Wakuu habarini.
Naomba kujua kwann Iphones zina specifications ndogo ukilinganisha na Simu nyingine zote hata ambazo zinachipukia.
Sijaona Iphone inayozidi hivi vigezo
Maximum RAM 3gb
Maximum Camera 12 Mega Pixels
Maximum Battery size </ = 3000 mAh
Hawa jamaa Inovation yao ipo katika mlengo upi???.
Hizi simu sijawahi kuzitumia na nahisi sizipendi japo ninapesa ya kununua Iphone niitakayo. Lakini naona simu kama ya waganga wa kienyeji. Maana Masharti ni mengi kuliko Enjoyments.
Yani kumiliki hizi simu ni kama Mkinga mfanya biashara anaelala chooni ilihali ana majumba ya kifahari
1. No interaction with PC without Itunes
2. No Bluetooth compatibility with other devices except Its Generic Siblings
3. Kupata Apps za local developers ni Msala.
4. No downloading on Websites and blogs
5. Poor documents perusing and management
6. No memory extension.
7. Finger print zinakufa Ovyo kuliko simu zozote
8. Poorness of IOS Ecosystem
9. No access of payable services in some many regions ( Especially Africa)
10. Poor navigation of ( BACK ) Button
Sijui watu wenye Iphone huwa mna enjoy nini kwenye simu zenu.
11. No dual SIM
12. No File Management App
13. Safari si a default Browser no way ndugu yangu
Naomba ushirikiano
Tatizo ni pale mtu unapotumia iphone ukitaka i behave kama android wakati ni platform mbili tofauti, Landrover 110 ilikuwa haichambui oil wala mafuta inapiga kazi bila kuwasha taa ya check engine wala miss lakini haiifanyi iwe gari bora kuliko evoque inayochambua oil na mafuta.
Apple kwanza wana sera moja ya kujaribu kuzuia piracy kuanzia kazi za wasanii mpaka apps za developers ndiyo maana wanazuia kudownload ovyo ovyo vitu vya watu na apps zao.
Pia kupitia kudownload na kuweka vitu via njia maalum ni ulinzi tosha dhidi ya wadudu na hacking ndiyo maana appstore haina apps ambazo ni takataka kama google play kuna kila utitiri wa apps za ovyo.
Local developers hawajazuiwa kuweka apps appstore ila wanahitajika kulipa fees na itachekiwa kabla ya kuruhusiwa ilil linafanya mtu awe serious mtu hawezi kudevelope ujinga ujinga akaweka wakati itamcost kulipia lazima aweke kitu cha maana.
Hawaruhusu memory expansion kwasababu memory stick nyingi ni fake ni zinafanya simu ziwe slow zinakwasababu ya slow reading and writting speed.
Unapoongelea econsystem una maana gani? ios ina ecosystem safi kabisa kuna interaction kubwa between ios na bidhaa nyingine za apple kuanzia smart watches zao, tvs, mac os driven devices na icloud based services zao sasa sijui unaongela nini. Unaweza fanya kazi kwenye mac ukaja iendeleaza kwenye ipad au simu kwasababu zina sync automaticcally.
Navigation yake iko poa sana unless we ni mgeni au mtumiaji amekariri, jambo moja ambalo lilifanya ios iwapiku wengine hata mac os ni kuwa na simple and friendly user interface sema watumiaji wa tanzania wamekariri wanataka kila kitu kiwe kama walivyozoea ndiyo maana hata windowsa alipata shida kuwahamisha kutoka start button.
Dual sim card za nini tazama apple kalenga market ya wapi.
kuhusu ram, ios iko smooth hahitaji ram kubwa ku run smoothly kuna simu za android zina ram mpaka 6gb lakini sinachelwa kuwaka na zina rug wakati iphone kustack ni nadra na apple hana tabia ya kuweka vitu ambavyo havina maana kwenye gadgets zake sa akuwekee ram 5gb wakati ios hahitaji hiyo ku run smoothly atakuwa na maana gani? In future may ikitoka ios 16 huko huenda itahitaji ram 5gb.
megapixel tu hazi determine ubora wa picha itakayopigwa na simu, ubora wa picha unakuwa determined na vitu vingi ndiyo maana iphone 4 ilikuwa na migapixel 5 lakini ilikuwa na picha bora kuliko sim nyingi zenye megapixel nyingi.
Yah safari ni default browser, hii setback na mtu wakati wanunua iphone jua ni ios siyo android kama wataka kitu kinachokupa uhuru nunua android sasa unanunua kitu ukijua kina limitations halfu later unalalamika utakuwa mwehu.