As far as specification Apple wapo pande mbili kuna vitu wapo vizuri zaidi ya competition na kuna vitu wapo ovyo. Mfano.
1. Soc yao kwa sasa ndio best sokoni hakuna simu yenye processor yenye nguvu kushinda iphone japo kwenye gpu bado qualcomm yupo juu na mambo mengine kama modem na wifi anapitwa na simu za android.
2. Usiangalie tu ukubwa wa ram nipo radhi nitumie simu ya 2gb ram yenye dual chanell na ddr4 memory zenye speed kuliko simu ya 4gb ama 8gb ram ambayo ni single chanell na ram za ddr2 ama ddr3 zenye speed ndogo. Zipo simu zenye ram nzuri zaidi ila iphone zake pia sio mbaya zinapita hizi ram kimeo za kichina. Ukumbuke simu gpu yake inatumia ram ya simu hivyo jinsi ram ya simu ilivyo fasta na ndio apps na games zitarun smoothly.
3. Pia megapixel kwenye camera humaanisha ukubwa wa picha na sio quality. Dslr camera kali unaweza kuta ni 8mp tu. Kifupi kuchukua content za 4k inahitajika mp 8 tu. Ambayo kwa sasa ndio vifaa vya kisasa kama tv na pc vinaitumia. Quality ya picha sana inasababishwa na sensor iliotumika pia kuna vitu kama software, ois, aperture, lens etc vinachangia.
Kuhusu mambo mengine nakubaliana na wewe Apple innovation yao ni ndogo sana na ukikuta kitu chao kizuri basi utakuta kina mkono wa kampuni nyengine mfano display za samsung, memory za smasung etc. Kifupi ana asemble vitu best toka makampuni mengine na sio mvumbuzi kama baadhi ya kampuni nyengine.
Kuhusu software na Ecosystem zao zimetengenezwa kwa watu ambao hawataki mambo mengi kwenye simu, upige simu utumie whatsapp na insta etc.
Ila ukitaka mambo makubwa zaidi vitu kama VR, casting, file management, etc ios si yako.
Umenena vyema Mwalimu!
Kitu kingine cha kuongelea ni kwamba Apple wao wameweza kuoptimize OS yao na Hardware i.e. iOS imetengenezwa kufit processor, gpu, na RAM management. Hii inapelekea kuwa na uwepesi na speed convenience kwenye kufungua na kutumia apps na games.
Shida ya Android ni kwamba ni mfumo wazi ambao hata wewe ukitaka utaweza download na kuedit unavyotaka (Open Sources OS). Kila kampuni inayotumia Android (unless unaongelea Android One) inai'customize Android OS ili kujiweka tofauti na makampuni mengine. Na hii wanafanya kwa kuweka skins (mabadiliko ya kimuonekano na matumizi) zao juu ya Android OS. Na zaidi ya hapo wanajaza bloatwares (apps zao ambazo unalazimishwa kuwa nazo hata ka huzitumii). Sasa hii ndo inapelekea mara nyingi kwa uzoefu wangu, kwa simu za Android in the long run kuanza kuchoka na kuwa slow hata kama uliinunua ikiwa na RAM 4Gb, octa core processor, n.k...
Na kwenye RAM pia teknolojia iliyotumika inamata wazee. Alichosema jamaa ni kweli, RAM za DDR4 zina clock speed kubwa sana lakini ni ghali kuliko hizi za DDR3 ambazo ni bei nafuu lakini clock speed ziko chini (sio chini kiviile, ila inaweza kuwa 30% chini ya DDR4). Sasa ndo unakuta RAM kuubwa lakini we jua tu teknolojia iliyotumika ndo iko nyuma.
Ila kwenye customization na uwezo wa mtumiaji kutumia kifaa to the fullest, asee Twende mbele turudi nyuma, Apple hawezi mkutia Android hata siku moja na ndio maana Android ndio Operating System yenye Market Share kubwa kuliko iOS.
Ila tukirudi kwenye security issues, tuwe wakweli, Android inaongoza kwa kuwa na udhaifu sana kutokana na Nature yake ya kuwa Open Source system na watumiaji wake wengi kutokuwa waangalifu na vitu wanavyoweka kwenye simu zao. Hapa Apple yuko vizuri.
Na kwenye suala la ubunifu, Apple kidogo wako nyuma. Inawachukua muda mrefu kidogo kuja na kitu kitakachoshangaza watu. Na vifaa vyao vingi wanasource toka kwa makampuni yanayotumia Android mfano. Camera sensor toka kwa Sony, screen tech ya Samsung, etc.
Binafsi ni mtumiaji wa Android, ila kimtizamo naona kila upande una ubora wake na mapungufu yake na kila Team ina haki ya kutetea upande wake.