Saint Anne
JF-Expert Member
- Aug 19, 2018
- 78,525
- 235,263
Umenena vizuri sana Mkuu.Andiko hili limenitafakarisha sana. Tuache kwanza habari ya Joanah. Tujiulize sisi wenyewe, sisi ambao hatujui siku, saa, wala muda wetu umefika lini, tumejiandaaje?
Huenda unaandika hapa kumpa pole, kumwonea huruma au kumfariji mtoa mada kwa sababu ameambiwa ana prognosis ya miezi miwili au chini ya hapo.
Lakini hebu geuza swali hilo kwako mwenyewe. Kama ingekuwa wewe umeambiwa, “Una miezi miwili tu au chini ya hapo,” ungefanya nini?
Wengi wetu tungeanza kusema, Nitajikaribisha zaidi kwa Mungu. Nitatubu. Nitasali zaidi. Nitawaomba msamaha nilio wakosea. Nitawasamehe walionikosea. Nitakaa karibu na familia yangu na watu ninaowapenda. Nitatengeneza mambo yangu na Mungu.
Vizuri kabisa! Lakini swali ni hili, Kwa nini tusifanye hivyo sasa?
Kwa nini tusimtafute Mungu kwa moyo wote wakati bado hatujaambiwa tuna miezi miwili?
Kwa nini tusitubu leo, badala ya kusubiri siku tutakayoogopa kifo?
Kwa nini tusisamehe leo, badala ya kusubiri dakika za mwisho?
Kwa nini tusimpende Mungu leo kwa nguvu zetu zote, badala ya kusubiri mwili utakapokuwa hauna nguvu tena?
Tunajua kabisa kwamba kifo hakitupi appointment. Hakipigi simu kusema, “Nakuja kesho saa 10.” Hakituandikii ujumbe kusema, “Jiandae, zimebaki siku 30.”
Wengine wanapewa taarifa ya muda wao. Sisi wengine tunaishi bila taarifa hiyo.
Na labda hapo ndipo kuna tofauti kubwa.
Yeye amepewa kile ambacho sisi hatujapewa. Nafasi ya kuhesabu siku zake.
Lakini sisi tunaishi kana kwamba tumepewa miaka mingi.
Tunapanga kesho, mwezi ujao, mwaka ujao… lakini hatujui kama tutafika huko.
Huenda mtu anayejua amebakiza miezi miwili ndiye aliyeanza kuishi kwa umakini kuliko yule anayefikiri ana miaka ishirini mbele yake.
Kwa hiyo, tusimwangalie tu kwa huruma.
Tujitazame sisi wenyewe.
Kama leo ungeambiwa huu ndio mwezi wako wa mwisho, ungeendelea na maisha haya haya?
Ungeendelea kubeba chuki hiyo?
Ungeendelea kuahirisha toba?
Ungeendelea kusema, “Nitabadilika baadaye”?
Ungeendelea kuishi mbali na Mungu?
Kama jibu ni hapana, basi kwa nini unasubiri mpaka uambiwe una muda mfupi wa kuishi?
Neema si kuambiwa siku yako ya mwisho. Neema ni kupewa leo.
Leo bado unaweza kutubu.
Leo bado unaweza kusamehe.
Leo bado unaweza kurekebisha.
Leo bado unaweza kumtafuta Mungu.
Leo bado unaweza kusema, “Bwana, niko hapa.”
Kwa hiyo, huenda hatuna neema ya kujua tumebakiwa na muda gani kama alivyoambiwa yeye. Lakini tunayo neema kubwa zaidi ambayo mara nyingi tunaipuuza.
Tunaishi leo.
Na leo ndiyo siku ya kujiandaa.
Usisubiri prognosis ikufundishe thamani ya maisha. Usisubiri kifo kikufundishe kumtafuta Mungu. Usisubiri dakika za mwisho ndipo uanze kuishi kwa ajili ya Mungu.
Kwa sababu ukweli mchungu ni huu:
Sote tuna prognosis tofauti ni kwamba hakuna aliyetuambia tarehe yake.
Tafakari.
Chukua hatua.
Mungu atusaidie tusije tukatamani tungepewa zile siku tunazopoteza leo. 🙏
Joanah ,Nakufa ndoa yangu ikiwa changa ambayo hatujapata uzao wowote 😭😭
Nakufa namuacha baba yangu
Nakufa namuacha mama yangu
Ee Mungu
Wahivi hua siwaelewi kabisa, anataka afatwe pmKuna umuhimu gn wa kuandika hosp x, hosp m?
Wazo zuriNiko na mixed feelings yaani hata sielewi nikuandikie nini kikupe faraja 😭
Sema kama uwezo upo jaribu hospitals tofauti,ikiwezekana nenda hata nairobi ukapate second opinion.
Hizi hospital zetu za bongo kwakweli sio za kuziamini mara moja kwa issue nzito kama hizi,
Kivyovyote vile usikubali kuondoka kirahisi jaribu kupambania uhai wako as you said bado mdogo mno!
Kama wewe ni mfatiliaji wa mziki kuna msanii anaitwa BRACKET anatokea NIGERIA aliwai patwa na CANCER na akapona vizuri Tu ( kumaanisha CANCER ilikuwa stage ya mwanzo aliwai pata matibabu). Kwahiyo pia mleta mada asijikatie tamaa anaweza pona vizuri tu.YEAH NAAMINI HUYU SISTA ANAWEZA KUA ANAUMWA CANCER, ITS TRUE, NAKUMBUKA YULE WAZIRI, ALIKIA ANATOA STORI YA MAISHA YAKE ANADAI, SIKU HIYO ALITOKA DODOMA AKAPANDA NDEGE KWENDA DAR PALE MUHIMBILI ALIKUA AMEENDA CHECK UP, HAKUA NA TATIZO LOLOTE LOLE MWILI WAKE ULIKUA SAFI KABISA.
ILIKUA NI KAWAIDA YAKE KUFANYA CHECK UP, SASA KAFIKA MUHIMBILI, AKAMKUTA DOKTA KISENGE WAKATI HUO NDIO ALIKIA DOKTA WAKE WA CHECK UP, WALIFANYA CHECK UP, NA BAADAE ALIONDOKA KIA ATATUMIWA MAJIBU KWENYE SIMU. AKIMWAMBIA DEREVA WAKE WAWASHE GARI KURUDI DODOMA, WAKIWA NJIANI ALIPIGIWA SIMU NA DOKTA KISENGE, AKIULIZWA UKO WAPI MUHESHIMIWA, AKAJIBU YUPO NJIANI ANAELEKEA DODOMA KWENYE KIKAO, DOKTA KISENGE AKAMWAMBIA AGEUZE GARI HARAKA, AANZE SAFARI KWENDA INDIA MANA AMEBAINIKA NA CANCER, CHA KISHANGAZA HUYO WAZIRI HAKUA NA DALILI YOYOTE ILE KIA ANA UMWA.
IKABIDI AMWAMBIE DEREVA AGEUZE GARI KURUDI DAR WALIPO FIKA, AKAONANA NA DOKTA KISENGE, HAPO HAPO SAFARAI YA KWENDA INDIA IKAANZA, UNAAMBIWA KAFIKA INDIA BADO HAAMINI KINACHO TOKEA, AKASHANGAA ANA NYOLEWA NYWELE ZOTE NA MAISHA YA KITANDANI YA KAANZIA HAPO, HII STORI ILINIFIKIRISHA SANA KAMA KUNA MTU ANAMFAHAMU HUYU WAZIRI ATWAMBIE JINA LAKE JAPO MPAKA LEO BADO ANAISHI, STORI NIMEISOMA MAHALA HATA MIEZI MITATU HAIJAPITA, ALIKUA AKISIMULIA YEYE MAPITO YAKE, UNAAMBIWA INDIA ALIKAA KAMA MWAKA, ANAWASHUKURU WATOTO WAKE MKEWE NA FAMILIA YAKE KWA UJUMLA KUSIMAMA NAE.
Kaitoa aisee!Avatar yake n mdada mwenye rasta hv? Ambayo ndio ameitoa?
Duuh kuna umuhimu wa kufanya checkup mara kwa maraYEAH NAAMINI HUYU SISTA ANAWEZA KUA ANAUMWA CANCER, ITS TRUE, NAKUMBUKA YULE WAZIRI, ALIKIA ANATOA STORI YA MAISHA YAKE ANADAI, SIKU HIYO ALITOKA DODOMA AKAPANDA NDEGE KWENDA DAR PALE MUHIMBILI ALIKUA AMEENDA CHECK UP, HAKUA NA TATIZO LOLOTE LOLE MWILI WAKE ULIKUA SAFI KABISA.
ILIKUA NI KAWAIDA YAKE KUFANYA CHECK UP, SASA KAFIKA MUHIMBILI, AKAMKUTA DOKTA KISENGE WAKATI HUO NDIO ALIKIA DOKTA WAKE WA CHECK UP, WALIFANYA CHECK UP, NA BAADAE ALIONDOKA KIA ATATUMIWA MAJIBU KWENYE SIMU. AKIMWAMBIA DEREVA WAKE WAWASHE GARI KURUDI DODOMA, WAKIWA NJIANI ALIPIGIWA SIMU NA DOKTA KISENGE, AKIULIZWA UKO WAPI MUHESHIMIWA, AKAJIBU YUPO NJIANI ANAELEKEA DODOMA KWENYE KIKAO, DOKTA KISENGE AKAMWAMBIA AGEUZE GARI HARAKA, AANZE SAFARI KWENDA INDIA MANA AMEBAINIKA NA CANCER, CHA KISHANGAZA HUYO WAZIRI HAKUA NA DALILI YOYOTE ILE KIA ANA UMWA.
IKABIDI AMWAMBIE DEREVA AGEUZE GARI KURUDI DAR WALIPO FIKA, AKAONANA NA DOKTA KISENGE, HAPO HAPO SAFARAI YA KWENDA INDIA IKAANZA, UNAAMBIWA KAFIKA INDIA BADO HAAMINI KINACHO TOKEA, AKASHANGAA ANA NYOLEWA NYWELE ZOTE NA MAISHA YA KITANDANI YA KAANZIA HAPO, HII STORI ILINIFIKIRISHA SANA KAMA KUNA MTU ANAMFAHAMU HUYU WAZIRI ATWAMBIE JINA LAKE JAPO MPAKA LEO BADO ANAISHI, STORI NIMEISOMA MAHALA HATA MIEZI MITATU HAIJAPITA, ALIKUA AKISIMULIA YEYE MAPITO YAKE, UNAAMBIWA INDIA ALIKAA KAMA MWAKA, ANAWASHUKURU WATOTO WAKE MKEWE NA FAMILIA YAKE KWA UJUMLA KUSIMAMA NAE.
Nigeria mbali,Babuu wa Kitaa,yule pale ni Balozi wa kansa na ana Taasisi yake ya kupambana na KansaKama wewe ni mfatiliaji wa mziki kuna msanii anaitwa BRACKET anatokea NIGERIA aliwai patwa na CANCER na akapona vizuri Tu ( kumaanisha CANCER ilikuwa stage ya mwanzo aliwai pata matibabu). Kwahiyo pia mleta mada asijikatie tamaa anaweza pona vizuri tu.
Take Courage Dr. Sio Mungu.Hey people,
Uzi huu ni wa kuwaaga wanaJF wenzangu
Nimekutwa na cancer ambayo kimsingi nimepewa taarifa kwamba ndani ya miezi miwili sitakuwepo
Naumia lakini sina jinsi
Believe me, ukiweza kuishinda hiyo nafsi utaishi.Mimi sijakata tamaa lakini kuna nafsi inaniambia sifiki mbali
Barikiwa sanaAndiko hili limenitafakarisha sana. Tuache kwanza habari ya Joanah. Tujiulize sisi wenyewe, sisi ambao hatujui siku, saa, wala muda wetu umefika lini, tumejiandaaje?
Huenda unaandika hapa kumpa pole, kumwonea huruma au kumfariji mtoa mada kwa sababu ameambiwa ana prognosis ya miezi miwili au chini ya hapo.
Lakini hebu geuza swali hilo kwako mwenyewe. Kama ingekuwa wewe umeambiwa, “Una miezi miwili tu au chini ya hapo,” ungefanya nini?
Wengi wetu tungeanza kusema, Nitajikaribisha zaidi kwa Mungu. Nitatubu. Nitasali zaidi. Nitawaomba msamaha nilio wakosea. Nitawasamehe walionikosea. Nitakaa karibu na familia yangu na watu ninaowapenda. Nitatengeneza mambo yangu na Mungu.
Vizuri kabisa! Lakini swali ni hili, Kwa nini tusifanye hivyo sasa?
Kwa nini tusimtafute Mungu kwa moyo wote wakati bado hatujaambiwa tuna miezi miwili?
Kwa nini tusitubu leo, badala ya kusubiri siku tutakayoogopa kifo?
Kwa nini tusisamehe leo, badala ya kusubiri dakika za mwisho?
Kwa nini tusimpende Mungu leo kwa nguvu zetu zote, badala ya kusubiri mwili utakapokuwa hauna nguvu tena?
Tunajua kabisa kwamba kifo hakitupi appointment. Hakipigi simu kusema, “Nakuja kesho saa 10.” Hakituandikii ujumbe kusema, “Jiandae, zimebaki siku 30.”
Wengine wanapewa taarifa ya muda wao. Sisi wengine tunaishi bila taarifa hiyo.
Na labda hapo ndipo kuna tofauti kubwa.
Yeye amepewa kile ambacho sisi hatujapewa. Nafasi ya kuhesabu siku zake.
Lakini sisi tunaishi kana kwamba tumepewa miaka mingi.
Tunapanga kesho, mwezi ujao, mwaka ujao… lakini hatujui kama tutafika huko.
Huenda mtu anayejua amebakiza miezi miwili ndiye aliyeanza kuishi kwa umakini kuliko yule anayefikiri ana miaka ishirini mbele yake.
Kwa hiyo, tusimwangalie tu kwa huruma.
Tujitazame sisi wenyewe.
Kama leo ungeambiwa huu ndio mwezi wako wa mwisho, ungeendelea na maisha haya haya?
Ungeendelea kubeba chuki hiyo?
Ungeendelea kuahirisha toba?
Ungeendelea kusema, “Nitabadilika baadaye”?
Ungeendelea kuishi mbali na Mungu?
Kama jibu ni hapana, basi kwa nini unasubiri mpaka uambiwe una muda mfupi wa kuishi?
Neema si kuambiwa siku yako ya mwisho. Neema ni kupewa leo.
Leo bado unaweza kutubu.
Leo bado unaweza kusamehe.
Leo bado unaweza kurekebisha.
Leo bado unaweza kumtafuta Mungu.
Leo bado unaweza kusema, “Bwana, niko hapa.”
Kwa hiyo, huenda hatuna neema ya kujua tumebakiwa na muda gani kama alivyoambiwa yeye. Lakini tunayo neema kubwa zaidi ambayo mara nyingi tunaipuuza.
Tunaishi leo.
Na leo ndiyo siku ya kujiandaa.
Usisubiri prognosis ikufundishe thamani ya maisha. Usisubiri kifo kikufundishe kumtafuta Mungu. Usisubiri dakika za mwisho ndipo uanze kuishi kwa ajili ya Mungu.
Kwa sababu ukweli mchungu ni huu:
Sote tuna prognosis tofauti ni kwamba hakuna aliyetuambia tarehe yake.
Tafakari.
Chukua hatua.
Mungu atusaidie tusije tukatamani tungepewa zile siku tunazopoteza leo. 🙏
Anadeka 😂Wahivi hua siwaelewi kabisa, anataka afatwe pm
Pole saanaHey people,
Uzi huu ni wa kuwaaga wanaJF wenzangu
Nimekutwa na cancer ambayo kimsingi nimepewa taarifa kwamba ndani ya miezi miwili sitakuwepo
Naumia lakini sina jinsi
Nakufa ndoa yangu ikiwa changa ambayo hatujapata uzao wowote 😭😭
Nakufa namuacha baba yangu
Nakufa namuacha mama yangu
Ee Mungu