Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

ROBERTO FIRMINO, FOWADI MWENYE ASILI YA MAKELELE.

Na Haatim Abdul

Wakati watu wanafurahia mabao ya Mohammed Salah msimu huu nadhani ni wakati wa kutambua pia uwezo na mchango wa Roberto Firmino pale Liverpool. Roberto Firmino ni fowadi wa kipekee katika uchezaji wake lakini tena uwezo wake haupewi sifa stahili pale England wazungu wanasema "Underrated".

Ni wachezaji wachache duniani ambao wangeinufaisha Liverpool hivi afanyavyo Firmino hata Salah hawezi pia. Kuna kitu cha kipekee ambacho anakileta kwenye timu ambacho kimemfanya atajwe kama mchezaji muhimu kwenye kikosi hicho kwa miaka kadhaa iliopita. Firmino ni defensive forward kwa maana ya mshambuliaji wa Ulinzi.

Katika miaka 130 ya historia ya mchezo wa mpira wa miguu narudia katika historia hakuna mshambuliaji yoyote kwenye soka aliewahi kufunga mabao 30, kufanya tackles 50+ na interceptions 60+ kwenye mashindano yote kwenye msimu mmoja. Hebu jiulize huyu fowadi ana muda gani wa kufunga magoli na mchango wake kwenye ulinzi ni huo hapo. Na tangu atue Liverpool amefanya tackling na interception nyingi kuliko hata nahodha wake, Jordan Henderson ambae ni kiungo wa kati.

Roberto Firmino ni mzaliwa wa Brazil eneo la Maceio, Alagoas. Alijiunga na timu ya vijana ya Figueirense akiwa na miaka 17 tu mwaka 2008. Daktari wa meno Marcellus Porteilla aligundua kipaji chake na Firmino alitumika kama kiungo mkabaji sikuizi tunaita mkata umeme. Firmino alikuwa mkata umeme huko Brazil na haishangazi akafunga mabao 8 kwenye mechi 36 za timu hiyo.

Bobby alifanya kutumika tu kama Defensive Midfielder mapema kabisa kwenye mpira wake licha ya kwamba kiasili ni mshambuliaji lakini ana uwezo mkubwa wa kukaka na Liverpool kwa sasa wanafaidika na Bobby mkata umeme wa Figueirense na huyu namba 9 muongo wa Liverpool. Hapa ndipo Firmino anapobaki mchezaji muhimu zaidi kwenye pressing ya Jurgen Klopp.

Firmino sio mshambuliaji ambae ataongoza chati za wafungaji, hana misuli ya kina Costa, wala mashuti ya Ibrahimovich, sio mpiga vichwa hatari kama Morata lakini Bobby ni wa kipekee sana. Ni mchanganyiko wa Bobby na mtu kama Casemiro wakati huo huo. Yani Casemiro au Kante angekuwa mshambuliaji basi angekuwa kama huyu jamaa.

Tangu atue Liverpool amefanya zaidi ya tackling 160 na zaidi ya Interceptions 60. Huyu ni beki ndani ya mshambuliaji. Ndio anaifanya kazi ya Liverpool kuwin mipira kule mbele iwe rahisi sana. Huyu hasa ndio Mr. Gengenpressing pale Liverpool. Ndio mchezaji anaeuelewa zaidi mfumo wa Klopp unahitaji nini. Na ndio mchezaji muhimu zaidi pale Liverpool. Mwenyewe Klopp amemwita "Injini".

Kazi anayoifanya Firmino pale Liverpool hakuna mchezaji mwingine yoyote mwenye uwezo wa kuifanya, kukaba na kushambulia. Kuongoza kwenye tackles na interceptions na bado ukafunga na kutoa pasi za goli. Historia haijapata mshambuliaji mwenye takwimu kama za Bobby.

Anakimbia, hachoki na anautafuta mpira baada ya kupokonywa kama mtoto alieporwa chapati. Anawin mpira na anawapa wenzie wamalize kazi. Huyu ndio Roberto Firmino Barbosa De Olivieira. Fowadi mwenye asili ya makelele. Fowadi wa kipekee kwenye soka.
 
Anamilikishwa kiwanja Macca
IMG_20180426_020203_908.jpg
 
Naona watu wanakariri sana mpira

Kosa sio kumtoa Salah ila hayo ni matokeo ya mpira na lazima tuujue na sio kuukurupukia.

Roma wangeweza kupata magoli ata Salah alipokuwepo uwanjani. Tayari watu wamesahau kuwa dakika 20 za mwanzo za mchezo Roma ndio walionekana kuwa hatari zaidi, je Salah hakuwepo uwanjani??

Wewe mpenzi wa mpira unayesema mechi bado mbichi huku moyoni mwako unasema Liverpool bila Salah ni nyeupe je huko kwao Roma Salah hatocheza?? Jibu ni kwamba atacheza.

Mnasahau kuwa Liverpool ni mabingwa mara 5 ulaya huku wakiwa na historia nyingi za comebacks ambazo huyo Roma hana. Kuwafunga Chelsea na Barca kwao sio kipimo cha ubora.

Wewe shabiki wa mpira unayekaa ukiwa na mtazamo wa mwelekeo mmoja nataka nikukumbushe tu kuwa, Liverpool ndiyo timu pekee ambao ina wastani wa kufunga angalau magoli matatu katika mechi za ugenini msimu huu wa UCL.

Hii post naiandika kishabiki ila na facts tupu. Unaposema kuwa Liverpool ina beki mbovu je unataka kusema kuwa beki nzuri huwa haifungwi magoli?? Je unataka kusema kuwa wao Roma waliweka wale washambuliaji wao wafanye jukumu la ulinzi au la kushambulia??

Unaposema Liverpool inabeki mbovu huku kuna timu mnazoamini kuwa zina beki bora kabisa na zimeshatolewa tunakuwa hatuwaelewi na tunakuwa na mashaka na uwezo wenu wa kuujua mpira.

Ndio mpira una maajabu yake na Roma wameweza kufanya msimu huu kwa kumtoa Barca ila niwaambie tu maajabu ya mpira sio Comebacks bali kuna maajabu mengine ya kufungwa nyumbani na ugenini kwa goli nyingi na hayo pia yatafanywa kwa Roma pia.

Ili Liverpool isikufunge basi cheza mipira ya kihuni huni ambayo haina utaratibu kama ya yule mwimbisha kwaya ya taarabu kikundi cha Old Trafford. Ukija wote tucheze mpira kwa faida ya mashabiki my friend hii Liverpool haitokuacha Salama.

Narudi kwa nini Salah anatoka: Salah kwa sasa ndo Star player wa timu ni lazima kocha amlinde.

Umeshaongoza goli tano unachotaka ni kipi tena?? Je unataka aendelee kuwepo uwanjani ili aumizwe na mabeki waloijikatia tamaa??

Je unapokuwa na timu yenye kikosi finyu huku wachezaji wako tegemezi wengi ni majeruhi unatakiwa kufanya nini zaidi ya kuwalinda waliopo ili usiongeze majeruhi??

Risk ya kurudisha goli tano bila Salah ni ndogo sana kuliko risk ya kumpoteza salah kwa majeruhi. Ni kichaa tu ndo asingemlinda mchezaji wake bora hasa pale anakuwa Tayari katimiza wajibu wake.

Niwaambie tu kitu: Tatizo la magoli kufungwa anapotoka Salah uwanjani sio Salah kutoka bali tatizo ni wanaoingia kama mbadala wake.

Mchezaji anayembadili Salah haingii kufanya majukumu ya Salah zaidi anaenda kuikaba timu yake.

Niwakumbushe tu: Mechi bado mbichi sana kama mnavyosema na maajabu yatatokea ila hayo maajabu yatakuwa ni ya Roma kufungwa goli nyingi sana kwake. Ila msije mkageuka na kusema kuwa Roma hakustahili kucheza nusu fainali na wengine mtasema hii ni nusu fainali mbovu kabisa ya muda wote...!

Ila kweli Liverpool inabeki mbovu sana ila nashangaa imefikaje nusu fainali na ubovu huo inamaana timu zingine nazo hazijui kufunga. Bora kuwa na silaha unayoweza kuitumia kifasaha kuliko kuwa na ngao ambayo haiwezi ata kukuokoa vitani.

Jana tumetia mpapaso mechi ya pili tunakula kiboga sebuleni kwenye nyumba ya mshua wao (sisi watoto wahuni)

TUKUTANE KIEV.
 
Jamani vp kuhusu chamberlain anarudi lini?


Kwanza Namshukuru Mungu Kwa #JF kurudi Hewani baada Ya Kuwa Hacked Kwa Siku Nzima.


Then, Kuhusu Chamberlain Hatoweza Kuichezea Tena Liverpool Msimu Huu Wala Hatoweza Kwenda Russia Kwa World Cup Kutokana Na injury ya Knee Ligaments.

Huenda Akarudi Kwenye Timu Mwezi July Kwa ajili ya Pre-Season.
 
Hivi Liverpool aliwahi lini kupoteza fainali nipe jibu


Mara moja tu, 2007!


Tumewahi Kupoteza Fainali Mara 2 Wakuu!

1) Mwaka 1985 tulipoteza dhidi ya Juventus! Walitufunga goli 1 - 0 na goli lilifungwa na Platin Kwa Njia Ya Mkwaju Wa Penalty.

2) Mwaka 2007 tulipoteza dhidi ya AC Milan Kwa Magoli 2 - 1.
 
Mane Leo Hakuripoti Mazoezi na Ameonekana Akiingia Hospitali Mjini Liverpool!! Amepata Minor injury hapo Juzi.
 
Tumewahi Kupoteza Fainali Mara 2 Wakuu!

1) Mwaka 1985 tulipoteza dhidi ya Juventus! Walitufunga goli 1 - 0 na goli lilifungwa na Platin Kwa Njia Ya Mkwaju Wa Penalty.

2) Mwaka 2007 tulipoteza dhidi ya AC Milan Kwa Magoli 2 - 1.
Asante kwa ufafanuzi mkuu
 
Jürgen Klopp confirmed Sadio Mane has an injury issue and the Liverpool forward will be assessed ahead of Saturday's meeting with Stoke City.

The No.19 missed training on Thursday but, at his pre-match press conference, the manager reported the problem is ‘not that serious’.

“Of course there is something. We will see,” said Klopp when asked for an update on Mane.

“It is not that serious; there is a chance for tomorrow. If we use that chance or not… it is quite early in the day.

“In these times, you always have to use each second and minute, speak to the player, speak to the Doc, speak to the physiotherapists and all that stuff. At the end, you have to make a decision and I will make a decision.”

Sadio Mane fitness latest
 
Jürgen Klopp’s team selection for Saturday’s meeting with Stoke City will be based entirely on his determination to get the three points.

Klopp Said: “My line-up, or the idea for the line-up is to win the game - that’s the only thing I can think about.
“It’s not about resting players or whatever, we all know that we are a quite short of options in a few departments. It’s the longer break of the intense week, we play Tuesday and Saturday then Wednesday again so that’s always OK from a recovery point of view, it’s always good so we could play the same team like we played against Roma if the players are available, that’s the only thing.
 
Sadio Mane Atakosa Mchezo Wa Kesho dhidi Ya Stoke City Kutokana Majeruhi! Tuombe Arudi Kikosini Kabla Ya Jumatano.
 
i think formation ya leo ni 3-5-2!!
best of luck!!!..to us Kops!
ynwa
 
Liverpool team: Karius, Alexander-Arnold, Gomez, Van Dijk, Klavan, Moreno, Henderson, Wijnaldum, Salah, Firmino, Ings.

Substitutes: Mignolet, Clyne, Lovren, Milner, Robertson, Solanke, Woodburn.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom