Kwanini Balozi za Marekani, Uingereza, EU na Canada hazijatoa tamko lolote kuhusu kukamatwa Mbowe?

Kwa wanaofuatilia masuala ya diplomasia, wanatambua kuwa mara nyingi balozi za Marekani, Uingereza, Canada na Umoja wa Ulaya nchini Tanzania huwa mstari wa mbele kutoa matamko pindi viongozi wa upinzani wanapokamatwa. Kumbukumbu ya karibuni ni balozi hizo zilipoijia juu serikali ya Magufuli kufuatia kukamatwa kwa Marehemu Maalim Seif na viongozi mbalimbali waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana...
Ni muda tu wamewapa serikali lakini watatoa habari tu
 
Umeongea mada kubwa sana ambayo wengi hapa hawatakuelewa wataongozwa na mihemko.

Hisia zangu jibu la hoja yako au swali lako:

Mosi hawa jamaa huangalia maslahi yao zaidi kuliko demekrasia. Ndiyo maana walinyamazia udikteta wa Cambodia ya kikomunisti ya 1970's sababu jamaa alikuwa anapigana na adui yao Vietnam. Hapa wameona awamu hii maslahi yao yatalindwa na mtawala.
Hatukuwasikia hawa jamaa wakipiga kelele wakati kuna tuhuma watu wanafukiwa kule Migodini wakati wa awamu ya tatu.

Walifumbia macho Saudia kisa cha Jamal Kashogi.

Pili inaweza kuwa kuna ukweli flani ktk tuhuma alizopewa Mbowe.

Tatu inaweza kuwa wanaona bora wawapotezee kwa muda Mbowe na wataka katiba mpya sasa ambapo bungeni wamejaa wabunge wa CCM tupu itapitishwa katiba mbaya zaidi hivyo bora wasubiri wakati muafaka.
 
Wanafanya kwanza biashara ya chanjo hayo mengine yatafuata baadae....😂😂😂
 
Kwa wanaofuatilia masuala ya diplomasia, wanatambua kuwa mara nyingi balozi za Marekani, Uingereza, Canada na Umoja wa Ulaya nchini Tanzania huwa mstari wa mbele kutoa matamko pindi viongozi wa upinzani wanapokamatwa. Kumbukumbu ya karibuni ni balozi hizo zilipoijia juu serikali ya Magufuli kufuatia kukamatwa kwa Marehemu Maalim Seif na viongozi mbalimbali waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana...
Wewe hata huwa hueleweki unasimamia nini. You are a hopeless fellow who deserve to be ignored by any sane person.
 
Kwa wanaofuatilia masuala ya diplomasia, wanatambua kuwa mara nyingi balozi za Marekani, Uingereza, Canada na Umoja wa Ulaya nchini Tanzania huwa mstari wa mbele kutoa matamko pindi viongozi wa upinzani wanapokamatwa. Kumbukumbu ya karibuni ni balozi hizo zilipoijia juu serikali ya Magufuli kufuatia kukamatwa kwa Marehemu Maalim Seif na viongozi mbalimbali waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana...
Kwani Magufuli alipokuwa anawapoteza Watanzania mpaka wewe Kukimbia hizo Balozi zilisemaje?
 
Cha msingi uwahakikishie wanachokitaka. Hata ungeua watu hadharani mchana kweupe, they won't bother!
Mzee Baba alikuwa anatishia maslahi yao. Chochote kilichowapa uchochoro wa kutoa matamko walikitumia hata kama hakina kichwa Wala miguu!

So to say mze baba alikuwa sahihi kuwasulubu chadema?na wao walikuwa wanapiga mayowe just kwa maslahi yao na siyo maslahi ya chadema?kama ni hivyo,mbona chadema wanakimbilia kwenye vyombo vyao vya habar kulalamikia huu uonevu?
 
Sasa mboye alitaka kulipua vituo vya mafuta ili apate faida gani??
 
Kwa kuwa Mbowe kafikishwa mahakamani tayari na kusomewa mashtaka, hizo balozi hazina tena grounds za kutoa matamko. Mbowe katuhumiwa na bila shaka Balozi zinataka kuona sheria ikifuata mkondo wake bila kuonekana wanameddle into other country's business

Kama mpaka leo angekuwa hajashtakiwa, bila shaka wangetia neno.
 
Option nzuri kwenye Natinal crisis kama hii ni kukutana na kuongea nao - sasa utemi wa kumpa kiongozi mwenzako UGAIDI haijawahi kuwa suluhu ya matatizo haya katika nchi yoyote ile.

Hata kwenye ngazi ya familia mtoto, mke ama Baba mwenye mji kudai haki yake huwa si UASI bali mnakaa chini wote mnayamaliza bila hata majirani kujua kinachoendelea.
 
Back
Top Bottom