Kwanini Simu za iPhone zina specifications ndogo?

Kwanini Simu za iPhone zina specifications ndogo?

Nani Kasema lazima uwe na Itunes?


Kwa Ajili ya nini Bluetooth? kurushiana picha na video? Hizo mambo ni old fashion mkuu. Tangu nianze kutumia iphone sijawahi kuona kitu kwa mtu akisha nkakiomba kurushiwa kwa bluetooth.


Msala wake ni upi? kama local developer hajatengeza app, hilo ni kosa la Apple?


Use another Browser if you cant donwload via Safari


Hii na 12 naona zinagongana, how can you say Poor documents perusing and management, halafu unasema NO file management app?


Buy one with 256 GB tatizo liko wapi mkuu?


Kivipi?


IOS ni Poor ecosystem? 😱 Bado huna uhakika na unachoongea ndugu yangu.


How is it poor? Android wanafollow the same Back button. Hakuna tofauti ya app navigation kwenye ios na Android. Insta , whatsapp n.k navigation ipo ivo ivo.


Zile simu fake tangu miaka 2005 ivi i think dual sim zilikuwepo. How is it an issue? Samsung S series kwani ni dual sim cards? Au SONY Xperia? Dual sim unakuta kwenye vitecno na wenzake tu.


Kama ni mtumiaje wa iphone hasa, huwezi kusema ichi kitu. File explorer zipo nyingi tu.


Safari is called a default browser kwa sababu ios inakuja na hio browser ikiwa tayari pre installed. Options zipo nyingi tu mbona.



Mfano kama zipi?

Samsung alimcheka Apple alivoweka Notch kwenye simu. Sasa anaetengeza Android ametoa tolea la OS kwa ajili ya simu zenye notch, na sasa Android nyingi zinafuata njia hio....

APPLE anawaburuta bado.

Ikiwa wewe sio power user, kazi yako ni kupiga na kupokea simu, apple wanaona haina haja ya kuwa na simu ambayo huwezi kuitumia power yake in full.

Samsung na wenzake simu unazikuta zina specs kubwa mara 8GB ram, processor octa cores, lakini ukitizama perfomance unakuta hata iphone 4s inawakimbiza
You nailed that dude, agiza soda nakuja kulipia, ukichukua bia silipii
 
Your so right chief. Asante kwa uchambuzi wako. Sasa je ni sahihi watu wa iphone kujiona ndo first class people?? Ili hali wanamasononeko mengi na simu zao?
Ukiona mtu unasononeka na kitu chako basi ujue hilo sio chaguo lako, kuna msemo unasema ukimpenda mwenye chongo utaona kama ana makengeza tu
 
Ungeinunua walau uitumie km mwez hv ungejijib vzr sana. Ninachopendea hz simu hawatumii vilaza. Over.
Kilaza ni yule anayetumia kwa kutaka sifa tu. Mtoa post katoa hoja nzito wewe ipinge kwa hoja yako. Taja specs za iphone unayotumia kama ni zaidi ya ulizotaja.
Mbwembwe nyiiiingi. Hamna kitu
 
Nimewai Tumia Samsung S3, then note 4. Baadae Nikatest Huawei na Tecno. Lengo lilikuq kujua hasa ladha na uzuri hususani baada ya kuona watu wanaongea ongea sana. Kila simu hapo juu, niliitumia kwa kipindi kirefu cha kuweza kujua uzuri na ubaya wa kila moja. Baada ya kupita kote huko, nikajilipua nikanunua iphone 8 plus. Ukweli ni kwamba, sijajutia hela yangu maana simu ina ladha asikwambie mtu. As well kuna vionjo fulani hivi ambavyo simu zangu zote za nyuma hazijuwa na huo uwezo. Apple Devices for sure are in another level. Comment yangu hii imebase from practical experience. Sina utaalam sana wa kuchambua jinsi iphone hii ilivyo but kuna tofauti kubwa sana na hizo samsung, huawei na tecno ambazo nilishawai kutumia.

Binafsi naona gepu ni kubwa sana kutoka samsung s3 mpaka kwenye iphone 8plus?kamata galaxy note 8,nafikiri majibu utayapata.
 
Wakuu habarini.
Naomba kujua kwann Iphones zina specifications ndogo ukilinganisha na Simu nyingine zote hata ambazo zinachipukia.

Sijaona Iphone inayozidi hivi vigezo

Maximum RAM 3gb
Maximum Camera 12 Mega Pixels
Maximum Battery size </ = 3000 mAh

Hawa jamaa Inovation yao ipo katika mlengo upi???.

Hizi simu sijawahi kuzitumia na nahisi sizipendi japo ninapesa ya kununua Iphone niitakayo. Lakini naona simu kama ya waganga wa kienyeji. Maana Masharti ni mengi kuliko Enjoyments.

Yani kumiliki hizi simu ni kama Mkinga mfanya biashara anaelala chooni ilihali ana majumba ya kifahari

1. No interaction with PC without Itunes
2. No Bluetooth compatibility with other devices except Its Generic Siblings
3. Kupata Apps za local developers ni Msala.
4. No downloading on Websites and blogs
5. Poor documents perusing and management
6. No memory extension.
7. Finger print zinakufa Ovyo kuliko simu zozote
8. Poorness of IOS Ecosystem
9. No access of payable services in some many regions ( Especially Africa)
10. Poor navigation of ( BACK ) Button
Sijui watu wenye Iphone huwa mna enjoy nini kwenye simu zenu.
11. No dual SIM
12. No File Management App
13. Safari si a default Browser no way ndugu yangu

Naomba ushirikiano
Bora niendelee kubaki na Techno yangu
 
Nimewai Tumia Samsung S3, then note 4. Baadae Nikatest Huawei na Tecno. Lengo lilikuq kujua hasa ladha na uzuri hususani baada ya kuona watu wanaongea ongea sana. Kila simu hapo juu, niliitumia kwa kipindi kirefu cha kuweza kujua uzuri na ubaya wa kila moja. Baada ya kupita kote huko, nikajilipua nikanunua iphone 8 plus. Ukweli ni kwamba, sijajutia hela yangu maana simu ina ladha asikwambie mtu. As well kuna vionjo fulani hivi ambavyo simu zangu zote za nyuma hazijuwa na huo uwezo. Apple Devices for sure are in another level. Comment yangu hii imebase from practical experience. Sina utaalam sana wa kuchambua jinsi iphone hii ilivyo but kuna tofauti kubwa sana na hizo samsung, huawei na tecno ambazo nilishawai kutumia.
Umetumia s3 alafu ukachukua iPhone 8 plus lazima uone tofauti s3 ni ya mda ukilinganisha na iphone 8 plus ukitumia s9 au note8 au note 9 utaona pia ni bora kuliko hiyo nenda YouTube fanya comparisons utakubali
 
Security unaficha nini???????

Picha za uchi?????

Mana watu wanakomaa na security lkn ukiangalia anachokificha hakuna.
Huna la maana unaloona kwenye security zaidi ya picha za uchi.

Akili yako ndo imeishia hapo. How imbecile you must have been.
 
Umenena vyema Mwalimu!

Kitu kingine cha kuongelea ni kwamba Apple wao wameweza kuoptimize OS yao na Hardware i.e. iOS imetengenezwa kufit processor, gpu, na RAM management. Hii inapelekea kuwa na uwepesi na speed convenience kwenye kufungua na kutumia apps na games.

Shida ya Android ni kwamba ni mfumo wazi ambao hata wewe ukitaka utaweza download na kuedit unavyotaka (Open Sources OS). Kila kampuni inayotumia Android (unless unaongelea Android One) inai'customize Android OS ili kujiweka tofauti na makampuni mengine. Na hii wanafanya kwa kuweka skins (mabadiliko ya kimuonekano na matumizi) zao juu ya Android OS. Na zaidi ya hapo wanajaza bloatwares (apps zao ambazo unalazimishwa kuwa nazo hata ka huzitumii). Sasa hii ndo inapelekea mara nyingi kwa uzoefu wangu, kwa simu za Android in the long run kuanza kuchoka na kuwa slow hata kama uliinunua ikiwa na RAM 4Gb, octa core processor, n.k...

Na kwenye RAM pia teknolojia iliyotumika inamata wazee. Alichosema jamaa ni kweli, RAM za DDR4 zina clock speed kubwa sana lakini ni ghali kuliko hizi za DDR3 ambazo ni bei nafuu lakini clock speed ziko chini (sio chini kiviile, ila inaweza kuwa 30% chini ya DDR4). Sasa ndo unakuta RAM kuubwa lakini we jua tu teknolojia iliyotumika ndo iko nyuma.

Ila kwenye customization na uwezo wa mtumiaji kutumia kifaa to the fullest, asee Twende mbele turudi nyuma, Apple hawezi mkutia Android hata siku moja na ndio maana Android ndio Operating System yenye Market Share kubwa kuliko iOS.

Ila tukirudi kwenye security issues, tuwe wakweli, Android inaongoza kwa kuwa na udhaifu sana kutokana na Nature yake ya kuwa Open Source system na watumiaji wake wengi kutokuwa waangalifu na vitu wanavyoweka kwenye simu zao. Hapa Apple yuko vizuri.

Na kwenye suala la ubunifu, Apple kidogo wako nyuma. Inawachukua muda mrefu kidogo kuja na kitu kitakachoshangaza watu. Na vifaa vyao vingi wanasource toka kwa makampuni yanayotumia Android mfano. Camera sensor toka kwa Sony, screen tech ya Samsung, etc.

Binafsi ni mtumiaji wa Android, ila kimtizamo naona kila upande una ubora wake na mapungufu yake na kila Team ina haki ya kutetea upande wake.
Hata makampuni ya magari wana source other parts from their competitors or third parties.
 
Nimetumia 1phone 6+ kwa miezi 6 nikaona mauzauza tuu nikabadilishana na mtu TECNO CX, now nipo sumsung,
Watu wenye hizi simu wanaona ufahari sana kuanazo lkn nafsini mwao mungu ndio anajua.

Ndo maana wanawatukana hamna akili, kweli mtu na akili yako timamu unabadirishana iphone 6+ na tecno????

Si bora uuze af ndo ununue hyo tecno yko
 
Nimewai Tumia Samsung S3, then note 4. Baadae Nikatest Huawei na Tecno. Lengo lilikuq kujua hasa ladha na uzuri hususani baada ya kuona watu wanaongea ongea sana. Kila simu hapo juu, niliitumia kwa kipindi kirefu cha kuweza kujua uzuri na ubaya wa kila moja. Baada ya kupita kote huko, nikajilipua nikanunua iphone 8 plus. Ukweli ni kwamba, sijajutia hela yangu maana simu ina ladha asikwambie mtu. As well kuna vionjo fulani hivi ambavyo simu zangu zote za nyuma hazijuwa na huo uwezo. Apple Devices for sure are in another level. Comment yangu hii imebase from practical experience. Sina utaalam sana wa kuchambua jinsi iphone hii ilivyo but kuna tofauti kubwa sana na hizo samsung, huawei na tecno ambazo nilishawai kutumia.

Binafsi naona gepu ni kubwa sana kutoka samsung s3 mpaka kwenye iphone 8plus?
Nafikiri ungefanya mpango wa galaxy note 8,nafikiri majibu ungeyapata.
 
Ndo maana wanawatukana hamna akili, kweli mtu na akili yako timamu unabadirishana iphone 6+ na tecno????

Si bora uuze af ndo ununue hyo tecno yko
Kwani kuna ubaya gani? Si simu kwa simu?
 
Iphone ni mtihani kwa kweli labda watumiaji wanaenjoy kwa kua iko ghali then wanavyoipromote kuwa haingiliana na simu ingine ndio sabbu.
 
Tatizo linakuja pale unapo nunua kofuli la milioni moja kufungia mali ya thaman ya laki 5.

Ina security kubwa lkn ulichokihifadhi ni kipi hasa??

Picha za uchi?

Nambie kitu kimoja tu sim yoyote ya android inachoipita iphone, kimoja2 katika functionality
 
1. Flagship ya oppo entry device inaanzia dola 1000 kuendelea, same kwa mchina mwengine ambaye ataweka latest specification kwenye simu yake, simu inauzwa bei rahisi sababu inakuwa haina vitu fulani. Same kwa wengine kama kina huawei flagship zao baadhi zinazidi hadi dola 1000. Huyo samsung nae pia ana vimeo vyake vinauzwa rahisi kama simu za kichina mfano on series.

2. Hayo ni matumizi yako, wengine matumizi yao yanahitaji simu kubwa zaidi, kuna watu matumizi yao ile simu ya kisasa zaidi haiwezi yatimiza hivyo ananunua yenye nguvu zaidi kila mwaka ili aweze kuyatimiza hayo matumizi angalau kwa asilimia kadhaa.

Mfano game jipya la android ambalo ni port ya pc linaitwa fortinite linahitaji hizi specs.
-Ram 3GB
-free space 3GB
-GPU adreno 530 na mali G72 MP12 ama zaidi

Hizo gpu zote ni flagship class GPU hakuna kisimu cha mwenzangu na mimi kitachorun hata kiwe na oreo ama android pie, sasa mtu hela anayo anataka kucheza hilo game kwanini asinunue kitu roho inapenda?

Hilo ni moja bado kuna emulation, conversion, multitasking, note taking, display quality, camera, warranty nzuri etc vyote vinapatikana kwa ubora zaidi kwenye simu highend kuliko simu lowend ama za zamani.

Hizo bei umeziona au unataja ilimradi tu
 
Wakuu habarini.
Naomba kujua kwann Iphones zina specifications ndogo ukilinganisha na Simu nyingine zote hata ambazo zinachipukia.

Sijaona Iphone inayozidi hivi vigezo

Maximum RAM 3gb
Maximum Camera 12 Mega Pixels
Maximum Battery size </ = 3000 mAh

Hawa jamaa Inovation yao ipo katika mlengo upi???.

Hizi simu sijawahi kuzitumia na nahisi sizipendi japo ninapesa ya kununua Iphone niitakayo. Lakini naona simu kama ya waganga wa kienyeji. Maana Masharti ni mengi kuliko Enjoyments.

Yani kumiliki hizi simu ni kama Mkinga mfanya biashara anaelala chooni ilihali ana majumba ya kifahari

1. No interaction with PC without Itunes
2. No Bluetooth compatibility with other devices except Its Generic Siblings
3. Kupata Apps za local developers ni Msala.
4. No downloading on Websites and blogs
5. Poor documents perusing and management
6. No memory extension.
7. Finger print zinakufa Ovyo kuliko simu zozote
8. Poorness of IOS Ecosystem
9. No access of payable services in some many regions ( Especially Africa)
10. Poor navigation of ( BACK ) Button
Sijui watu wenye Iphone huwa mna enjoy nini kwenye simu zenu.
11. No dual SIM
12. No File Management App
13. Safari si a default Browser no way ndugu yangu

Naomba ushirikiano
Mie nilitumiaga mwaka flani enz hizo wasap inauzwa $0.99 kwa mwaka kabla hajanunuliwa na Facebook, bas ukitaka kudownload eti ulipie kwanza hio hela, pia apps zote za trails eti ulipie kwanza ndo uipakue, kuanzia siku hiyo nikamtafuta mtu nikamuuzia nikanunua Samsung. Ila kwa sasa ni mpenz wa Tecno maana haipiti miezi wanahamia Version latest ya Android.
 
Ungeinunua walau uitumie km mwez hv ungejijib vzr sana. Ninachopendea hz simu hawatumii vilaza. Over.
Aah wapi, sio kwamba ni vilaza hawatumii, hio Simu ya Iphone hovyo mno, yaani ili ufurahie uwe na Mac, ila uhamishaji wa mafaili na Windows mgumu had uwe na Itunes.
 
Back
Top Bottom