hongereni liverpool kwa ushindi kwenye mechi dhidi ya West Ham United
niwe mkweli sijwahi kuishabikia liverpool lakini bahati nzuri juzi nilifanikiwa kuiangalia liverpool kwa dakika dakika 70. kwa mpira mulioendelea kucheza juzi liverpool wataendelea kuwa ndio timu pekee nchini uingereza yenye uwezo wa kuifunga manchester city kihalali.
maisha yangu yote nimekuwa nikiishabikia manchester united na tuna wachezaji bora zaidi ya liverpool lakini liverpool wanacheza vizuri zaidi kwa msimu wa tatu mfululizo kuliko manchester united na ndio maana nikasema wao pekee ndio wenye uwezo wa kuwafunga wababe wa etihad kihalali pasina kulinda ovyo kama umevamiwa na intarahamwe au boko haram mtaani kwenu, Ila kumfunga manchester city peke yake hakukukufanyi kuwa bingwa wa ligi kuu ya uingereza.
kwa mara ya kwanza nimebahatika kumuona
naby keita akicheza mpira na amenishangaza sana uwezo aliouonyesha kwenye mechi ya juzi na nadhani kwa sasa liverpool muna kiungo bora na aliyekamilika zaidi ya
ngolo kante wa chelsea, ushirikiano wake pamoja na
widjnaldum ulikuwa ni wa kuvutia sana.
ila bado nimebaki nikijiuliza dhumuni kuu la liverpool msimu huu hasa ni lipi?
kuwania ubingwa wa uingereza na ligi ya mabingwa au kuwania nafasi nne za juu?
kama dhamira kuu ni kuwa na timu yenye ushindani kama real madrid, barcelona, juventus, psg na bayern munich kwa nini mumeshindwa kutafuta back up ya wachezaji kama mohammed salah, van djik, firmino na mlinzi mwengine mwenye uwezo wa kuleta ushindani dhidi ya lovren.
hivi bado kuna mashabiki humu ndani wanaoamini backup bora ya
mohammed salah, van djik ni
adam lallana, origi, matip na sturidge.
- misimu miwili ya ligi kuu kila klabu inacheza mechi 76 lakini cha ajabu zaidi ni kwamba joel matip tokea asajiliwe liverpool amecheza mechi 54 za mashindano yote lakini bado klopp hakuona umuhimu wa kuongeza mlinzi mwengine
- solanke tokea asajiliwe na liverpool amecheza mechi 21 na amefunga goli moja kwenye mechi za timu kubwa.
- msimu uliopita daniel sturridge alicheza mechi 6 tu msimu mzima.
- msimu uliopita adam lallana amecheza mechi 11 msimu mzima na hakufunga goli hata moja.
- msimu uliopita kupitia klabu ya wolfsburg origi alifunga magoli 6 kwenye mechi 31.
inamaana liverpool mumesahau kilichotokezea kwenye mechi dhidi ya real madrid?
ngoja tuone ila nilichojifunza ni kwamba timu zote za uingereza bado hazijawa tayari kupambana na timu kubwa za nchi nyengine.
kule kwetu sisi unafungwa na sevilla nyumbani kwako halafu bado unaingia sokoni kutafuta mchezaji mmoja ambaye ataleta ushindani kikosi cha kwanza wakati barcelona wana mwanadamu anayekupa uhakika wa kufunga magoli 40 kwa msimu na bado wameingia sokoni kutafuta viungo washambuliaji.