Sio Kwamba Sijiamimi Mkuu!
Mimi siamini Utabiri! Kwahiyo Si mtu Wa Kutangaza Kushinda Game kabla sijaicheza! Ninakiamini Mimi Ni Kile Kinachotokea Baada Ya Dakika 90 au 120.
Na ndiyomana Mimi Hata Siku moja Hunikuti Kutangaza Kuchukua Kombe Kabla Ya Ligi haijaanza.
Na Ninachoamini Mimi Ni Kwamba Mtu yeyote unayemsika anasema na Kujihakikishia Kuwa Msimu huu atabeba Kombe Kwenye Timu Yake basi Huyo Hajui Mpira. Kwasababu yeye Ni sawa na Mganga Wa Kienyeji tu na Ndiyomana haangalii Kuwa Mpira Ni Mchezo Wa Mahasebu, Makosa, Uimara Wa Timu, Mbinu, Fitness na Utayari. Factor moja tu Kati ya Hizo inaweza Kukunyima Ubingwa Hata Kama Una Kikosi Bora Kiasi gani.
Mtu anaejua Mpira Maranyingi Husema Msimu huu Nina matumaini Ya Kubeba Ubingwa... Na Sio Kujihakikishia Kuwa lazima Ataubeba kama wanavyosema baadhi ya Watu utafikiria Matokeo ya Mchezoni wanayapanga wao.
Mimi Ni Mshabiki Wa Liverpool lakini Kama Mshabiki Wa Mpira basi Msimu huu Naipa Nafasi Man City ya Kubeba Ubingwa Wa EPL... Lakini Sisemi Kuwa Lazima itabeba Bali naipa nafasi tu Kutokana na Uimara Wa Timu Yao. Kwani Kama Nilivyotaja Hapo juu zipo Factors ambazo zinaweza Kumkosesha Ubingwa.