Kwanini Simu za iPhone zina specifications ndogo?

Kwanini Simu za iPhone zina specifications ndogo?

Sijutiii kutumia samsung kwa kweliiii.... yaan J7 Prime tu iko bomba kuliko hivyo vi iphones..
 
Duu mwanangu si bora hata ungekua unatumia S series yeyote kama S8, S9, S5, S7 kuliko hiyo takataka eti J7 Prime hiyo ni Low end sana aisee
S series sizielewi kabisaaa kama ilivyo kwa A series...
 
Nimewai Tumia Samsung S3, then note 4. Baadae Nikatest Huawei na Tecno. Lengo lilikuq kujua hasa ladha na uzuri hususani baada ya kuona watu wanaongea ongea sana. Kila simu hapo juu, niliitumia kwa kipindi kirefu cha kuweza kujua uzuri na ubaya wa kila moja. Baada ya kupita kote huko, nikajilipua nikanunua iphone 8 plus. Ukweli ni kwamba, sijajutia hela yangu maana simu ina ladha asikwambie mtu. As well kuna vionjo fulani hivi ambavyo simu zangu zote za nyuma hazijuwa na huo uwezo. Apple Devices for sure are in another level. Comment yangu hii imebase from practical experience. Sina utaalam sana wa kuchambua jinsi iphone hii ilivyo but kuna tofauti kubwa sana na hizo samsung, huawei na tecno ambazo nilishawai kutumia.
Sasa mkuu unafananisha iPhon 8+ na Note 4 halafu eti unakuja kutoa comments. You are not fair. Chukua Huawei P20 Pro halafu ndio ufananishe na hiyo iPhone 8+.
 
Ndio maana umeambiwa hizi simu wanatumia watu wanaojielewa
Sema ni kitu gani watu wana enjoy katika iphones?
Binafsi sijawahi kuvutiwa na iphone kutokana na limitations zake.
Mi mdau wa Samsung mwanzo mwisho
 
iPhone Hana cha kumzidi Samsung na Sony au LG zaidi ya security.....

Unanunua simu ya ml 2 halafu mipaka ya matumizi wanakupangia ....huo utumwa sikubaliani nao.

Siku hizi simu zinafanya mambo mengi karibia uwezo wa PC, lakini sio za iPhone.
 
Wakuu habarini.
Naomba kujua kwann Iphones zina specifications ndogo ukilinganisha na Simu nyingine zote hata ambazo zinachipukia.

Sijaona Iphone inayozidi hivi vigezo

Maximum RAM 3gb
Maximum Camera 12 Mega Pixels
Maximum Battery size </ = 3000 mAh

Hawa jamaa Inovation yao ipo katika mlengo upi???.

Hizi simu sijawahi kuzitumia na nahisi sizipendi japo ninapesa ya kununua Iphone niitakayo. Lakini naona simu kama ya waganga wa kienyeji. Maana Masharti ni mengi kuliko Enjoyments.

Yani kumiliki hizi simu ni kama Mkinga mfanya biashara anaelala chooni ilihali ana majumba ya kifahari

1. No interaction with PC without Itunes
2. No Bluetooth compatibility with other devices except Its Generic Siblings
3. Kupata Apps za local developers ni Msala.
4. No downloading on Websites and blogs
5. Poor documents perusing and management
6. No memory extension.
7. Finger print zinakufa Ovyo kuliko simu zozote
8. Poorness of IOS Ecosystem
9. No access of payable services in some many regions ( Especially Africa)
10. Poor navigation of ( BACK ) Button
Sijui watu wenye Iphone huwa mna enjoy nini kwenye simu zenu.
11. No dual SIM
12. No File Management App
13. Safari si a default Browser no way ndugu yangu

Naomba ushirikiano
Mi nishasemaga iOS mashart meng siztak na pesa ya kununua ipo AOS ndo kila kitu
 
Mp 8 za iPhone yoyote ile ni zaid ya mp 16 za Samsung, kamera bora haing'arishi pcha wala kutia nakshi yoyote ile

Tuache sukari humu bana,unapotaja simu samsung hata tim cook anageuka,maana ndiye mpinzani wake wa ukweli.
 
Sasa mkuu unafananisha iPhon 8+ na Note 4 halafu eti unakuja kutoa comments. You are not fair. Chukua Huawei P20 Pro halafu ndio ufananishe na hiyo iPhone 8+.

Sijui watu humu wanakuwaje,kuna note 8 au s8+ na s9+,weka meza moja na hiyo iphone 8+ yake atajua hajui.
 
Sasa mkuu unafananisha iPhon 8+ na Note 4 halafu eti unakuja kutoa comments. You are not fair. Chukua Huawei P20 Pro halafu ndio ufananishe na hiyo iPhone 8+.

Sijui watu humu wanakuwaje,kuna note 8 au s8+ na s9+,weka meza moja na hiyo iphone 8+ yake atajua hajui.
 
Mwisho wa siku haya mambo yanaweza kuwa mazoea tu, binafsi mara ya mwisho nimetumia Android ni 2012, baada ya hapo nikajikuta nimetumbukia kwenye iPhone na sijawahi kuwaza kutumia android, naona kama zina vitu vingi sana.
Napenda iPhone kwasababu ni simple, haizeeki mapema, haina muingiliano na unsecured sources of applications, haipokei application zinazoweza kupunguza ufanisi wa simu automatically (unless uipakue mwenyewe).
Hizo setbacks zako sioni kama ni strong reasons labda ya extension of memory, nikiwa na simu yenye uwezo mdogo huwa nakereka pale inapojaa mapema inanilazimu kufuta picha na music. Otherwise kwa matoleo mapya ni kuanzia 64 GB which is enough kwa matumizi ya simu unless kama unataka kuigeuza iwe TV, Radio, PC na Photo album yako.
1. Interaction with PC unataka ufanye nini? There a lot of ways to transfer your documents to wherever you want.
2. Bluetooth compartibility sijawahi hata kuona kama ni setback kwangu, kitu ninachohitaji nitakitafuta kwa njia ninayoweza, tuna Whatsapp, emails na njia nyingine nyingi za kushare documents. Hatuko kwenye zama za Infrared and bluetooth
3. Local developer apps, kama developer hajaona umuhimu wa kutengeneza iOS app mimi sioni umuhimu wa hiyo app, by the way sipendi kujaza apps kwenye simu yangu, i just use the basic ones, vingine nitavitafuta kwa website, kama app ipo kwenye appstore haisumbui kuipata.
4. Downloading on website, if you are talking about music and videos its a YES, lakini ukiwa mtumiaji wa iPhone hii haikusumbui, we have a lot of options for Audios, labda wanaopenda kuangalia videos na wako nje ya mtandao hawawezi kustream ndo wanapata shida.
Downloading of other materials and documents is possible, labda kama haujui kuitumia simu.
5. Document perusing inakua poor vipi? Hapa linakuja suala la ugeni na iOS. The only thing i cant do is working on spreed sheets coz ni complicated, all other documents i can open them and even edit the possible ones
7. Finger print kufa hovyo!! You might be talking about iPhone 4s zilizokua zinakufa home button na hazikua na fingerprint, i have never seen an iphone with such a problem ninazotumia mimi au watu wanaonizunguka. Tatizo pekee nimeliona kwa watu kama watatu ni shida ya charging system kwa iPhone 6plus
8. iOS ecosystem iko poor! I may have not understood what you meant here
9. An example of those payable services which cant be accessed by an iPhone please.
10. Back button has never been a problem to me, i use an assistive touch naenjoy kiasi ukinipa hizo zenu zenye back buttons nitateseka.
11. Dual sim ndo sijawahi kuihitaji kabisa, ukizingatia mazingira niliyokulia hata kabla ya kuanza kutumia smartphone niliaminishwa simu genuine ni zile single line.
12. You dont need an app to manage your files if they are all stored at respective sites. Nikitaka Muzik najua ipo Music app, PDF books nazikuta iBook, Photos zipo kwenye file la photos, what do i need an app for?
13. Safari is a default browser, how is this a setback? Kwani explorer kuwa default browser kwa window computers inasababisha shida gani? By the way Safari is the best browser ever, hizo nyingine zina mapungufu kibao.
 
Mzeee raia wana ipendea camera ya nyuma tu na kale ka apple pale nyuma basi lakin pale amna simu... ukitaka u enjoy chukua samsung s8
 
Me nime tumia simu zote...


Huawei..tecno...itel...iPhone....Nokia...samsung...sony...infinix.... lakin mwisho wa siku simu ilio nivutia zaidi ni samsung s8 na baada ya apo ni iphone 6
 
Watu wengi hawafahamu muwa apple ni kampunz yenye nguvu sana kwenye soko lakin haimaanishi ndio simu bora kuliko zote zipo simu hata kwenye soko la kwetu huku hazijafika sababu kwanza zina bei na bora zaid ya Iphone ila wana nguvu ya soko ingia mtandaoni utafute simu zenye ubora na bei kibwa kuliko iphone utaikuta imetupwa mbali tu nyingi zinaeishia america na ulaya.!
Kuna simu zina itwa oppo...one plus...google nexus... aisee ni kiboko
 
Back
Top Bottom