Kwanini imekuwa changamoto kwa ajira mpya kulipwa pesa za kujikimu katika Halmashauri nyingi

Dbaba

Senior Member
Jun 18, 2022
170
515
Habari za muda ndugu zangu.

Kwanza kabisa niipongeze serikali kwa juhudi za kuajiri hasa mwaka huu wa 2023, imejitahidi sana kuajiri vijana katika kada mbalimbali tofauti na za ualimu na afya sambamba na pongezi hizo naomba serikali kupitia wizara hasa TAMISEMI wawape maelekezo na miongozo watumishi katika halmashauri hizo maana vijana wengi wanakumbana na changamoto ya watu ambao sio wataalamu husika waliokuwa wanakaimu baadhi ya nafasi kuzing'ang'ania na kuona vijana hao wapya hawajui chochote kitu ambacho ni kuchelewesha maendelea ambayo serikali imekusudia (wengi wa ajira mpya katika halmashauri wamekumbana na hii)

Kama uzi unavyoeleza juu pamoja na maagizo ya Mhe. Waziri Mchengerwa juu ya malipo ya kujikimu kwa wakati kwa ajira mpya ila changamoto imekuwa kufanya malipo hayo kwani yamekuwa ni kama hisani tu waajiriwa hao hali inayopelekea kuishi katika hali ngumu.

Ikumbukwe ajira mpya wengi wanatoka mbali na maeneo yao ya kazi hivyo hutegemea pesa hiyo kwa ajili ya kujikimu na kuanzia maisha.

Naomba wahusika kupitia TAMISEMI wafatilie hili jambo waone kwa nini kumekuwa na ugumu ilihali Mhe. Waziri alishaagiza.
 
Habari za muda ndugu zangu.
Kwanza kabisa niipongeze serikali kwa juhudi za kuajiri hasa mwaka huu wa 2023,imejitahidi sana kuajiri vijana katika kada mbalimbali tofauti na za ualimu na afya.sambamba na pongezi hizo naomba serikali kupitia wizara hasa tamisemi wawape maelekezo na miongozo watumishi katika halmashauri hizo maana vijana wengi wanakumbana na changamoto ya watu ambao sio wataalamu husika waliokuwa wanakaimu baadhi ya nafasi kuzing'ang'ania na kuona vijana hao wapya hawajui chochote kitu ambacho ni kuchelewesha maendelea ambayo serikali imekusudia.(wengi wa ajira mpya katika halmashauri wamekumbana na hii)
Kama uzi unavyoeleza juu pamoja na maagizo ya MH waziri mchengerwa juu ya malipo ya kujikimu kwa wakati kwa ajira mpya ila changamoto imekuwa kufanya malipo hayo kwani yamekuwa ni kama hisani tu waajiriwa hao hali inayopelekea kuishi katika hali ngumu.ikumbukwe ajira mpya wengi wanatoka mbali na maeneo yao ya kazi hivyo hutegemea pesa hiyo kwa ajili ya kujikimu na kuanzia maisha.naomba wahusika kupitia TAMISEMI wafatilie hili jambo waone kwa nini kumekuwa na ugumu ilihali mh waziri alishaagiza.
Wazir Mchengerwa anaujua ukweli ndio maana wakurugenzi hawatekelezi maagizo yake na yanaonekana ni ya kutafuta umaarufu zaid kuliko uhalisia ulivyo.
 
Mchengerwa anae safari ndefu huku tamisemi

Walimu waliopunjwa madaraja kwenye baadhi ya halmashauri bado halijatekelezwa

Anapaswa kujipanga maana pia kuna walimu wameachwa na hilo zoezi kutokana na nafasi zao (vyeo) vya mwajiri au mahali walipo au kujiendekeza kimasomo
 
Tatizo siyo halmashauri bali ni serikali kuu. Serikali haijapeleka OC halimashauri na mashirikani kwa miezi kadhaq. Kwa maelezo hayo mafupi naamini utajua sehemu sahihi ya kuelekeza lawama zako.
 
Mchengerwa anafahamu kuwa Kibubu Mama Mkwe wake Mama Abdul kakimaliza chote. Anajua Bibi wa wajukuu zake namna anavyofuja pesa za wananchi maskini ili ampendeze Mzee Hafidh. Kuwa mke wa nne tena wewe ndio wa mwisho sio kitu kidogo lazima ujirembulishe ili umvutie jamaa.

Kimsingi, Mama Abdul hama afanyalo. Toka mwezi wa 9 hakuna OC iliyoingia sio Halmashauri wala kwenye mashirika ya umma. Anajua hakuna Pesa toka Miradi ya Maendeleo iliyolipwa toka mwezi wa 10. Hakuna pesa yoyote inayolipwa kwa sasa kwani kibubu kimeisha so hao Halmashauri watawalipa kwa Pesa ipi kama sisi wakandarasi tu hatujalipwa hadi leo pesa za miradi tulizofanyia kazi.
 
Tena waanzie CHATO kabisa.

Ile halmashauri ina mambo mengi ya hovyo sana linapokuja suala la pesa. Kuanzia hizo za kujikimu, likizo, uhamisho, nk. Yaani kumpatia mtumishi stahiki zake wanaona kama ni kumfanyia hisani

Nakumbuka hata 2020 kwenye ule wa kuitwa uchaguzi niliona jopo la watumishi zaidi ya 800 wakiandamana kwenda kwa DC kulalamikia kuminywa 50k@ kwenye posho za kusimamia ule ulioitwa uchaguzi. Kwakuwa hawakuwa na alama nami nikajitupia humo kati yao nikaishuhudie show, tulikaa kama lisaa lizima. Mwanzo dc alionekana kusikiliza na kujali, alipokuja afisa utumishi jamaa mmoja bonge na mhasibu wake naye bonge (sijui kama bado wapo pale hadi leo hii) wakazama ofisini kwa dc na kuzungumza kwa dakika kadhaa, mara dc katoka nje kachenji anawaambia mchukue kilichopo au nikawasondeke ndani, sishindwi pamoja na wingi wenu. Sakata likaishia hapo.

Ajabu hayo madudu yote yanafanyika pale miaka yote na JPM alikuwepo na umwamba wake wote, na hakuwahi kufanya lolote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mchengerwa anafahamu kuwa Kibubu Mama Mkwe wake Mama Abdul kakimaliza chote. Anajua Bibi wa wajukuu zake namna anavyofuja pesa za wananchi maskini ili ampendeze Mzee Hafidh. Kuwa mke wa nne tena wewe ndio wa mwisho sio kitu kidogo lazima ujirembulishe ili umvutie jamaa.

Kimsingi, Mama Abdul hama afanyalo. Toka mwezi wa 9 hakuna OC iliyoingia sio Halmashauri wala kwenye mashirika ya umma. Anajua hakuna Pesa toka Miradi ya Maendeleo iliyolipwa toka mwezi wa 10. Hakuna pesa yoyote inayolipwa kwa sasa kwani kibubu kimeisha so hao Halmashauri watawalipa kwa Pesa ipi kama sisi wakandarasi tu hatujalipwa hadi leo pesa za miradi tulizofanyia kazi.
Upo sahihi kwa kiasi fulani.

Hizo changamoto za muda zaweza kuwa kweli chanzo ni halmashauri kutokupokea fedha kutoka juu. Lakini kuna halmashauri zina watu wana miaka hata kumi kazini hawajalipwa fedha za kujikimu, yaani fedha ambayo unatakiwa umlipe mtu kabla hata hajaanza kazi, linakuwa deni la kudumu! Watu wanahamishwa, mishahara ya miezi fulani haiingii, yote hayo yanakuwa madeni ya kudumu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mchengerwa anafahamu kuwa Kibubu Mama Mkwe wake Mama Abdul kakimaliza chote. Anajua Bibi wa wajukuu zake namna anavyofuja pesa za wananchi maskini ili ampendeze Mzee Hafidh. Kuwa mke wa nne tena wewe ndio wa mwisho sio kitu kidogo lazima ujirembulishe ili umvutie jamaa.

Kimsingi, Mama Abdul hama afanyalo. Toka mwezi wa 9 hakuna OC iliyoingia sio Halmashauri wala kwenye mashirika ya umma. Anajua hakuna Pesa toka Miradi ya Maendeleo iliyolipwa toka mwezi wa 10. Hakuna pesa yoyote inayolipwa kwa sasa kwani kibubu kimeisha so hao Halmashauri watawalipa kwa Pesa ipi kama sisi wakandarasi tu hatujalipwa hadi leo pesa za miradi tulizofanyia kazi.
Duh! Ubinadamu kazi. Hayo yooooote,ndo chanzo cha changamoto!
 
Tatizo siyo halmashauri bali ni serikali kuu. Serikali haijapeleka OC halimashauri na mashirikani kwa miezi kadhaq. Kwa maelezo hayo mafupi naamini utajua sehemu sahihi ya kuelekeza lawama zako.
Kwani halmashauri hawana mapato yao ya ndani, au siku hizi ngoma yote inadumbukia hazina...
 
Tatizo siyo halmashauri bali ni serikali kuu. Serikali haijapeleka OC halimashauri na mashirikani kwa miezi kadhaq. Kwa maelezo hayo mafupi naamini utajua sehemu sahihi ya kuelekeza lawama zako.
Unazungumzia miezi kadhaa kwa tatizo la miaka kibao!

Kwanza fedha za kujikimu huwa zinatokana na mapato ya ndani na halmashauri huwa zinalipa kwa cash kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Iko hivi:
Kila mwaka kila taasisi inapanga bajeti yake;
# Kwa matumizi ya kawaida(Oc).
# Kwa ajili ya Maendeleo/Miradi.
# Na mwisho kwa ajili ya Mishahara(Pe).
Lakini inatokea Serikali Kuu kwa ajili ya kunusuru au kuondoa upungufu fulani inakuja na mkakati maalumu wa kuajiri na ajira hizi zinakuwa haziko kwenye mpango/bajeti ya taasisi husika hivyo kuilazimu Serikali Kuu kugharamia vile ambavyo taasisi husika haikuweka kwenye Mipango yake kwa kulipa Posho za kujikimu na Mishahara.
Hoja/Utata unakuja je? Serikali Kuu imepeleka hizo pesa kwa Taasisi husika kama fidia/ nyongeza na hiyo Taasisi ikashindwa kulipa? Na kama Serikali Kuu haijapeleka Taasisi haiwezi kusema hivyo wazi wazi bali itakubali kubeba mzigo wa mkubwa wake( hiki ni kitu cha kawaida kwenye Jamii zetu..mkubwa akitoa ushuzi mdogo lazima useme wewe ndio umefanya hivyo)
Cha msingi kwa Watumishi ni uvumilivu kwani hayo yanabaki kuwa madeni na hata kama itachukua muda yatakuja kulipwa.
Kwenye Utumishi hivi vitu siyo vigeni vilikuwepo sana ila siku hizi kwa sababu ya utandawazi ndiyo maana vinaonekana sana.
 
Hayo mapato ya ndani sharti yasome hazina halafu ndo hazina iyarejeshe au pia inaweza isiyarejeshe kwa wakati.
 
Kwani halmashauri hawana mapato yao ya ndani, au siku hizi ngoma yote inadumbukia hazina...
Hayo mapato ya ndani sharti yasome hazina halafu ndo hazina iyarejeshe au pia inaweza isiyarejeshe kwa wakati.
 
Back
Top Bottom