Kwa wanawake tu mwanaume usifungue hapa

Kwa wanawake tu mwanaume usifungue hapa

Jamani toka 2003, 3 yrs kabla ya ndoa na 9yrs sasa after ndoa sijawahi chepuka lknlkn kinachoniudhi no wanawake kudanganyana na kukosa kujiamini. Utasikia wanaume nyie mbwa tu, hakuna mwanaume asiye na mchepuko.ukishawaza tu hayo hutaishi kwa a man I wala kufurahia ndoa

Kweli kabisa!
Endelea hivyo hivyo mkuu

Wanawake tunaongea sn msamehe tu wifi
 
Sisi pia tunachangia sana wanaume zetu kuchepuka tunachangia kwa asilimia zote

sikubaliani na wewe kabisa mamii haiwezekani wanawake wote wachangie waume zao kuchepuka sema,kuchepuka ni kawaida yao so we have to live,with it as long as heshima ipo ndani ya ndoa/ mapenzi
 
Akirudi tu mvue suruali umnuse dushelee utajua tu na akijua unamfatilia kwa kumnusa ataacha kuchepuka

wengine wanachepukia sehemu safi kama guest house etc ina maana huyu akimaliza anaoga anajisafisha utamjua mama
 
Cheating ni stage katika ndoa...what matters ni aftermath...
Ukisusa wenzio wala...

Kwanza kuwa na msimamo; na usipanic...mwanaume ku sex nje ya ndoa inaweza isimaanishe kuwa hampendi mkewe...ni udadisi tu...wakisikia wanawake wa Tanga sijuhi nini wanataka wajaribu...wakisikia wa bara sijuhi nini wanataka wajaribu...wakisikia wenye wowowo sijuhi wakoje wanajaribu...

Na in all these experiments wanakuta hakuna jipya...lakini usipotumia busara wanaondoka kimoja japo aendako anajua fika hakuna la ziada...

Ila ukigundua unachitiwa na ukatumia busara kumrudisha mumeo kwenye mstari...itakuwa historia...

Siri kubwa ni kutotoa nafasi...kaba mpaka penati...jumamosi ni mtoko wa familia (na watoto) jumapili ni wa baba na mama...huyo wa pembeni ata enjoy mda gani?

Ukiona mabadiliko jigeuze FBI...si kumlilia Mungu wakati katupa mbinu za kuwalinda waume zetu...

Kingine jipende ili aogope kuwa akikuacha asubuhi jioni umeshapata mume mwingine...

Lazima ujiweke in such a way mumeo anakuwa na wasiwasi wa kukupoteza...ukiona wivu mumeo hana jiulize...labda umejiachia umechuja...

Additional like..nakupa nyingine 5
 
za saa hizi jamani? 50/50 hoyeeeee!!!!!!! nimesoma mada nimeielewa na michango pia. Wengi wetu kama si wote inaonekana kukubaliana ibara inayosema kwamba wanaume waendelee kuchiti kwa kuwa ni asili yao ilimradi watuheshimu (hapa kamati imekabiliwa na utata mkubwa kuhusu maana ya neno heshima). Hili la kujisopu sopu na kudayat na kupeleka maji bafuni (sijui wanawake wa masaki wenye maji na heater bafuni na mashine za kufulia hawana changamoto za michepukoo?) limepigiwa kura nyingi za ndiyo lakini naona nafasi yake ni ndogo sana kumaliza tatizo kwani tumeona waume wengi sana, si kidogo, wakisarandia wanawake wenzetu wasiojua kupaka wanja wala uturi halafu waneneee wakati wake zao wanakaribia kufanana na cleopatra. Wanawake wenzetu maskini wamejkuta wakikoboa mpaka ngozi kwa maji ya betri ili kmshawishi mume kwamba yeye ni mzuri. Yaani acheni tu! Hili la unyenyekevu labda, ila sijui inakuwaje unakuta mwanaume anakuwa na mke mnyenyekevu lakini anachepuka na kibinti (kianamke chenzetu, mtoto wa mwanamke mwenzetu) kinampeleksha mpaka anatia huruma- hafurukuti. Sijui ndo yale maombi ya jumamosi alosema lara???? Wengine tumeambiwa tuwabane bane twende nao mpirani, bar (sijui nao watakaa na sisi kuangalia isidingo zetu?), wikiendi mitoko na familia....haya, jumatatu mpaka ijumaa mida ya kazi tunafanyaje?

Wajumbe wengi wamepigia ibara ya MAOMBI kura ya ndiyooooo....Hapa sasa sina budi kuokoka maana maombi bila wokovu ni sawa kuwa na kuni bila kibiriti. Lakini hata nikiokoka nikawa nasugua goti majibu ya Mungu huwa hayaji mara zote kama ninavyotaka. Kuna kuletewa majaribu, na mojawapo ya majaribu ndo haya ya mume kuchepuka, ila akichepuka ilhali ulikuwa unaomba basi unageuza maombi unaomba mungu akuonyeshe nini kusudi lake katika jaribu hili, na akupe nguvu ya kusamehe ili usimuaibishe shetani kwa kukubali ndoa takatifu kusarambatika. Mwe!! Kwenye ibada za jumamosi nako tunakabiliwa na changamoto ya kuovadozi wenzi wetu kiasi cha kuwatoa uhai au kuwapotezea netwek kichwani.

Mheshimiwa mwenyekiti, ukijumlisha kura za kipengele cha maombi, ugagula, uvumilivu, kujipiga sop sop na kukaba mpaka penati, ukagawanya kwa ibara zote zilizojadiliwa, theluthi mbili wameonyesha wanaume ni wanyama - hawawezi kudhibiti. Lakini kwa kuwa demokrasia ni kukubali na kuheshimu maoni ya wachache, na kwa kuwa nia ya mjadala huu ni kuboresha ustawi wa familia kwa maslahi ya taifa, na kwa kuwa maoni ya wachache yanaonekana kutimiza lengo hilo, basi mheshimiwa mwenyekiti, wale waliosema wanaume ni binadamu walioumbwa kwa mfano wa mungu- wana utashi - wanaweza kujua jema na baya hivyo kuwa na uwezo kwa kufanya maamuzi sahihi, basi rasimu yenye mrengo huu ndiyo itakayopitishwa kwa ajili ya kupigiwa kura. WANAUME NI KIINI CHA MABADILIKO! (hapa sasa!) Naomba kuwasilisha.
 
Ile dhambi ya mwanamke mwenzenu Hawa haijatubiwa bado. Hiyo ndio inayowatesa na sio wanaume.
 
Kwa mtazamo wangu nikwamba mazoea ndiyo yanayotuaribia pia naubunifu.kama umefanya uchunguzi wenzetu wenye ngozi nyeupe unawakuta wanazeeka wakiwa bado unawaona wanapendana.1.Mazingira miaka mitatu hiyohiyo chumba hikohiko kitanda hikohiko kilipo geukia kulia ni hapohapo kwa hiyo mwanaume anaona kawaida sana au anaweza kuona kama uko sawa nae 2.ubunifu jaribu kufanya suprise labda jmos au ijumàa mpaka jumapili mnatoka mnatafuta hotel mnapumzika au kama hamjabahatika kupatika watoto mnaweza kufanya mapenzi hata sebuleni jikoni hata bafuni.nihayo tu wadau mtanisamehe kàma nitakuwa nimekosea
 
chamaana ni kujipenda na kumpenda mwenzako mpe mapenzi yote hata akitoka huko nje akumbue kuna mtu anayempenda zaidi amemwacha nyumbani, vinginevyo huwezi kumchunga mwanaume kama anatamaa anayo tu huwezi kuibadili
 
Wanaume kutoka nje sometimes kama nature yao vile ila sababu kubwa tunasababisha sie tunabana mchezo sana kila siku tukiombwa tumechoka mara tunaumwa hahahaha hebu tuwape mchezo hadi asubuh lol alafu tuone pumzi za kutoka nje atazitolea wapiiiii........

Kama unayo hio tabia jirekebishe shoga angu

Kwann huwa mnabania papuchi? farkhina
 
Back
Top Bottom