Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mashabiki wa livakuku mbona munalazisha ligi isimame?
Wachezaji walianza kulazimisha VAR isitumike utafikiri haikuwapa ubingwa msimu uliopita..

Mpango ulivyofeli wakaja na project ya kujihakikishia hawarudi tena Misri.

Project imefeli wakaanza kusema ligi isimame.

Mpango huu ukifeli lawama zitaenda kwa hali ya hewa na majeruhi.
 
Nitatofautiana na mtazamo wako kidogo, msimu uliopita timu zilikuwa sawa sawa na msimu huu, isipokuwa Liverpool alikuwa Bora Sana.

Mpaka game ya 17, Liverpool alikuwa ameshinda 16 na ametoa draw 1, points 49 hizo out of 51. Wanaomfatia walikuwa na points kama hizi tulizoko sasa hivi.

Katika mtazamo mwingine ambao nakuondoa kwenye watu wa mpira, ni kusema eti Klopp hana ufundi wowote isipokuwa anawakimbiza wachezaji. Huu ni mtazamo wa kishabiki au wa mbumbumbu wa mpira.

Unapigia mbuzi gita
 
Paragraph ya mwisho ilibidi ni-apply uNgwaba.

Unakumbuka kuna posts zilizopita niliwahi kumgusia TAA mara kadhaa kuwa kashuka kiwango ambaye ndiye mtengenezaji nafasi wetu mkubwa?
Unalionaje hili? Coz Watu hawapendi kutaka kujua msingi wa Tatizo.

Sasa tuendelee kushuhudia between 0 to 2 on target kwa kila game.
 
Unakumbuka kuna posts zilizopita niliwahi kumgusia TAA mara kadhaa kuwa kashuka kiwango ambaye ndiye mtengenezaji nafasi wetu mkubwa?
Unalionaje hili? Coz Watu hawapendi kutaka kujua msingi wa Tatizo.

Sasa tuendelee kushuhudia between 0 to 2 on target kwa kila game.

Trent ni kweli baada ya kutoka majeruhi hajawa yule Trent tunayemfahamu, very unfortunate siyo mkabaji mzuri, kwa hiyo akikosa makali kwenye kushambulia anakuwa garbage.

Kuna muda nikawa natamani kipangwe kikosi cha maajabu, Milner akae namba 2, Trent apande juu wing ya kulia (acheze kama kiungo). Sasa wa kumweka benchi hapo ndo nikakosa.

Point ni kuona kama akipewa jukumu moja tu ataweza kurudisha makali yake kwenye kushambulia?
 
Unakumbuka kuna posts zilizopita niliwahi kumgusia TAA mara kadhaa kuwa kashuka kiwango ambaye ndiye mtengenezaji nafasi wetu mkubwa?
Unalionaje hili? Coz Watu hawapendi kutaka kujua msingi wa Tatizo.

Sasa tuendelee kushuhudia between 0 to 2 on target kwa kila game.

Hasa game za ugenini.
 
Ukifanya analysis ya timu moja kwa game 17 za mwanzo last season na season hii, ni Manchester United peke yake ambaye anakuwa na +.

City anabaki alipo (assuming viporo vyake ameshinda)

1. Liverpool: 49 kwa 33: -16

2. Leicester: 39 kwa 29: -10

3. Manchester City: 35 kwa 35 (assuming viporo ni ushindi): 0

4. Chelsea: 29 kwa 26: -3

5. Spurs: 26 kwa 26: 0

6. Manchester United: 25 kwa 36 (kama akishinda kiporo chake): +11.

Doesn't this tell you something?

With that look, ni kwamba Liverpool amedrop sana.

Man Utd yuko on the massive plus. City yuko alipokuwa mwaka jana.

Ndo maana nikasema, bado timu ziko pale pale isipokuwa Liverpool kashuka sana.

Unanikumbusha zile posts zangu za mara kwa mara ninazosema kuwa Washabiki wengi wa mpira hawapendi kutumia Takwimu badala yake wanaongelea hisia.

Mtu anakwambia Ligi mwaka jana Timu zilikuwa mbovu! Ukimuuliza katumia vigezo gani basi hana! Lakini angelikuwa anatumia takwimu basi angejua kuwa msimu uliopita na huu hauna tofauti kwa Timu zote isipokuwa Liverpool na Manure.

Liverpool kashuka kiwango
Manure kaongezewa kiwango

Watu wajifunze kutafsiri takwimu
 
Hili jukwaa naona tumevamiwa ila pamoja na yote bado tupo kwenye nafasi ya kupambana YNWA

Swala la muda tu wataondoka tu hao .tuna nafasi kubwa sana.bado tunasifa zote za kuwa bingwa.

Kelele zao hao mashabiki wa Manyumbu zisikutishe mkuu. Kuongoza hata ligi wajaongoza wanaleta kelele kama wamechukua ubingwa.
 
Hasa game za ugenini.

Hapa ndiyo inakuja ile kauli ya kuwa Klopp hana Plan B.

Klopp ni Kocha bora sana lakini with limited Plan ya only attacking by using Fullbacks.

Plan B ilikuwa iwe ni kuswitch from using Fullbacks to Midfielders! FBs zetu zinapopotea alikuwa atumie Midos kucreate nafasi using Center of the pitch hiyo ndiyo Plan B, but kwa Mido gani?
 
Trent ni kweli baada ya kutoka majeruhi hajawa yule Trent tunayemfahamu, very unfortunate siyo mkabaji mzuri, kwa hiyo akikosa makali kwenye kushambulia anakuwa garbage.

Kuna muda nikawa natamani kipangwe kikosi cha maajabu, Milner akae namba 2, Trent apande juu wing ya kulia (acheze kama kiungo). Sasa wa kumweka benchi hapo ndo nikakosa.

Point ni kuona kama akipewa jukumu moja tu ataweza kurudisha makali yake kwenye kushambulia?

TAA ni aina ya Wachezaji kama alivyokuwa Coutinho, akitoka injury inamchukua muda kugain his confidence.
Tofauti na Matip anatoka injury leo tena ya muda mrefu na anaperform vizuri tu.
 
Swala la muda tu wataondoka tu hao .tuna nafasi kubwa sana.bado tunasifa zote za kuwa bingwa.

Kelele zao hao mashabiki wa Manyumbu zisikutishe mkuu. Kuongoza hata ligi wajaongoza wanaleta kelele kama wamechukua ubingwa.

Kwenye kila msimu Timu zina kawaida ya kufika kipindi zikawa zinadrop points ambapo sisi mara nyingi ilikuwa ni Jan - Feb.

Sasa mara hii imetokea December, Sasa hawa wanaopiga kelele hapa itafika kipindi chao nao kudrop points tena kwenye kipindi kibaya zaidi cha round ya pili ambapo sisi tayari tutakuwa tumesharudia mchezoni hapo ndiyo watakapokimbia wote hapa.
 
TAA ni aina ya Wachezaji kama alivyokuwa Coutinho, akitoka injury inamchukua muda kugain his confidence.
Tofauti na Matip anatoka injury leo tena ya muda mrefu na anaperform vizuri tu.

Na inaumiza, maana dogo ni moja ya nguzo za mashambulizi.

Walau front 3 ingekuwa clinical angerudi haraka kwenye kiwango, sasa jamaa zetu hata pasi chache wanazopewa wanazitumia vibaya.

Toka ligi imeanza, Liverpool alikuwa hajamaliza game bila goli, ila sasa game 2 mfululizo zimepita bila goli!

Ukiacha draw na kufungwa, swala linalonipeleka kwenye panic mode ni kumaliza game 2 mfululizo bila goli hata moja!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom