Mkuu BAK, unafahamu mimi nilikuwa mtundu sana na kwa sababu ya utundu huo nilianza kujifunza kusoma magazeti nikiwa na miaka mitatu kabla hata ya kwenda shule, kwahilo namshukuru sana marehemu mdingi ambae kila siku alikuwa akirudi na ama gazeti la Uhuru, Daily News, na Mzalendo.
Jumamosi ilikuwa ni bonus kwangu, kwasababu kulikuwa na magazeti matatu Uhuru , Daily News na Mfanyakazi.
Halafu mimi pia nilikuwa na tabia ya kukata picha na habari fulani muhimu sana na leo hii ningekuwa na nafasi fulani hivi kuchangia historia kwani nilikuwa na kumbukumbu zote za kesi ya uhaini, kesi ya mauaji ya Asha Mkwizu, uvunjaji wa baraza jipya la mawaziri aloufanya Alhaj Mzee Ali Hassan Mwinyi na pia nilikuwa ninayo picha ambayo Hayati Mwalimu Nyerere alipiga na akiwa Chamwino na mheshimiwa Seif Shariff Hamad kabla hatamvua uwaziri kiongozi.
Lakini kwa bahati mbaya nilikuja kupoteza "treasure" hiyo kwenye masuala ya kuhamahama kikazi.
Asikudanganye mtu BAK, Old Skool ndio yenyewe.