Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Nimekubali Kiongozi.

Alichokitaka KLOPP kimefanya KAZI.

KLOPP ni Mwalimu Mzuri sana.

Sema Mashabiki wa Liverpool walikuwa wanashindwa kumuelewa.

Mwalimu Mzuri Siku zote mpe Muda kwenye KLABU hata kama mtakua hamchukui MAKOMBE, cha kufanya ni kuvumilia.

MATUNDA Siku zote yanaonekana baadae

Mkuu mm nilishtukia kama Liverpool sasa ina kocha kitambo sana wkt ule anafungwa fungwa lkn unaona kabisa team ina progress!
Wengi sana hapa hawakuwa na subira!Siwezi badili Klopp na kocha yyt hapa duniani
 
Kwa hakika tangu aje VVD upande wa ulinzi umeimarika sana, yale makosa yaliyo tu cost game ya Arsenal, Westbrom,Swansea n.k kwa sasa hayajatokea tena
Pep kwa mara ya kwanza amekua mdogo kama piliton lakini pia hata mashabiki wa Manshit sio wapiga kerere kama pale Kops end Anfiled...yaaani mashabiki wishaona kutupiga goli 4 bila ni pangumu...
kwa mwendo huu Klop naamini atatuteletea kikosi cha kuchukua EPL msimu ujao...
Tusubiri Ijumaa draw aje Roma, Real au Munich...hapa watakaaaa
Kiongozi.

Ujue sio kitu rahisi kubadilisha Matokeo kama yale.

Kwenye Mashindano (Michuano) makubwa kama yale.

Kwa KLABU kubwa yenye FOMU nzuri Msimu huu, halafu Nyumbani kwao.

Kwa kweli KLOPP anastahili Pongezi nyingi sana
 
Wakuu Tukiangalia Nje Ya Champion League Basi Yule Dogo Wetu H. Wilson na leo Katupia Kamoja... Yule Dogo ananuka Nyavu balaa Kuliko Mvuvi Wa Sangara.
 
Kiongozi.

Ujue sio kitu rahisi kubadilisha Matokeo kama yale.

Kwenye Mashindano (Michuano) makubwa kama yale.

Kwa KLABU kubwa yenye FOMU nzuri Msimu huu, halafu Nyumbani kwao.

Kwa kweli KLOPP anastahili Pongezi nyingi sana

Mkuu klopp ni master class, game yetu leo ilikuwa underpressure sana.lakini tumeondoka na ushindi kwa taabu hivyo hivyo,klopp bonge la kocha hili kombe tunabeba msimu huu.in klopp we trust
 
Man City Wanalalamika Kuwa Goli lao limekataliwa! Lakini Wamesahau Kuwa Kabla Ya Kufunga Goli lao la Kwanza Raheem Sterling alimsukuma VVD ndiyo akachukua Mpira.
Wanalalamika ujinga, kipa akiwa hayupo golini na kuna mshambuliaji kabaki na beki hyo ni offside, sheria hamtaji golikipa wanatumia neno opponent
 
BARCA Mungu mtu wa yule jamaa leo kawa OUT kwa Roma
Barca anafungwa bao 3-0 na hana shoot hata moja on target!
Barca huyu hawezi mfunga Liverpool yetu popote pale
Huwezi tumikia mabwana wawili, yaani makombe mawili
Hizi timu mbili zinafanana
Barca wanaposses na Man City wanaposes
Barca wanahitaji point mbili kutawazwa mabingwa wa Hispania na Mancity wanahitaji point 6 kutawazwa mabingwa wa Uingereza
Hongereni Liverpool maana ni dhahiri mtakutana na AS Roma, mtu wa kumchunga pale ni Edin Dzeko tu na MO asije kuionea huruma timu iliyomuinua kisoka mpaka sasa hivi matajiri wa dunia kama akina RM wanammulika kwa ukaribu
 
JOSE ni Mwalimu wa kuua VIPAJI.

Yeye anataka Mchezaji mpaka awe na jina.

Huwa hana Muda wa kutengeneza VIPAJI, kuendeleza VIPAJI, kukuza VIPAJI
Mafala wa Liverpool mmepumbazwa na matokeo mmesahau Klopp alitaka kuishusha daraja Dortmund
 
Mkuu mm nilishtukia kama Liverpool sasa ina kocha kitambo sana wkt ule anafungwa fungwa lkn unaona kabisa team ina progress!
Wengi sana hapa hawakuwa na subira!Siwezi badili Klopp na kocha yyt hapa duniani
Unajua MASHABIKI siku zote wanataka mabadiliko ya haraka haraka, kitu ambacho hakiwezekani kwa Mwalimu Mgeni. Labda tu huyo Mwalimu akute KLABU Wachezaji wake wamekaa vizuri, walishajengeka kitimu au wawe na UWEZO binafsi.

Siku zote kwa Mwalimu mgeni, kuna kitu cha kuyazoea Mazingira.

Hapa kwenye kuyazoea Mazingira ni pamoja na Wachezaji uliowakuta, na wewe uweke/ulete Wachezaji wako ambao pia itawachukua Muda kuendana na MFUMO wa waliowakuta pale. Na kisha tena wewe Mwalimu uwabadilishe Wote (Wachezaji wapya na wazamani) waendane kwenye MFUMO unaoutaka wewe.

Ujue hapo mpaka waje kukaa sawa, ujue ni Suala la Muda hilo.

Mkifanya Mchezo mtakuwa mnabadilisha WALIMU kila leo na Mafanikio hayaonekani
 
Mie na United damu damu mpaka kiama. Ukiacha hilo mnastahili kombe na hongera kem kem. Mpaka ninammiss Steven Gerrard.

Tulikuwa hatuna kocha miaka yote na ndiyo sasa tumepata kocha!
Tunaanza kunyanyua kwapa makombe makubwa na tunaanzia UCL huko Jijini Kiev
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom