Kutoka kwenye familia tuliyosomeshwa kwa gharama kubwa kumeniathiri kiuchumi, Kupeleka watoto kayumba ni aibu, Napambana kukwepa aibu

Mtoto wa Kayumba form anapata division one, wewe umetumia miaka minne kulipa school total million 20 halafu mtoto anapata division two.

Wazazi tuanze kutumia akili, wazazi wengi hawana akili hata kama wana degree.
Duh leo Dokta Manyaunyau umeongea pwenti
 
Wewe wazazi wako wanajivunia nn kutoka kwako ?
Maana wanasema utakachowatendea wazazi wako ndicho watoto wako watakutendea
Kwakweli sijui ndgu yangu, hilo wanajua wao mioyoni mwao ila nachoshukuru Mungu ni kua hawakua wanalalamika kama wazazi wa miaka hii, wala kua na stress za ada na malezi.
 
Chekechea na Primary nimesoma english medium private.

Sekondari Form 1 hadi 6 nimesoma Boarding private, Msosi Pilau kila J5 na J2, Ugali ni nadra sana.

Chuo kikuu sikupata mkopo ila si haba sikuwahi kupata changamoto za kiuchumi.

Rasmi na mimi nikawa baba, nikaanza kuwaza watoto waje kusoma KAYUMBA wakati mimi sijasoma huko ?

Hali yangu ni tofauti na waliowahi kusoma kayumba wao hata wakiwa matajiri wanaweza kusomesha watoto kayumba kwa uhuru, wana uzoefu na hizo shule kwahiyo wanaweza kuwasaidia watoto mawazo na ushauri, sasa mimi sijasoma kayumba wala siyajui mazingira yapoje nitamshauri nini mtoto ?

Natoa mfano mwepesi hata kama umesoma kayumba lakini ulipambaniwa ule milo mitatu, ni kwamba na wewe ukiwa mzazi kuna msukumo unakuingia upambane watoto wale milo mitatu, ukikutana na mzazi aliekulia maisha ya milo miwili nae analisha watoto mara mbili, akikupa ushauri kwamba ulishe watoto mara mbili ni ngumu kumuelewa hata kama watoto wake wana nguvu na afya kuzidi wako.

Ndivyo ilivyo kwa upande wangu, nilipambaniwa ili maisha yangu ya shule yawe mepesi ni ngumu mimi kuwapeleka watoto Kayumba, pia hata wazazi watanichukuliaje ? wamenipambania nisome kwa raha kisha waje kuona wajukuu wanaenda kayumba ?


Kwa sasa nina watoto watatu nawapambania wasije pitia maisha ambayo mimi sikupitia,
  • First yupo form 1 boarding, ada milioni 2 na nusu kwa mwaka
  • wa pili yupo Primary day ada laki 9.
  • Huyu mwengine nae soon anaanza shule hio ya laki 9
  • Sina mpango wa kuongeza mtoto wa ziada labda uchumi ukae sawa

Suala la kufaulu wapo wanafunzi wanaokalia ndoo wanapasua vibaya mno, Kusomesha private kumelenga zaidi kumrahishia mtoto maisha ya shuleni

  • Vyoo visafi kila siku vinasafishwa
  • Chakula kizuri shuleni
  • Mazingira tulivu
  • Usafiri shuleni hadi nyumbani
  • kutumia kiingereza kwenye masomo tangu shule ya msingi
  • Kila mwanafunzi ana kiti na dawati lake
  • Hakuna kujazana darasani
  • kujifunza computer utotoni
  • Library
  • masomo ya kupika, kushona, kuchora, n.k.
  • watoto wengi hutokea familia zinazojali malezi na maadili.
  • n.k.

Ninajua zipo shule za bei rahisi mfano kuna shule za serikali za englsh medium, shule za sekondari za jumuia ya wazazi, n.k. kwa research yangu zimetofautiana kidogo na Kayumba.

Kwa sasa nina miaka 36 kiuchumi bado najibana sana hasa kwasababu bado najenga ili nihamie kwangu, imenibidi nitembelea IST ili kupunguza gharama za usafiri, Simu yangu ina miaka mitatu sijabadili, wife nae nashukuru anajua tunayopitia nae kapunguza vizinga
Ofcourse kama nimesoma shule bora siwez peleka wanangu Kayumba. Wazazi walipambana, namimi lazima nipambane
 
Chekechea na Primary nimesoma english medium private.

Sekondari Form 1 hadi 6 nimesoma Boarding private, Msosi Pilau kila J5 na J2, Ugali ni nadra sana.

Chuo kikuu sikupata mkopo ila si haba sikuwahi kupata changamoto za kiuchumi.

Rasmi na mimi nikawa baba, nikaanza kuwaza watoto waje kusoma KAYUMBA wakati mimi sijasoma huko ?

Hali yangu ni tofauti na waliowahi kusoma kayumba wao hata wakiwa matajiri wanaweza kusomesha watoto kayumba kwa uhuru, wana uzoefu na hizo shule kwahiyo wanaweza kuwasaidia watoto mawazo na ushauri, sasa mimi sijasoma kayumba wala siyajui mazingira yapoje nitamshauri nini mtoto ?

Natoa mfano mwepesi hata kama umesoma kayumba lakini ulipambaniwa ule milo mitatu, ni kwamba na wewe ukiwa mzazi kuna msukumo unakuingia upambane watoto wale milo mitatu, ukikutana na mzazi aliekulia maisha ya milo miwili nae analisha watoto mara mbili, akikupa ushauri kwamba ulishe watoto mara mbili ni ngumu kumuelewa hata kama watoto wake wana nguvu na afya kuzidi wako.

Ndivyo ilivyo kwa upande wangu, nilipambaniwa ili maisha yangu ya shule yawe mepesi ni ngumu mimi kuwapeleka watoto Kayumba, pia hata wazazi watanichukuliaje ? wamenipambania nisome kwa raha kisha waje kuona wajukuu wanaenda kayumba ?


Kwa sasa nina watoto watatu nawapambania wasije pitia maisha ambayo mimi sikupitia,
  • First yupo form 1 boarding, ada milioni 2 na nusu kwa mwaka
  • wa pili yupo Primary day ada laki 9.
  • Huyu mwengine nae soon anaanza shule hio ya laki 9
  • Sina mpango wa kuongeza mtoto wa ziada labda uchumi ukae sawa

Suala la kufaulu wapo wanafunzi wanaokalia ndoo wanapasua vibaya mno, Kusomesha private kumelenga zaidi kumrahishia mtoto maisha ya shuleni

  • Vyoo visafi kila siku vinasafishwa
  • Chakula kizuri shuleni
  • Mazingira tulivu
  • Usafiri shuleni hadi nyumbani
  • kutumia kiingereza kwenye masomo tangu shule ya msingi
  • Kila mwanafunzi ana kiti na dawati lake
  • Hakuna kujazana darasani
  • kujifunza computer utotoni
  • Library
  • masomo ya kupika, kushona, kuchora, n.k.
  • watoto wengi hutokea familia zinazojali malezi na maadili.
  • n.k.

Ninajua zipo shule za bei rahisi mfano kuna shule za serikali za englsh medium, shule za sekondari za jumuia ya wazazi, n.k. kwa research yangu zimetofautiana kidogo na Kayumba.

Kwa sasa nina miaka 36 kiuchumi bado najibana sana hasa kwasababu bado najenga ili nihamie kwangu, imenibidi nitembelea IST ili kupunguza gharama za usafiri, Simu yangu ina miaka mitatu sijabadili, wife nae nashukuru anajua tunayopitia nae kapunguza vizinga
Tofauti ya english medium na kayumba ni ndogo sana kiuhalisia ila binafsi huwa naona.
English medium zinaigiza maisha ya kizungu ihali sisi si wazungu na (kifupi hawa watoto ndio wakikua wanaleta stress kwenye falimia zao wanaforce kuishi kizungu) na kayumba zinaishi kiuhalisia kabisa kulingana na mazingira yetu.
 
Watoto kusoma ama kupata elimu nzuri ni wajibu wa mzazi lakini hakuwezi kunifanya nikose usingizi ni wapi wapate hiyo elimu. Kulingana na kipato chàngu wanangu watasoma mahala popote. Thanks
 
Kwa mfano mwepesi hata kama umesoma kayumba lakini ulipambaniwa ule milo mitatu (breakfast, lunch na dinner), ni kwamba na wewe ukiwa mzazi kuna msukumo unakuingia upambane kuhakikisha watoto wanakula milo mitatu, vinginevyo ni aibu yako binafsi hata kama utaifanya iwe siri.

Mtu aliekuzwa kwa milo miwili kwake kawaida kuja kulisha watoto milo miwili, akikwambia na wewe uwalishe watoto milo miwili ni ngumu kumuelewa.
Try to be open minded usitumie nguvu kubwa kubishana kwa mifano na mawazo yawatu yatakayoweza kukupatia idea nzuri nn ufanye

Maana at the end of day ni ww na familia yako mkuu na chaguo ni lako ufanyeje

Kwa kuleta mada kunakitu umeisi hakiendi sawa sasa acha sindano ziingie ,kupona kwake ukae chini na mawazo yaliyotolewa na members afu upate conclusion yaunachoisi hakipo sawa kwa unachofanya now
 
Kweli mkuu pambana ufanikishe hilo kusudio lako, tuliosoma Shule za kata tumeshuhudia uozo mwingi sana wa Elimu na ukijitia kuhoji tuu unashutumiwa ni Usalama wa taifa

Shule za kata walimu wengi ni vigagula( wachawi) hata vile wqnafunzi wanafail kwao ni Furaha kwasababu wao wenyewe watoto wao hawasomi hizo Shule
 
naomba nikupe mfano mdogo tu mkuu, wewe kwenu mlikuwa mnakula milo mitatu kila siku, hutajihisi uchungu watoto wako wakila milo miwili ?
Swali langu la msingi hujalijibu kwenye huo mfano wako, ingekuwa uko huru hubanwi na historia ya makuzi yako..... wanao ungesomesha Kayumba?
 
Dadeki noma sana.

Hivi watoto huwa wanawasaidia nini maishani?? Zaidi ya wengi kulalamika, sionagi watu wakisifia uwepo wao.
(Tafiti nimeifanyia jf na mtaani)
Duh! Mbona wanitoa kwenye kona? Kwangu furaha kubwa kuliko zooote, ni kuwa na watoto wangu pamoja. Nagamani niwe nao wengi iwezekanavyo.
Mtoa mad hongera kwa mpango wako. Ila ongeza watoto taf walau wafikie 5
 
Duh! Mbona wanitoa kwenye kona? Kwangu furaha kubwa kuliko zooote, ni kuwa na watoto wangu pamoja. Nagamani niwe nao wengi iwezekanavyo.
Mtoa mad hongera kwa mpango wako. Ila ongeza watoto taf walau wafikie 5
Ndo msilalamike sasa, na pia msione ugumu kuwapa wakitakacho.

Na siku nyingine mje na nyuzi kuwasifia watoto wenu, sio za lawama tu.
 
Swali langu la msingi hujalijibu kwenye huo mfano wako, ingekuwa uko huru hubanwi na historia ya makuzi yako..... wanao ungesomesha Kayumba?
offcourse ningeweza kuchagua wasome kayuma ama private.

Kama ningekuwa nimesoma kayumba ningekuwa na uzoefu kwenye mazingira, changamoto, wanafunzi, n.k. hivyo ningeweza kumpa ushauri mtoto jinsi ya kuweza kufit kwenye hizo shule.
 
Back
Top Bottom