Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Naona msimu umeanza mmejaa kama kawaida ,msimu ukikaribia kuisha kama kawaida mnamuachia jukwaa Malafyale peke yake
Kuna wakati hata keyboard unaiona ina moto, kuna muda ndani ya tunnel unauona mwanga unahisi umekaribia mwisho kumbe ni mwanga wa tochi mwingine naye anatafuta pa kutokea inakubidi tu uwe mpole.

Ila msimu huu tuko bega kwa bega hatuwezi kuanguka
 
Wewe unaifunga westham ambayo ina wachezaji wa tano wageni ukimjimlisha na kocha halafu unajihakikishia nafasi ya kwanza!!

Bado sana kuimprove uwezo wako.
Hongera wewe mwenye timu nzuri iliyo improve kwa kuifunga Huddersfield
 
Kwani Hapo Nimezungumzia Nafasi ya Kwanza?

Hivi uliyemfunga 3 - 0 Siku ya Jumamosi Yeye Ni Bingwa Mtetezi?
Sio bingwa mtetezi lakini ukiangalia kikosi cha Westham bado ni kipya sana.

Wachezaji wengi bado hawajaelewana ..enewei bado tunasonga mbele na huu ndo mwanzo tu
 
Pamoja na yote bado Liverpool hii haijafikia kiwango cha ile Liverpool ya akina Pepe Reina, Gerald, Kuit, Alonso na Torres. Na bado ilishindwa kubeba EPL

• Hata Intermilan Ya Kina Christian Panucci, Javier Zanetti, Laurent Blanc, Ronaldo, Roberto Baggio, Vieri, Taribo West, Ivan Zamorano na Clarence Seedorf haikuwahi Kuchukua CL Na Kwenye Ligi Mwaka 1999/2000 imekamata Nafasi ya 4.
Lakini Intermilan Ya 2010 ya Kina Cambiaso, Sneida na Balotelli imefanikiwa Kubeba Champion League na Ligi Kuu.

• Hata Chelsea ya 2012 iliyochukuwa CL haijaifikia Chelsea Bora Kabisa Kuwahi Kutokea duniani ya 2004/2005 ambayo haikuwahi Kubeba CL.

• Hata Manchester ya 2011 iliyobeba Ubingwa Wa EPL yakina Carrick haijaifika hii Ya Mastaa Wa Bei mbaya Ya Kina Pogba, Sanchez, Lukaku, Fred, Martial, Matic na De Degea ambayo Haijabeba Ubingwa Wa EPL.

• Hata Real Madrid hii iliyobeba CL Mara 3 mfululizo haijaifikia Real Madrid ya Kina Casillas, Hiero, Medieta, Morientes, Raul, MacCmanaman, Roberto Carlos, Figo, Ronaldo na Zidane ambayo imeshindwa Hata Kubeba CL mbili.

Kwahiyo Jifunze tena kupenda Mpira Mdogo wangu Mpira Hauchambuliwi Hivyo.

Mpira Ni Kitu Kinachehesabiwa Kwa Wakati Uliopo.

Kwataarifa Yako Liverpool hii ya Sasa Ni More Stable kulinganisha na Hiyo unayosema Wewe.
 
Milner ni jembe ndugu yangu, japo umri ndio huo but jamaa ni mpambanaji, real professional...hivi Origi, Markavic, Lallana kweli msimu huu si watapata dakika chache sana uwanjani..maana Klopp lazima a deliver EPL n even better UCL...YNWA
Naona mmeshahakikisha kuwa EPL ni yenu. Time will tell
 
Sio Huddersfield tu hadi Wewe nitakufunga.
We kichaa unataka kila kitu tukufunze sisi ulikuwa unatumia q badala ya k sasahivi unajidai mjuaji kila timu INA haki ya kusherehekea ushindi, nenda Europa huku si saizi yako
 
Kuna wakati hata keyboard unaiona ina moto, kuna muda ndani ya tunnel unauona mwanga unahisi umekaribia mwisho kumbe ni mwanga wa tochi mwingine naye anatafuta pa kutokea inakubidi tu uwe mpole.

Ila msimu huu tuko bega kwa bega hatuwezi kuanguka
I pinned this post for future use
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom