Mchezaji Ukishamuekea Kipengele cha "Release Clause" unakuwa Huwezi Kumcontrol tena na Mamlaka Yako Kwake ni Madogo Sana Kwani Anakuwa na Mamlaka kamili ya Kujiuza mwenye Bila ya Kuishirikisha Timu Hata kidogo! Si unaona Kilichotutokea Kwa Suarez! Au Kilichowatokea Barcelona Kwa Neymar! Au Tulichowafanyia RB Leipzig kwa Keita!!!
Sasa Liverpool Hawataki tena kuingiza Kipengele Hicho Katika Mikataba ya Wachezaji ili wasije wakawa na mamlaka ya Kujiuza Wenyewe kama Neymar au Suarez au Nabby Keita.
Timu Kama Real Madrid inaweka Kipengele cha "Release Clause" Kwa Wachezaji lakini Kinakuwa na Thamani ambayo Mchezaji Hanunuliki!
Kwa mfano Benzema Release Clause Yake ni €1000m, Rinaldo €1000m na Bale €1000m kwahiyo Timu haziwezi kuwanunua Kwa Kipengele hicho...
Lakini Kwa Upande Wa EMRE CAN wakala wake anataka lazima Aekewe Kipengele cha "Release Clause" kisichozidi thamani ya £85m na Mshahara Wa £120K jambo ambalo Liverpool imekataa....
Na sababu Ya Kukataa wanaona Kuwa CAN bado umri wake ni Mdogo, Kwahiyo wanachelea Kuja akaongezeka Kipaji ikisha akaja akachukuliwa Kiubwete kwa £85m wakati anakula £120K za watu.