Kutoka Dodoma!

Kutoka Dodoma!

Katika mjadala huu bado kuna kitu kimoja ambacho hakijazungumzwa nami napenda nikiweke wazi. Inasemekana kamera za usalama zilikuwa zimezimwa, swali la kujiuliza ni kwamba kwa nini kamera za usalama zilikuwa zimezimwa? Kwa sababu, kimantiki kamera za usalama zinatakiwa ziwe zinafanya kazi muda wote 24/7, kuwe na vikao ndani au visiwepo. Maana lengo la kamera siyo kutoa ulinzi wakati vikao vikiendela ndani tu bali kuchukua kumbukumbu ya jambo lolote linalofanyika ndani ya ukumbi wa bunge, liwe la uhalifu au la, kuwe na vikao ndani au kusiwe na vikao maana jengo lile linatakiwa kulindwa dhidi ya vitendo vyovyote vya kihalifu kama vile ugaidi n.k.

Viongozi wa bunge na wanaoshughulika usalama bungeni wanatakiwa watueleza kwa nini kamera za usalama zinazimwa wabunge wanapomaliza shughuli ndani ya jengo, kitu ambacho hakitakiwi kufanyika.
 
Nawaonea huruma sana familia ya chenge!kumbe Namge wa nyumba yao ni mtu anaeamini mambo ya kwa sangoma!Kweli za mwizi arobaini MUNGU kawaaibisha na unyatuzu wao!Wanyatunzu wanajidai sana sasa atakoma!hiloooooooo!iNAELEKEA hii tabia ni ya kwake kabisa naona jamaa alikuwa anaweka dawa ili kuwapoza hao wabunge labda ni machachari na wanatetea maslah ya taifa letu!Du aibu kweli kwa wanafamilia!
 
Inasemekana kamera za usalama zilikuwa zimezimwa, swali la kujiuliza ni kwamba kwa nini kamera za usalama zilikuwa zimezimwa? Kwa sababu, kimantiki kamera za usalama zinatakiwa ziwe zinafanya kazi muda wote 24/7, kuwe na vikao ndani au visiwepo.

Inawezekana kabisa na wao wapo katika huu mchongo maana tulishatahadharishwa kwamba shughuli zao aghalabu si kwa maslahi ya taifa ila usalama wa watawala.
 
Kutoka huko Dom nimepata ndogondogo kuwa timu ya RPC imeshakamilisha upelelezi wake. Naamini Mkuu ESFM utakuwa sambamba kutuhabarisha maana huenda wakamwaga maneno baadaye leo
 
Katika mjadala huu bado kuna kitu kimoja ambacho hakijazungumzwa nami napenda nikiweke wazi. Inasemekana kamera za usalama zilikuwa zimezimwa, swali la kujiuliza ni kwamba kwa nini kamera za usalama zilikuwa zimezimwa? Kwa sababu, kimantiki kamera za usalama zinatakiwa ziwe zinafanya kazi muda wote 24/7, kuwe na vikao ndani au visiwepo. Maana lengo la kamera siyo kutoa ulinzi wakati vikao vikiendela ndani tu bali kuchukua kumbukumbu ya jambo lolote linalofanyika ndani ya ukumbi wa bunge, liwe la uhalifu au la, kuwe na vikao ndani au kusiwe na vikao maana jengo lile linatakiwa kulindwa dhidi ya vitendo vyovyote vya kihalifu kama vile ugaidi n.k.

Viongozi wa bunge na wanaoshughulika usalama bungeni wanatakiwa watueleza kwa nini kamera za usalama zinazimwa wabunge wanapomaliza shughuli ndani ya jengo, kitu ambacho hakitakiwi kufanyika.


Ngereja that is a million dollar question, which will give us answers. Kama hili suala lisiposhughulikiwa ipasavyo tutakuwa tunaona kwa mara nyingine uozo uliopo ndani ya taasisi zetu. I can not imagine mtu anacheza na sehemu amabao kuwa watu waliochaguliwa na mamilioni ya watanzania. I look at this from that Angle first. Then we can talk about that potion later. I am sure sio usangoma, and i believe Harrison is on the way, jamaa asingehangaika kuweka mitishamba itakuwa ni polonium type of a thing.
 
Kutoka huko Dom nimepata ndogondogo kuwa timu ya RPC imeshakamilisha upelelezi wake. Naamini Mkuu ESFM utakuwa sambamba kutuhabarisha maana huenda wakamwaga maneno baadaye leo


Ndugu yangu umesema PRC Dodoma, una hakika kama kweli wana uwezo wa kweli kufanya kazi hii? una uhakika kama kweli uchunguzi wao ulikuwa free bila kuwa na influence yoyote. I am sure hata kilichonyunyizwa inawezekana hawakijui. Huenda hata hawakuwa na lab technician hata mmoja!
 
Maoni ya Wasomaji (Tanzania Daima)


NI ANDREW CHENGE MHITIMU WA Hogwarts School of Witchcraft and Wizardry ALIYOSOMA HARRY POTTER!

na mjusi, dar, - 15.06.08 @ 09:13 | #16590






kweli kama ni chenge!Basi tu i cant beliave my iyiz!Shetani ni mbaya sana!watu wataogopa kuoa nyumbani wakijua ukoo wote ni walozi!sijui tutaolewa?eeh MUNGU tusaidie!for sure inauma sana tena sana

na Hollo, USA, - 15.06.08 @ 09:27 | #16594



Chenge! Chenge! Chenge!
Jana amehojiwa na polisi. Fisadi jizi halafu chawi. Lakuvishwa tairi achomwe moto.

na bigup, tz, - 15.06.08 @ 09:41 | #16596



http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/6/15/habari1.php
 
Bunge la wabunge wanaoogopa ushirikina? Wao wenyewe kabla ya kuingia bungeni, wengi wao walitembea uchi makaburini.

Halafu tunashangaa nchi yetu iko nyuma, kama tunaongozwa na hawa wajinga, unafikiri tutegemee nini?

Mtanzania, inawezekana sisi na wenye magazeti ndio wajinga kwa kuacha kujadili uwezekano wa kuwapo kemikali hatari tunasisitiza ni uchawi kama vile tumethibitisha ni uchawi ama tunaendeleza mkakati wa hao jamaa wa kutulazimisha tuache kujadili jambo zito kama ambavyo Amina Chifupa, alielezwa kwamba ni uchawi na watu wakahangaika na uchawi hadi walipozinduka na kumpeleka Lugalo, hali ilikua imebadilika na kuwa haiwezekani kabisa. NASISITIZA Mwakyembe/Spika wanalifahamu hilo na hawaliangalii kwa upande wa uchawi wanaliangalia kisayansi zaidi, hata kama SPika naye anakua makini kujifanya anazungumzia uchawi lakini linaangaliwa kwa makini zaidi. Kawaida mtu anaweza kutumia mbinu hyata akaweka kemikali katika kibuyu (japo hakuweka) ili akili zenu zione ni uchawi na kwa kuwa ni WASOMI mutadharau na kuacha ifanye kazi vyema. INAWEZEKANA NI HUO UJINGA WA KISHIRIKINA LAKINI TUSIUPE UZITO TUSISITIZE UCHUNGUZI WA KISAYANSI ZAIDI
 
kweli kama ni chenge!Basi tu i cant beliave my iyiz!Shetani ni mbaya sana!watu wataogopa kuoa nyumbani wakijua ukoo wote ni walozi!sijui tutaolewa?eeh MUNGU tusaidie!for sure inauma sana tena sana

na Hollo, USA, - 15.06.08 @ 09:27 | #16594

Jamani huyu Hollo ndiye huyu humu JF? Maana hilo jina linatoka huko huko kwao mzee wa VIJISENTI na hata mjadala unaelekea huko huko KUMTETEA mtu wa "KUKAYA" naona alikua akifanya "MAHOLELO" na akina "HOLLO" wanajua
 
Mtanzania, inawezekana sisi na wenye magazeti ndio wajinga kwa kuacha kujadili uwezekano wa kuwapo kemikali hatari tunasisitiza ni uchawi kama vile tumethibitisha ni uchawi ama tunaendeleza mkakati wa hao jamaa wa kutulazimisha tuache kujadili jambo zito kama ambavyo Amina Chifupa, alielezwa kwamba ni uchawi na watu wakahangaika na uchawi hadi walipozinduka na kumpeleka Lugalo, hali ilikua imebadilika na kuwa haiwezekani kabisa. NASISITIZA Mwakyembe/Spika wanalifahamu hilo na hawaliangalii kwa upande wa uchawi wanaliangalia kisayansi zaidi, hata kama SPika naye anakua makini kujifanya anazungumzia uchawi lakini linaangaliwa kwa makini zaidi. Kawaida mtu anaweza kutumia mbinu hyata akaweka kemikali katika kibuyu (japo hakuweka) ili akili zenu zione ni uchawi na kwa kuwa ni WASOMI mutadharau na kuacha ifanye kazi vyema. INAWEZEKANA NI HUO UJINGA WA KISHIRIKINA LAKINI TUSIUPE UZITO TUSISITIZE UCHUNGUZI WA KISAYANSI ZAIDI

Mkuu Halisi,

Nakubaliana na wewe kwamba jambo lililotokea bungeni lazima lichunguzwe ipasavyo. Nilishangaa kusoma kwamba jambo lilitokea Jumanne na bado wabunge wakaruhusiwa Jumatano kurudi kwenye hilo jengo.

Spika alifanya la maana kutoa taarifa polisi, ni wajibu wa polisi kuchunguza kwanza kabla ya kusema ni uchawi au kemikali.

Tukiacha hilo, suala la Dr. Mwakyembe kwa taarifa ambazo mimi ninazo kutoka kwa hao waliomtibu Muhimbili ni kwamba alikuwa na stroke ndogo. Suala la sumu halipo. Kuhusu Amina Chifupa, nafikiri ni upumbavu (ndio natumia neno upumbavu) wa familia yake. Nashindwa kuamini kwamba kanali wa jeshi anshindwa kuelewa umuhimu wa hospitali. Upumbavu wake umesababisha kumpoteza mwanawe.

Watanzania tunarudi nyuma badala ya kwenda mbele shauri ya imani za kijinga ambazo hazitusaidii. Matokeo yake kila mtu anakimbilia kwenye uchawi badala ya kufanya uchunguzi wa kina na kutoa taarifa juu ya nini kilifanyika.

Huenda Chenge alijua kabisa kwamba camera zilikuwa on na alifanya makusudi kama yale ya Kinjikitile (risasis kugeuka kuwa maji), alitaka wabaya wake wajue yeye zaidi ili watishike wakidhani kamwaga uchawi kumbe ni vijiti alivyookota nje ya bunge. Ukisoma saikoloji ya mwanadamu unaweza kumchezea unavyotaka.

Mimi kule kwetu vijana wakaniambia yule mzee mchawi anasambaza funza, nikawaambia wakamwambie huyo mzee akisababisha mimi nikamatwe na funza nitamlipa 10,000. Kule vijijini hizo ni pesa nyingi. Baadaye wakasema huyu brother ni mzima kajikinga ipasavyo. Ukiangalia watu wanaosema wameletewa funza, nyumba zao chafu, vumbi kibao nk.

Sisi Watanzania wachawi wetu ni sisi wenyewe.
 
Imetolewa mara ya mwisho: 15.06.2008 1320 EAT

•
Wabunge 'kususa' kikao cha bajeti kesho, Wahofia yaliyomsibu Dkt. Mwakyembe

sogeza Habari Zinazoshabihiana
• Demokrasia ndani ya Bunge kujadiliwa 13.06.2006 [Soma]
• Lowassa aokoa jahazi matumizi ya dola 11.08.2007 [Soma]
• Mbunge avunjika mguu akishuka kwenye lifti 28.03.2008 [Soma]

Na John Daniel, Dodoma

SIKU chache baada ya kugundulika kwa njama za kuwadhuru Mbunge wa Kyela Dkt. Herrison Mwakyembe, Spika wa Bunge Bw. Samwel Sitta, Naibu wake Bi. Anna Makinda, Mbunge wa Same Bi. Anna Kilango na baadhi ya Wabunge sasa hofu imetanda miongoni mwao na kutaka kufanyika kwa uchuguzi wa kina kwenye viti vyote na maeneo mbalimbali ya ukumbi wa Bunge, kabla ya kuendelea kutumia ukumbi huo kesho.

Sambamba na hilo, Taarifa zilizolifikia Majira Jumapili jana jioni zilisema watuhumiwa wanaodaiwa kutaka kuwadhuru Wabunge wameanza mkakati mahususi kuhakikisha kwamba ushihidi kuhusu uchunguzi wa kuwanasa unakwama kwa lengo la kumzushia Bw. Sitta na vyombo vya habari kwa kusema uwongo.

Taarifa hizo pia zilieleza kwamba tayari maofisa wa usalama na wataalamu wa kuchunguza aina mbalimbali za sumu waliwasili mjini hapa na kufanmya ukaguzi wa kutosha katika ukumbi huo usiku wa kuamkia jana ili kuhakikisha kwamba shughuli za Bunge zinaendelea kesho kama kawaida.

Wakizungumza na Majira Jumapili kwa nyakati tofauti mjini hapa jana, Wabunge hao walielezea kutokuwa na imani na usalama wa ukumbi huo na kudai kwamba huenda mtuhumiwa aliyeweka 'uganga' huo alichanganya na sumu maalum ya kuangamiza watu taratibu.

"Mimi binafsi nilikwenda kukaa karibu na Mhe. Mwakyembe siku alipopata matatizo ya kiafya na nilipotoka hapo niliharisha usiku kucha," alisema Mbunge mmoja wa CCM ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

"Sikulala ingawa sasa najisikia vizuri lakini sina hakika kama niko kawaida, nina shaka na ule ukumbi na hata kama nitaenda bungeni, nitabadilisha kiti," alisema Mbunge huyo.

Mbunge mwingine ambaye pia hakutaka kutajwa jina gazetini alisema atamuomba Spika kusitisha kwa muda vikao Bunge Jumatatu kama wataalamu wa sumu hawatafanya uchunguzi wa kina kwenye viti.

Habari kutoka katika vyanzo vyetu zilieleza kwamba watuhumiwa hao wameanza mkakati wa kupoteza ushidi kwa kushirikiana na baadhi wachunguzi wa suala hilo.

"Mmoja wa Ofisa ambaye anatoka katika chombo nyeti ameanza kutaka kumsaidia mtuhumiwa yule kwa kutuambia kwamba hakuna kitu kama hicho, sasa sisi tunajiuliza yeye amepewa jukumu la kuchunguza suala hili sasa inakuaje anatangaza kwamba si kweli wakati uchunguzi haujakamilika?,"alihoji mmoja wa Wabunge.

Akizungumza na Majira kwa nijia ya simu Kaimu Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilila alisema hana taarifa hizo na kwamba anachojua ni kwamba taratibu zote za Bunge zitaendelea kama kawaida.

Alipouliozwa kuhusu taarifa za ukumbi wa Bunge kufanyiwa uchunguzi wa kina juzi usiku na wataalam wa kuchunguza sumu waliokuwa na vifaa vya aina mbalimbali alisema hilo ni suala la kiusalama na si la umma hivyo hawezi kulizungumza.

"Nani amekwambia habari hizo, huenda yeye anayajua zaidi, hilo ni suala la kiusalama si Public, siwezi kulizungumza,"alisema Dkt. Kashilila.

Hata hivyo habari zaidi zilieleza kwamba ukaguzi huo wa kitaalaamu umefanywa hadi kwenye mavazi ya Spika na Naibu wake ili kuhakikisha kwamba havina madhara yoyote.

Habari hizo zilieleza kwamba kutokana na hali hiyo kutakwepo na mabadiliko makubwa ya ukaguzi na udhibiti wa usalama Bungeni kuhakikisha kwamba vitendo vyovyote vinavyoweza kuleta hofu ndani ya ukumbi huo havitokei tena.

Source: Majira Jumapili 15 June 2008
 
Hasa hasa mistari hii
"Mimi binafsi nilikwenda kukaa karibu na Mhe. Mwakyembe siku alipopata matatizo ya kiafya na nilipotoka hapo niliharisha usiku kucha," alisema Mbunge mmoja wa CCM ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

"Sikulala ingawa sasa najisikia vizuri lakini sina hakika kama niko kawaida, nina shaka na ule ukumbi na hata kama nitaenda bungeni, nitabadilisha kiti," alisema Mbunge huyo.
 
Wakizungumza na Majira Jumapili kwa nyakati tofauti mjini hapa jana, Wabunge hao walielezea kutokuwa na imani na usalama wa ukumbi huo na kudai kwamba huenda mtuhumiwa aliyeweka 'uganga' huo alichanganya na sumu maalum ya kuangamiza watu taratibu.

"Mimi binafsi nilikwenda kukaa karibu na Mhe. Mwakyembe siku alipopata matatizo ya kiafya na nilipotoka hapo niliharisha usiku kucha," alisema Mbunge mmoja wa CCM ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

"Sikulala ingawa sasa najisikia vizuri lakini sina hakika kama niko kawaida, nina shaka na ule ukumbi na hata kama nitaenda bungeni, nitabadilisha kiti," alisema Mbunge huyo.

Hiyo ndio nilikuwa naongelea hofu inayofuata ni kubwa kuliko athari za sumu au uchawi
ambao ulimwagwa.

Huyo aliyeharisha huenda ni ubongo wake ndio ulikuwa unamtuma kuharisha shauri ya hofu. Kwi kwi kwi!!!

Hao ndio wabunge wa jamhuri ya muungano ya Tanzania, kweli kazi ipo! Sasa kama aliharisha alienda hospitali? Au na yeye alimpigia simu mwenyekiti wa kamati yake ya ufundi?
 
Huyu mbunge na mfanyakazi wa bunge waliokuwa wakitandaza "Tambiko" wafunguliwe mashitaka ya uhaini kwa kutaka kuvuruga shughuli za utendaji wa Serikali.
 
SIKU chache baada ya kugundulika kwa njama za kuwadhuru Mbunge wa Kyela Dkt. Herrison Mwakyembe, Spika wa Bunge Bw. Samwel Sitta, Naibu wake Bi. Anna Makinda, Mbunge wa Same Bi. Anna Kilango na baadhi ya Wabunge sasa hofu imetanda miongoni mwao na kutaka kufanyika kwa uchuguzi wa kina kwenye viti vyote na maeneo mbalimbali ya ukumbi wa Bunge, kabla ya kuendelea kutumia ukumbi huo kesho.

Hakuna haja ya kuwa na wasiwasi, si mama Lwakatere yupo Bungeni Jamani... atakemea mapepo na Mkutano wa Bunge utaendelea bila wasiwasi...

Alafu ile sala ya kuliombea Bunge wakisoma kutoka moyoni inatosha... tatizo wanasoma kama wanasoma ngonjera vile...
 
Hasa hasa mistari hii
"Mimi binafsi nilikwenda kukaa karibu na Mhe. Mwakyembe siku alipopata matatizo ya kiafya na nilipotoka hapo niliharisha usiku kucha," alisema Mbunge mmoja wa CCM ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

"Sikulala ingawa sasa najisikia vizuri lakini sina hakika kama niko kawaida, nina shaka na ule ukumbi na hata kama nitaenda bungeni, nitabadilisha kiti," alisema Mbunge huyo.

Ooh my dog! Chenge is so cumbersome fisadi, this is serious. i call for the strict measures against him for the sake of our MPs safety.
 
Tukiacha hilo, suala la Dr. Mwakyembe kwa taarifa ambazo mimi ninazo kutoka kwa hao waliomtibu Muhimbili ni kwamba alikuwa na stroke ndogo. Suala la sumu halipo. Kuhusu Amina Chifupa, nafikiri ni upumbavu (ndio natumia neno upumbavu) wa familia yake. Nashindwa kuamini kwamba kanali wa jeshi anshindwa kuelewa umuhimu wa hospitali. Upumbavu wake umesababisha kumpoteza mwanawe.

Nashukuru sana na nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja. Mwakyembe kwa kuwa alikua pekee aliyekua na taarifa za undani kuhusu tukio la ndani ya Bunge ndio maana akapata hofu kubwa na kupatwa na huo mshituko. Nilipoongea naye alikua akihofia kitu kingine kabisa na si uchawi na ndio maana alienda Muhimbili.
 
Huyu mbunge na mfanyakazi wa bunge waliokuwa wakitandaza "Tambiko" wafunguliwe mashitaka ya uhaini kwa kutaka kuvuruga shughuli za utendaji wa Serikali.

Mkuu Kishoka,

Inategemeana na sheria zetu zinasema nini. Kama mtu mwenyewe alikuwa mwanasheria mkuu, huenda alisoma sheria kwanza zinasemaje kabla ya kufanya hicho anachodaiwa kufanya.

Nakubaliana na wewe kama kuna ushahidi inatakiwa apewe adhabu kali sana kama onyo kwa watu wengine wenye mawazo kama yake.

Watu kama hao inatakiwa hata vyama vyao viwafukuze uanachama.

Nawasifu CUF juu ya jinsi walivyochukua hatua za haraka kwa wale wabunge waliokuwa
wanawapa diplomatic passports hawara zao Wasomali.

Mambo kama haya inatakiwa hatua kali kuchukuliwa na mapema ipasavyo, hakuna kumwonea huruma mtu. Wajinga wachache wanalibabaisha taifa zima, utafikiri wote ni wendawazimu.
 
Nashukuru sana na nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja. Mwakyembe kwa kuwa alikua pekee aliyekua na taarifa za undani kuhusu tukio la ndani ya Bunge ndio maana akapata hofu kubwa na kupatwa na huo mshituko. Nilipoongea naye alikua akihofia kitu kingine kabisa na si uchawi na ndio maana alienda Muhimbili.

Mkuu Halisi,

Umetoa taarifa moja muhimu sana hapo juu. una maana Dr. Mwakyembe alikuwa anajua sakata la Chenge kabla ya kuanguka? Ilikuwaje yeye akapewa taarifa wakati wabunge wengine hawakuwa na taarifa?

Nafikiri hao waliotoa taarifa, kitu cha kwanza kingelikuwa kuhakikisha wahusika wanapimwa ili kuangaliwa hakuna madhara yoyote.

Kama Dr. Mwakyembe alikuwa na taarifa basi sishangai kwamba alipata stroke. Ila hapo atakuwa ameniangusha maana hiyo ni dalili ya woga, ukiwa mpiganaji kama yeye hutakiwi kuwa mwoga. Mwisho wa mpiganaji yeyote ni kifo kwahiyo hutakiwi kuogopa kifo hivyo.
 
Nakubaliana na wewe kama kuna ushahidi inatakiwa apewe adhabu kali sana kama onyo kwa watu wengine wenye mawazo kama yake.

Watu kama hao inatakiwa hata vyama vyao viwafukuze uanachama.

Nawasifu CUF juu ya jinsi walivyochukua hatua za haraka kwa wale wabunge waliokuwa
wanawapa diplomatic passports hawara zao Wasomali.

Mambo kama haya inatakiwa hatua kali kuchukuliwa na mapema ipasavyo, hakuna kumwonea huruma mtu. Wajinga wachache wanalibabaisha taifa zima, utafikiri wote ni wendawazimu.

Mtanzania,

Kama kweli sisi wengine hatuamini hizo imani za kichawi... sidhani kama tuna haja kweli ya kwenda mahakamani/polisi etc...

Dawa ya hili jambo kwa maoni yangu ilikuwa rahisi sana!!! ni kulipuuza ili nasisi wengine (wananchi, wabunge na serikali) tusionekane ni wapagani kama huyo muhusika....

Lakini hili lilitakiwa kufanyika mara moja... kuchukua content/footage za CCTV cameras za Bunge... na kuwapa vituo vya runinga/television nchini... vitangaze kama ilivyo pia kusema lolote...

Wao waseme tu haya ndio yaliyojiri Bungeni... simple....

Hatuna haja hata ya kumpa adhabu huyu mtuhumiwa,,, hata hatuna haja hata ya kumtaja jina!!! wananchi wenyewe waone... na wananchi wenyewe waamue what to be done...

Simple... we don't need to complicate vitu vya kijinga kiasi hiki... and spend a lot of resources ati kuchunguza,,,, kwa usalama wa taifa una uwezo wa kuchunguza uchawi/sangoma?
 
Back
Top Bottom