Na ukiweka dhana wanaume wote ndivyo walivyo na ndivyo itakavyo kuwa,
Waache wanasema kuwa ndivyo walivyo
Wewe kuwa tofauti sema wakwangu yupo tofauti na wengine, wangu analindwa na Mungu, na achilia hofu ya Mungu iingie ndani yake kamwe hato thubutu
Tusipende kuwa na ndoa za kigroup
Sijui naeleweka,?
Kigroup ni hivi , yaani kwakuwa wengine wanaume wengine wanacheat basi ni kawaida hata mimi ni kawaida. Kuwa mwanamke wa tofauti, hata kama wengine wooote watacheat sema wangu ni hato cheat nitakaa kumuombea kila siku, nitakaa katika zamu yangu kuomba vizuri
Wazungu wanasema unique
Sema mume wangu ni wa kipekee au ndoa yangu ni ya kipekee haifanani na mwingine,
Utaona utakuwa mwajibikaji katika maombi
Sio tu uombe asicheat, ombea na mengine kazi watoto uchumi ndugu elimu nk
Utaona ndoa ni nzuri
Niamin kuna ndoa zina raha sana hawajui hata shida na hii ni sababu wamemuweka Mungu kwanza, hata mikwaruzi ikitokea watasolve sababu Mungu wanamjua vyema
Mbinguni hatuolewi hivyo hakikisha ndoa yako ni paradiso ndogo hapa duniani na Mungu anachukia kuachana na anachukia uzinzi
Kaa zamu, narudia tena kaa zamu kaa zamu ya ulinzi katika maombi na sio kumchunguza bila kuomba ukaishia maumivu ya magonjwa
Mume wako akikukosea kama upo vizuri na Mungu utaona atajua tu sababu nilifanya kosa hili kwa mke hata kama hakuniona wapo wanao confess
Na ambao hamjaolewa fanya maombi ya akiba mapema kabla hujaingia katika ndoa.
Muda ukifika Mungu atayatumia hayo maombi
Wapo wanaume waaminifu sana hata kama wengine wakibisha, ila wapo sana tu
In ua Presence Jesus is where I belong