajwa kuwataka kweli maisha yanakwenda kasi 5G...Captain kama huyu alicheza na mabeki wa kati kama Skirtel na Kaygriakos.
Alicheza na mabeki wa pembeni ka Arbeloa na Emily Insua.
Alicheza na Viungo kama Lucas Leiva na Jordan Henderson.
Alicheza na Washambuliaji kama Voronin na David Ngog.
But still alimanage kutupa chochote kupitia jitihada binafsi.
Wakati wa shida yeye ndiyo anashika hatamu ya mapambano.
Huyu Captain hakupata bahati ya kucheza na Liverpool ya kina VVD, MANE, SALAH, ALISON, FABINHO, TAA na ROBBO.
Enzi hizo wachezaji wetu ni Downing, Charie Adams, Jerry Spearing, Insua, Peter Crouch nk bado tulitulia tulii tukijua kuna siku tutakaa sawa na kweli baada ya kutua Klopp tupo sawa na huu wa sasa ni upepo utapita tu...
Hakika kumfananisha Steve Gerrard na Hendo ni kama kufananisha usiku na mchana...
Hendo ana bahati amezungukwa na wachezaji wenye talanta bora kabisa zaidi yake na anacheza chini ya kocha bora kabisaaaa... Hii bahati Steve hakuipata.
YNWA
