Matip sio beki makini ndugu yangu, anajitahidi kuimprove lakini bado sana
Ndiyomana kukabuniwa Msamiati unaitwa "MAONI" kwasababu kama hizi.
Kulingana na Maoni/Mtazamo wa Mourinho Robben hakuwa mchezaji wa maana, Lakini kulingana na Maoni ya LVG Robben ni one of the Best player in last Two decades.
Kama hao Magwiji wawili katika ukocha wametofautiana Mtazamo juu ya mchezaji mmoja basi hakuna sababu ya kuwa Mimi na wewe tusitofautiane kwa mchezaji mwengine mmoja as long as tutaheshimiana kwenye kutoa Maoni yetu.
Kwa uwezo wangu hata kama ni mdogo wa kutazama mpira basi nasema popote kuwa Matip ni miongoni mwa mabeki bora japo hajafikia level za kina VVD.
Mimi Beki ninampima kwa Vitu viwili tu!
1) Uwezo wake wa kukaba
2) Kutokuwa na error prone zinazoleading to goal
Sasa Matip tumchambue katika mambo hayo Mawili!
1) Je ni error prone?
2) Je from last season to this season amefanya error ngapi zilizopelekea goli?
3) Amekuwa mzembe kwenye kukaba au anashindwa kabisa kukaba kwenye Defence?
4) Naomba mifano ya hizo mechi ambazo utazijibia hayo maswali.
Nadhani ukijibu hayo maswali ndiyo yatatupa picha kuwa Matip ni beki wa aina gani.
Lakini tukiendelea kusema/kuamini tu kuwa Matip ni beki mbovu bila ya kuthibitisha huo ubovu wake na kwa Mechi zipi! Hapo itakuwa tunazungumzia ubovu wa kinadharia.
Kwamfano Mimi ukinihoji kwanini ninasema Hendo mbovu?
Nitakujibu kuwa Hendo ni Attacking Midfielder (AM)
Kwahiyo AM ninampima kwa mambo hayo.
1) Assists
2) Goals
3) Take on
4) Touch
5) Passes complete
6) Dribbling
Sasa kama Ndani ya Msimu mzima hafiki ata Assists 7 wakati Beki TAA ana 13 hapo nitamuelewaje?
Nikitazama Wachezaji wa Kawaida tu kina Fraser wana takriba Assists 15 kwenye EPL tu, yeye kwenye all competitions hafikishi hata assists 7 halafu mtu aniambie ni Mzuri kwasababu akiwa hana mpira ni Mkali?
AM hafikishi hata Goli 5 per season in all competitions?
AM hawezi hata kukokota mpira na kudrible?
Kwahiyo nakuomba ujenge hoja kwa mifano juu ya ubovu wa Matip na si kushikilia misimamo tu kuwa Matip ni Mbovu.