UZUSHI Kuvaa nguo nyekundu kunasababisha kupigwa na radi

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
1673611900113.png


Madai:
Yapo madai kutoka katika jamii mbalimbali yakihusisha rangi nyekundu na radi. Baadhi ya jamii zinaamini kwamba kuvaa mavazi yenye rangi nyekundu wakati wa mvua ni hatari kwa sababu yanaweza kusababisha ukapigwa na radi. Sambamba na hilo jamii nyingine zinaamini Mjusi kafiri na Kondoo wana uwezo wa kupambana na radi.
---
 
Tunachokijua
Radi ni mwangaza na miale ya mwanga mithili ya shoti za umeme inayotokea wakati wa ngurumo wa mvua ya radi. Neno radi linaweza kutaja pia sauti yenyewe na mwanga katikati ya mawingu unaweza kuitwa "umeme".

Asili yake ni volteji inayojijenga kati ya mawingu angani yenye chaji tofauti au pia kati ya mawingu na ardhi. Volteji hiyo ikiongezeka mno husababisha mkondo wa umeme hewani unaoonekana kama mwangaza mkali.

Mkondo unatoa pia joto kali na joto hilo husababisha kupanuka kwa hewa ghafla. Upanuzi huo unaleta sauti inayosikika kama ngurumo kama ni mbali, lakini inaweza kusikika pia sawa na mshtuko wa mlipuko kama ni karibu.
387px-Lightning_in_Arlington.jpg
Ni kweli kwamba kumekuwa na imani mbalimbali kwa jamii nyingi za Kiafrika Tanzania na Rwanda ikiwamo zinaitazama radi kijadi zaidi. Wapo wanaamini ni hatari kuvaa mavazi yenye rangi nyekundu wakati wa mvua kwa sababu mavazi hayo yanavutia radi kukufata. Hata hivyo, bado hakuna uthibitisho kamili unaobainisha chanzo cha jamii hizo kuamini hivyo.

Zipo Imani nyingine kadhaa za kijamii kuhusu radi ambapo pia baadhi ya jamii za Afrika ya sasa na Ugiriki zamani zinaamini radi zinatengenezwa na watu au miungu inatumika kama silaha ya kijadi kuwashambulia wengine au kutoa adhabu.

Hoja zote hizi ni sehemu ya hoja nyingine nyingi za kijamii kuhusu radi. Lakini hazithibitiki kisayansi

Je, sayansi inasema nini kuhusu uhusiano wa nguo nyekundu na radi?
Wataalamu wa hali ya hewa wanaeleza kuwa kwa tafiti zilizopo mpaka sasa ulimwenguni hakuna uhusiano wowote kati ya radi na rangi yoyote Ile. Mathalani, Wilbert Kikwasi wa TMA anaeleza kuwa radi inatokana na tofauti ya nguvu za umeme kati ya mawingu na ardhi. Anaongeza kuwa hakuna uthibitisho wa kisayansi unaobainisha namna rangi nyekundu inavyoweza kuchochea au kuvutia radi.

Zaidi ya hayo, Wataalamu wa masuala ya hali ya hewa wanafafanua kuwa Radi hutokana na kuachiliwa kwa umeme tuli, tukio ambalo hutokea kutokana na tofauti ya nguvu za umeme kati ya mawingu na ardhi. Radi ni Umeme ambao husafiri kutoka juu hadi chini na kwa kawaida hugonga vitu virefu zaidi.

Mazingira ya kupigwa na radi yanategemea zaidi kama umekaa kwenye vitu virefu kama miti, milima, kwenye minara shamba au kwenye mimea mifupi ambayo umeizidi Kimo n.k.
radi-pc-data.jpg

Hakuna uhusiano wowote kati ya nguo za rangi nyekundu na kupigwa na radi, JamiiForums inasisitiza kuchukua hatua za kitaalamu za kujikinga na radi kama, kutokaa chini ya miti na majengo marefu wakati wa mvua.
Yes hivi ni kweli, rangi hii huwa ina attract nguvu mbalibali, angalia hata katika mambo makubwa makubwa huwezi kosa
 
Mbona sayansi inaukataa ukweli kwamba radi ni kuku! Tena jogoo mwekundu kuanzia kucha Hadi utosini, tena anaevutia haswa.....ifike mahala tukubali ya kwamba, ya kaisari, hayathibitiki popote kisayansi!...inapoishia sayansi, ndipo anapoanzia.

yuko yeye yule jana,leo na hata milele..
 
Mbona sayansi inaukataa ukweli kwamba radi ni kuku! Tena jogoo mwekundu kuanzia kucha Hadi utosini, tena anaevutia haswa.....ifike mahala tukubali ya kwamba, ya kaisari, hayathibitiki popote kisayansi!...yuko yeye yule jana,leo na hata milele..
Wengine wanasema ni kondoo.

Haya mambo yapo. Ila inategemea kama huyo radi amekulenga wewe...utamuona akishuka na anavyotembea ila kama sio wa kutumwa hutaona mnyama
 
Nijitahidi kuelezea kwa lugha rahisi:

Kujua kama kuna aina fulani ya nguo au rangi fulani inaweza kuvuta radi, yabidi ufahamu radi ni nini.

Nadhani kila mmoja amewahi kuchukua plastic au kitana cha plastic, akakisugua sana kwenye nywele zake, halafu upeleke plastic hiyo kwenye karatasi. Plastic itaivuta karatasi, na baadaye huachia. Kitendo hiki nakifananisha na radi inavyotengenezeka.

Kwenye anga, mawingu husuguana, msuguano huo huwa ni mkubwa kiasi cha kutengeneza kiwango kikubwa sana cha charge za umeme, negative na positive. Msuguano huo husababisha joto kali mpaka kufikia nyuzi joto sentigredi 25,000. Ufahamu kuwa chuma huyeyuka kwenye nyuzi joto sentigredi 800 tu.

Charge hizi zinafuata kanuni ya umeme yaani wakati wote zinatafuta low potential energy ambayo ni ardhi. Zinashindwa mara mpoa kwenda ardhini kwa sababu hewa ni poor conductor. Lakini charge hizi zinapofikia kiwango kikubwa sana, na kusababisha joto kali, hewa hulazimishwa kuwa conductor, na kuzipitisha hizi charge kuelekea ardhini, ambayo ni low potential area. Kwa vile hewa ni poor conductor, charge hizi zinaposhuka wakati wote hutafuta conductor iliyo bora zaidi kuliko hewa. Kama kuna jengo refu, mti mrefu, mnara mrefu, basi zitaamua kupitia hapo, na kwa vile charge hizi zimebeba joto kubwa, zikipitia kwenye mti mrefu, utachanika na kukauka, kama mtu alisimama chini ya huo mti, naye atakaushwa (kumbuka kanuni ya umeme: katika kwenda kwenye low potential area, always seeks the shortest path possible). Kama binadamu umesimama kwenye uwanda wa wazi, hakuna miti wala kitu kilicho kirefu kukuzidi wewe, shortest path kufikia ardhi itakuwa ni kupitia kwako, na hapo ndiyo tunasema, mtu amepigwa na radi.

Kanuni ya charge, kama ilivyofanyiwa kazi na mtaalam Faraday, charge hazipenyi kwenye sphere, zitaizunguka tu. Ndiyo maana huwezi kusikia gari limepigwa na radi. Kwa sababu lenyewe ni kama sphere, charge zitazunguka nje, hazitapenya ndani, na kwa vile tairi ni mpira, ambao ni non-conductor, basi gari haitakuwa the shortest path ya kupeleka charge za umeme ardhini. Kipindi cha mvua, kama unaendesha gari, na kulikuwa na radi, usipende kulishika gari kwa nje wakati unashuka, kunaweza kuwa na charge za umeme wa radi ambazo hazijapata njia ya kwenda ardhini, ukishika zitapitia mwilini mwako, utapata mshtuko, lakini hazina uwezo wa kuua kwa sababu huwa ni kiasi kidogo.

Kanuni nyingine ni charge hizi kupenda sharp point, yaani ukiwa na chuma kipana na kingine kimechongoka, charge za radi zitapitia kwenye kile chuma kilichochongoka. Ndiyo maana ile mitego ya radi kwenye majengo marefu ni chuma chembamba kilichochongoka kitakachozidi kidogo urefu wa jengo, na lazima kiwe conductor nzuri. Radi kwa kutafuta shortest distance na kanuni ya kutafuta sharp point, lazima ipige hapo.

Radi ni discharge ya umeme kutoka kwenye atmosphere, hazina macho wala hazina uhai, haziwezi kutambua rangi ya kitu. Hivyo, hakuna rangi ambayo inavuta radi.

Mnyama kondoo hawezi kupigana na radi, bali mwanga mkali wa radi humshtua. Kondoo kama ilivyo kiumbe kingine chochote, akiwa kwenye njia ya radi inapoelekea ardhini, naye atapigwa na kufa. Huko Georgea, Marekani, kondoo wapatao 500 walipigwa na radi na wote kufa kwa pamoja.
 
Nijitahidi kuelezea kwa lugha rahisi:

Kujua kama kuna aina fulani ya nguo au rangi fulani inaweza kuvuta radi, yabidi ufahamu radi ni nini.

Nadhani kila mmoja amewahi kuchukua plastic au kitana cha plastic, akakisugua sana kwenye nywele zake, halafu upeleke plastic hiyo kwenye karatasi. Plastic itaivuta karatasi, na baadaye huachia. Kitendo hiki nakifananisha na radi inavyotengenezeka...
Ahsante kwa elimu nzuri
 
Inawezekana kwenye hilo eneo wewe ndiyo ukawa kitu kirefu alafu umevaa nyekundu... kitakachokupata...
 
radi inategemea na itakachoanza kukutana nacho kirefu zaidi ya kingine. ila sio rangi
 
Nijitahidi kuelezea kwa lugha rahisi:

Kujua kama kuna aina fulani ya nguo au rangi fulani inaweza kuvuta radi, yabidi ufahamu radi ni nini.

Nadhani kila mmoja amewahi kuchukua plastic au kitana cha plastic, akakisugua sana kwenye nywele zake, halafu upeleke plastic hiyo kwenye karatasi. Plastic itaivuta karatasi, na baadaye huachia. Kitendo hiki nakifananisha na radi inavyotengenezeka...
Umeeleza vizuri Mkuu

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Inategemea uko wapi na umekutana na radi ya aina gani, kama ni hii ya kisayansi tunayoijua wote sawa, ila kama ndio uko nyanda za juu kusini na ukakutana na ile radi ya kichawi, unaweza usipate huo muda wa kujuta kwamba hatukwambia, shauri yenu mengine msijaribu hasa mkiingia anga za watu! Iteni tu uzushi
 
Mkuu ahasante kwa elimu hii ya bure, nimeitafuta kwa miaka mingi kuijua.
Barikiwa sana.
 
Nijitahidi kuelezea kwa lugha rahisi:

Kujua kama kuna aina fulani ya nguo au rangi fulani inaweza kuvuta radi, yabidi ufahamu radi ni nini.

Nadhani kila mmoja amewahi kuchukua plastic au kitana cha plastic, akakisugua sana kwenye nywele zake, halafu upeleke plastic hiyo kwenye karatasi. Plastic itaivuta karatasi, na baadaye huachia. Kitendo hiki nakifananisha na radi inavyotengenezeka.

Kwenye anga, mawingu husuguana, msuguano huo huwa ni mkubwa kiasi cha kutengeneza kiwango kikubwa sana cha charge za umeme, negative na positive. Msuguano huo husababisha joto kali mpaka kufikia nyuzi joto sentigredi 25,000. Ufahamu kuwa chuma huyeyuka kwenye nyuzi joto sentigredi 800 tu.

Charge hizi zinafuata kanuni ya umeme yaani wakati wote zinatafuta low potential energy ambayo ni ardhi. Zinashindwa mara mpoa kwenda ardhini kwa sababu hewa ni poor conductor. Lakini charge hizi zinapofikia kiwango kikubwa sana, na kusababisha joto kali, hewa hulazimishwa kuwa conductor, na kuzipitisha hizi charge kuelekea ardhini, ambayo ni low potential area. Kwa vile hewa ni poor conductor, charge hizi zinaposhuka wakati wote hutafuta conductor iliyo bora zaidi kuliko hewa. Kama kuna jengo refu, mti mrefu, mnara mrefu, basi zitaamua kupitia hapo, na kwa vile charge hizi zimebeba joto kubwa, zikipitia kwenye mti mrefu, utachanika na kukauka, kama mtu alisimama chini ya huo mti, naye atakaushwa (kumbuka kanuni ya umeme: katika kwenda kwenye low potential area, always seeks the shortest path possible). Kama binadamu umesimama kwenye uwanda wa wazi, hakuna miti wala kitu kilicho kirefu kukuzidi wewe, shortest path kufikia ardhi itakuwa ni kupitia kwako, na hapo ndiyo tunasema, mtu amepigwa na radi.

Kanuni ya charge, kama ilivyofanyiwa kazi na mtaalam Faraday, charge hazipenyi kwenye sphere, zitaizunguka tu. Ndiyo maana huwezi kusikia gari limepigwa na radi. Kwa sababu lenyewe ni kama sphere, charge zitazunguka nje, hazitapenya ndani, na kwa vile tairi ni mpira, ambao ni non-conductor, basi gari haitakuwa the shortest path ya kupeleka charge za umeme ardhini. Kipindi cha mvua, kama unaendesha gari, na kulikuwa na radi, usipende kulishika gari kwa nje wakati unashuka, kunaweza kuwa na charge za umeme wa radi ambazo hazijapata njia ya kwenda ardhini, ukishika zitapitia mwilini mwako, utapata mshtuko, lakini hazina uwezo wa kuua kwa sababu huwa ni kiasi kidogo.

Kanuni nyingine ni charge hizi kupenda sharp point, yaani ukiwa na chuma kipana na kingine kimechongoka, charge za radi zitapitia kwenye kile chuma kilichochongoka. Ndiyo maana ile mitego ya radi kwenye majengo marefu ni chuma chembamba kilichochongoka kitakachozidi kidogo urefu wa jengo, na lazima kiwe conductor nzuri. Radi kwa kutafuta shortest distance na kanuni ya kutafuta sharp point, lazima ipige hapo.

Radi ni discharge ya umeme kutoka kwenye atmosphere, hazina macho wala hazina uhai, haziwezi kutambua rangi ya kitu. Hivyo, hakuna rangi ambayo inavuta radi.

Mnyama kondoo hawezi kupigana na radi, bali mwanga mkali wa radi humshtua. Kondoo kama ilivyo kiumbe kingine chochote, akiwa kwenye njia ya radi inapoelekea ardhini, naye atapigwa na kufa. Huko Georgea, Marekani, kondoo wapatao 500 walipigwa na radi na wote kufa kwa pamoja.
Mkuu ahsante kwa Elimu hii ya bure. Nimeitafuta muda mrefu sikuipata.
Ubarikiwe sana
 
Nijitahidi kuelezea kwa lugha rahisi:

Kujua kama kuna aina fulani ya nguo au rangi fulani inaweza kuvuta radi, yabidi ufahamu radi ni nini.

Nadhani kila mmoja amewahi kuchukua plastic au kitana cha plastic, akakisugua sana kwenye nywele zake, halafu upeleke plastic hiyo kwenye karatasi. Plastic itaivuta karatasi, na baadaye huachia. Kitendo hiki nakifananisha na radi inavyotengenezeka.

Kwenye anga, mawingu husuguana, msuguano huo huwa ni mkubwa kiasi cha kutengeneza kiwango kikubwa sana cha charge za umeme, negative na positive. Msuguano huo husababisha joto kali mpaka kufikia nyuzi joto sentigredi 25,000. Ufahamu kuwa chuma huyeyuka kwenye nyuzi joto sentigredi 800 tu.

Charge hizi zinafuata kanuni ya umeme yaani wakati wote zinatafuta low potential energy ambayo ni ardhi. Zinashindwa mara mpoa kwenda ardhini kwa sababu hewa ni poor conductor. Lakini charge hizi zinapofikia kiwango kikubwa sana, na kusababisha joto kali, hewa hulazimishwa kuwa conductor, na kuzipitisha hizi charge kuelekea ardhini, ambayo ni low potential area. Kwa vile hewa ni poor conductor, charge hizi zinaposhuka wakati wote hutafuta conductor iliyo bora zaidi kuliko hewa. Kama kuna jengo refu, mti mrefu, mnara mrefu, basi zitaamua kupitia hapo, na kwa vile charge hizi zimebeba joto kubwa, zikipitia kwenye mti mrefu, utachanika na kukauka, kama mtu alisimama chini ya huo mti, naye atakaushwa (kumbuka kanuni ya umeme: katika kwenda kwenye low potential area, always seeks the shortest path possible). Kama binadamu umesimama kwenye uwanda wa wazi, hakuna miti wala kitu kilicho kirefu kukuzidi wewe, shortest path kufikia ardhi itakuwa ni kupitia kwako, na hapo ndiyo tunasema, mtu amepigwa na radi.

Kanuni ya charge, kama ilivyofanyiwa kazi na mtaalam Faraday, charge hazipenyi kwenye sphere, zitaizunguka tu. Ndiyo maana huwezi kusikia gari limepigwa na radi. Kwa sababu lenyewe ni kama sphere, charge zitazunguka nje, hazitapenya ndani, na kwa vile tairi ni mpira, ambao ni non-conductor, basi gari haitakuwa the shortest path ya kupeleka charge za umeme ardhini. Kipindi cha mvua, kama unaendesha gari, na kulikuwa na radi, usipende kulishika gari kwa nje wakati unashuka, kunaweza kuwa na charge za umeme wa radi ambazo hazijapata njia ya kwenda ardhini, ukishika zitapitia mwilini mwako, utapata mshtuko, lakini hazina uwezo wa kuua kwa sababu huwa ni kiasi kidogo.

Kanuni nyingine ni charge hizi kupenda sharp point, yaani ukiwa na chuma kipana na kingine kimechongoka, charge za radi zitapitia kwenye kile chuma kilichochongoka. Ndiyo maana ile mitego ya radi kwenye majengo marefu ni chuma chembamba kilichochongoka kitakachozidi kidogo urefu wa jengo, na lazima kiwe conductor nzuri. Radi kwa kutafuta shortest distance na kanuni ya kutafuta sharp point, lazima ipige hapo.

Radi ni discharge ya umeme kutoka kwenye atmosphere, hazina macho wala hazina uhai, haziwezi kutambua rangi ya kitu. Hivyo, hakuna rangi ambayo inavuta radi.

Mnyama kondoo hawezi kupigana na radi, bali mwanga mkali wa radi humshtua. Kondoo kama ilivyo kiumbe kingine chochote, akiwa kwenye njia ya radi inapoelekea ardhini, naye atapigwa na kufa. Huko Georgea, Marekani, kondoo wapatao 500 walipigwa na radi na wote kufa kwa pamoja.
Hii ndio JF ninayo ijua tangu miaka na miaka. Watu wa aina yako wamepungua sana humu jukwaani. Tumebaki na vijana wa hovyo. Hongera sana mkuu.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom