Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mkuu city hawezi kukaa juu kama akilingana idadi ya michezo na Utd.
Utd atakuwa juu kwa point moja. Nakusahihisha...angalia vizuri msimamo...city ana viporo viwili ukilinganisha na nyie (liver) ila kimoja ukilinganisha na Utd.

Piga hesabu vizuri!
Mimi siyo shabiki wa liva.

Pia ndiyo maana nimepoint kua na man u ana game mkononi
 
Wewe kweli akili zako jau Mancity ina complete squad ao walio majeruhi tu wanaweza beba ubingwa kina sane

Duuh!
Sane anacheza Bayern Munich kaka toka September mwaka jana!
Silva yupo Spain
Man C hawezi chukua ubingwa hana watu kwa sasa
 
Most likely huu ubingwa akachukua Guardiola

Zifunge timu kubwa kwa ndogo sio ndogo tu ndio labda uchukue ubingwa

Msimu huu Spurs anawafunga nje ndani, Round ya pili Emirates stadium hamshindi ,Chelsea pia sidhani kama mtamfunga msimu huu
Ushakuwa mganga wa kienyeji sasa, sio?
Huyo City wako, kwanza tunaanza kumgonga kesho, ili kudhihirisha kua msimu huu Manchester United tuna jambo letu.
 
Most likely huu ubingwa akachukua Guardiola

Zifunge timu kubwa kwa ndogo sio ndogo tu ndio labda uchukue ubingwa

Msimu huu Spurs anawafunga nje ndani, Round ya pili Emirates stadium hamshindi ,Chelsea pia sidhani kama mtamfunga msimu huu
Hizo ni porojo tu..Kuwafunga wakubwa huku wadogo wanakukazia ni upumbavu..na ndo maana mechi ya 17 tunaenda kukaa juu ya table..hao wanaowafunga big teams watakuwa wapi?

Msimu huu huwezi kuu-judge kwa principle zilezile ulizozizoea.
 
Kitoabu shida yako ndiyo hii.

City ana games mbili mkononi hizi games akishinda anaenda kua namba moja kwa tofauti ya points mbili.

Na nyinyi mna game moja nafikiri.

Tukiangalia rekodi za kuperform kwa man u na city ni ngumu kusema man u atakazana hapo alipo. Mashabiki mmemtukana kocha na kutaka atoke amekusanya points mnaanza kuhisi muda wa kombe ndiyo umefika, siyo kweli.

Ligi ya sasa kuanzia wa 11 akishinda games tatu mfululizo ana chansi ya kufika namba 6 akipoteza games 2 mfululizo anajikuta nafasi ya 15. Kuna siku nilikuambia hiyo nafasi ya pili kakaa, leicester, chelsea, villa, southampton, city, spurs na wote wametoka haitakua ajabu na man u akitoka.
Mkuu, City amecheza michezo 15 ana points 29.
Manchester United ame cheza 16 ana points 33.
Hii maana yake hata akishinda zote (na mimi nimfunge Burnley) bado nitakua point 1 mbele yake.
Sasa anawezaje kuwa mbele kwa points 2?

Au nahapo nimekosea? (Maana huchelewi kuniambia sijui mpira)
 
Mashabiki wa livakuku mbona munalazisha ligi isimame?
Breaking news:
PM Boris to adress the nation at 1:30 PM UK time!
League ya EPL kusimamishwa sababu ya kuenea sana maambukizi ya corona?
Stay tuned
 
Mkuu, City amecheza michezo 15 ana points 29.
Manchester United ame cheza 16 ana points 33.
Hii maana yake hata akishinda zote (na mimi nimfunge Burnley) bado nitakua point 1 mbele yake.
Sasa anawezaje kuwa mbele kwa points 2?

Au nahapo nimekosea? (Maana huchelewi kuniambia sijui mpira)
Hujakosea boss. Ngoja tuone mnavyochukua kombe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom