Live: Kizota Dodoma

Live: Kizota Dodoma

  • Thread starter Thread starter MegaPyne
  • Start date Start date
Na John Daniel, Dodoma


Mgombea mwingine Diwani wa Ukonga, Dar es Salaam Bw. Jerry Slaa aliomba asihukumiwe kwa dhambi isiyo yake kutokana na jina lake la mwisho kufanana na mwanasiasa machahari wa kambi ya upinzani ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbrod Slaa

Alijitetea kwamba hana uhusiano wowote na mwanasiasa hivyo anaomba achague ili atoe mchango wake kwa CCM.

MAJIRA-05/11/2007
kijana huyu ni fisadi,alishawahi kula pesa pale Mlimani wakati akiwa Waziri wafedha wa Daruso,alikula kama million 8,ila ana uwezo mkubwa wa kujieleza..
kwa Mtazamo wangu,hakuja jipya ambalo tulitegemea..siku zote na nitaendela kulisimamia hili..kura yangu ya Ubunge lazima nitampa Mpinzani,ila Urais Mapenzi yangu yako sisiemu tu..ila sisiemu si mama yangu,wakiboronga hata Urais nitamchagua Zitto.
Hongera Slaa
 
CMB kwa kweli tunakushukuru sana kwa kutuhabarisha vizuri na kwa ufasaha wa hali ya juu...si kama wababaishaji wengine hapa JF..ambao wanatukwaza kweli hata kusoma postings zao...Big up!! Hivi Matayo David hakugombea ama alichaguliwa kupitia kura za mikoani? ....
 
Mapya yanaweza yasiwe mengi lakini yapo!!! mfano mmojawapo ni kwamba Pius Msekwa ameahidi siasa za hoja na kuhakikisha watashirikiana na vyama vingine vya upinzani kwa kupitia kwenye muungano ule unaongozwa na Cheyo... pia amesema ndani ya CCM mijadala huru itaruhisiwa bila shaka!!

Hili ni jambo jema!!!
 
Mapya yanaweza yasiwe mengi lakini yapo!!! mfano mmojawapo ni kwamba Pius Msekwa ameahidi siasa za hoja na kuhakikisha watashirikiana na vyama vingine vya upinzani kwa kupitia kwenye muungano ule unaongozwa na Cheyo... pia amesema ndani ya CCM mijadala huru itaruhisiwa bila shaka!!

Hili ni jambo jema!!!

Na kutafuta wasomi Chuo Kikuu etc ili baadae tuwe na Viongozi Bora Zaidi.
 
CMB kwa kweli tunakushukuru sana kwa kutuhabarisha vizuri na kwa ufasaha wa hali ya juu...si kama wababaishaji wengine hapa JF..ambao wanatukwaza kweli hata kusoma postings zao...Big up!! Hivi Matayo David hakugombea ama alichaguliwa kupitia kura za mikoani? ....

Dr. Mathayo ameanguka!

CMB naomba ulete list ya walipiga chini ili mzee shukrani ziwe kamili mzee!!!
 
si kama wababaishaji wengine hapa JF..ambao wanatukwaza kweli hata kusoma postings zao....

ushirombo,
wanakukwaza kwa lipi?hiyo ni tabia ya kibaguzi na lazima ipigwe vita,wanatumia ibara ya 18 na 22 kuwasilisha fikra zao...kumbuka ni watanzania wenzako..
 
tupe current news kiongozi,nani kachaguliwa nani kapigwa chini,namuona na mh cheyo je naye kachaguliwa?
 
20 BORA KWA KUNDI LA CCM BARA Edward Lowassa,Makamba,Andrew Chenge,Bernand Membe,Jaka Mwambi,Kapuya,Kinana,Kachuma,Wassira,Jaka Mwambi, Makongoro,Mahanga,Sumaye,Katp. Komba,Kingunge,Lukuvi,Chiligati,Amos Makala,Samwel Wangwe,Mwakuysa,Jackson Msome
Kundi la watu 20 kutoka Zanzibar.Mohamed Shein,Shams Vuai Naotha,Hussein Ali Mwinyi,Mohamed Bilali,Sale Feruzi,Muhamed Khatibu,Samia Hassan,Kidawa Sale,Salim Msabaha
Hadija Abood,Mansuru Hemed,Omari Yusufu Mzee,Balozi Seif Iddi,Mohamed Moyo,Modilin Sirus,Prof. Makambe Mnyaa,Vuai Ali Vuai,Brig. Adam Mwakanjuki,Edinton Kisasi, ShauAbdala Hamisi.
Hawa ni Kundi la Wazazi Bara NEC CCM Stela manyanya,Zainab Gama,Musa Assan zungu,Adam Malima,Muhamed Nondo,Richard Said Nyaulawa
Washindi kwa wanawake. CCM BARA Sofia simba,Kate Silvia Kikamba,Asha baraka,Hadija Omari Kopa,Samsha Mwagunga,Rehema Nchimbi,Anna Malecela,Aisha Kidoga,
Diana mkumba Chilolo,Anna Semamba Makinda,Pinde Chanda,Zakia Megji,Magret Sita.
Washindi NEC Vijana. CCM BARA Lucy Mahenga,Zainab Mfaume Kawawa,Violet Mzindakaya,Nape Moses,Jerry William Slaa,Sara Msfari Ali,Seleman Chambi,Benard Malisa,
Edwin Sanda
Imenukuliwa kutoka JF.
 
Nampongeza muungwana kwa kumpendekeza "Spika Msekwa" kuwa M/Mwenyekiti Tz Bara. Hali hii ni dalili njema kwa wapenda demokrasia ya kushindana kwa hoja badala ya mbinu chafu zilizokuwa zinafanyika hapo awali. Mzee Msekwa pamoja na kuwa mwana demokrasia makini, bado ana busara ya kutambua matakwa ya wakati na wananchi katika ulingo wa siasa. Baada ya kumsikiliza akitoa salamu zake za pongezi kwa kuteuliwa na kupigiwa kura,muda mfupi uliopita; ameonyesha kufahamu wajibu na mipaka ya kazi yake! Lakini zaidi amesisitiza umuhimu wa kushirikiana na wapinzani katika kujenga siasa za hoja badala ya siasa za chuki na vijembe ( nadhani zilizozoeleka ndani ya ccm). Kwa kifupi binafsi nategemea kuona ccm mpya inayotambua utashi wa wanachama wake na wananchi kwa ujumla katika kufanya maamuzi ya haki na ya kidemokrasia............Kidumu chama cha Mapinduzi!
 
Kitendo cha Membe kushika nafasi ya 4 right behind Lowassa ni statement of intent Its like "Watch out ur days r numbered!"

By the way Mudhihir hakugombea? just being curious... talk abt sympathy votes...
 
Ningeshangaa sana iwapo Hiza Tambwe na Thomas Ngawaiya wangeshida, ingekuwa sio kitu cha kawaida katika makundi husika waliyogombea. Hawa wasubiri nafasi za upendeleo toka kwa mkuu wa kaya, kwani pamoja na kurudi sisiemu bado hawana lao pale, sisiemu ina wenyewe, kama hawa:

Wafuatao 'Kama baba Kama mwana'
Adam Kighoma Malima
Violet Mzindakaya Majiyatanga
Nape Moses Nnauye
Hussein Alli Mwinyi
Amani Abeid Karume
Zainab Mfaume Kawawa

Tutafika tu!
 
Jamani naomba kujua nini kimemtokea Nchimbi! ... Mbona jina lake halimo au hakugombea?
 
Kama Baba, kama mwana, kanyaga twende. Maji hufuata mkondo.

1. Adam Kighoma Malima
2. Zainab Mfaume Kawawa
3. Violet Crisant Mzindakaya
4. Nape Moses Nnauye
5. Hussein Ally Mwinyi
6. Amani Abeid Karume
7. .........
8. ........


Sisiemu ina wenyewe!
 
Ningeshangaa sana iwapo Hiza Tambwe na Thomas Ngawaiya wangeshida, ingekuwa sio kitu cha kawaida katika makundi husika waliyogombea. Hawa wasubiri nafasi za upendeleo toka kwa mkuu wa kaya, kwani pamoja na kurudi sisiemu bado hawana lao pale, sisiemu ina wenyewe, kama hawa:

Wafuatao 'Kama baba Kama mwana'
Adam Kighoma Malima
Violet Mzindakaya Majiyatanga
Nape Moses Nnauye
Hussein Alli Mwinyi
Amani Abeid Karume
Zainab Mfaume Kawawa

Tutafika tu!
tutafika kama wananchi wakichukua hatua,yuko wapi mtoto wa Kenyata,Uhuru kenyatta...haya mambo yana mwisho,tatizo nchi hii inaongozwa na system,na ukitaka kuharibu system yoyote ni kutoa fuse inayoruhusu umeme kupita..
 
Final Version!

Hawa ni Kundi la Wazazi Bara NEC CCM


Washindi kwa wanawake. CCM BARA


Sofia simba
Kate Silvia Kikamba
Asha baraka
Hadija Omari Kopa
Samsha Mwagunga
Rehema Nchimbi
Anna Malecela
Aisha Kidoga
Diana mkumba Chilolo
Anna Semamba Makinda
Pinde Chanda
Zakia Megji
Magret Sita

NOTE; Spelling za majina mengine nimekosea


Huyu ana UHUSIANO na Emmanuel Nchimbi?
 
Dr. Mathayo ameanguka!

CMB naomba ulete list ya walipiga chini ili mzee shukrani ziwe kamili mzee!!!

Huyo bora alivyoanguka! mwenzie kapata ajari badala ya kutoa msaada alikuwa busy anapiga picha! sasa wamempiga na yeye.. chini!
 
Jamani naomba kujua nini kimemtokea Nchimbi! ... Mbona jina lake halimo au hakugombea?


Kuna aliyekuwa Dodoma jana, anasema kuwa Nchimbi aliaga kwa uongozi kuwa kafiwa, kwa hiyo aliondoka kwenda mazishini.
 
Shyrose banji kimempata nini manake nina kumbukumbu kama kafanya kampeni ya nguvu au hayupo kwenye system?
 
Unaposema 20 bora unamaanisha nini? Mchujo unaendelea au hao ndio wameshachaguliwa tayari?
 
Back
Top Bottom