Kutoka Dodoma!


UFF! Ndugu yangu wee!! Watu tunao-suggest zichukuliwe hatua sio kama tunahofia uchawi..... we are concerning with the motive behind the whole scenerio, and what will be the next move from this fisadi!!!! Kumbuka akumilikae mchana usiku atakuchome. Kumbuka nia ya huyu fisadi ni kuangamiza! Akiachiwa kesho atachukua ma-henchmen/hitmen wamtekelezee anachotaka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 

Kwa kuongezea...iwe sumu or not..iwe juju or not...the fact remains kuwa whatever the substance,.. he had ulterior motive... hata kama ni kuinstil fear tu.... bado ni sooo!!
 

asante mkuu kwa dataz hizi.

hilo kundi lilikuwa hatari zaidi wakati halijajitokeza wazi kiasi hiki lakini sasa nadhani kwa sasa wanajulikana na ugumu wa kufuatilia nyendo na mikakati yao umepungua.

jambo muhimu la kuzingatia ni kwamba mpambano huu ni mgumu na unahitaji umakini wa hali ya juu yaani ni ile "one mistake one goal" kwa hiyo hakuna kulala.

mola ibariki tanzania
 

kazi kweli kweli.....
 


Asante kwa data hizi.Nimejiuliza why Rostam anaongea ndani ya vikao vya CCM lakini Bungeni ama hayupo ama anakaa kimya .Kejeli ya JK inaweza ikawa na maana nyingine positive kwao sisi tukadhani ni kejeli lazima kusoma vyema alama za nyakati .

Nime futa safari yangu mbali na sasa natudi Tanzania baada ya kusoma habari hii naona kama Taifa liko njia panda .
 
je inawezekana mambo ya kuambiwa kideo kilichochukuliwa
kiko hafifu na wahusika hawaonekani vyema ni sehemu ya
mpambano mkubwa zaidi? labda ndio maana mzee six anasita
kutaja jina kwa kuuelewa huo mpambano yaani ni kutaka
kumuingiza mkenge mzee six akurupuke na kutaja jina la
vijisenti kisha kideo kionyeshe ni mtu mwingine na hapo lile
ajenda la kumng'oa mzee six linatimia kiulaini kabisa.

ni mawazo tuu.
 

Mkuu FMES,

Asante sana kwa data, ila mimi siwaamini CCM, watajifanya wanagombana lakini lao moja tu. Dawa ya kukomesha ufisadi Tanzania ni kuwang'oa CCM kwanza, wakae nje, waone wenzao wanavyofanya changes za kweli kweli.

Hawa CCM baadhi yao nawajua kwa karibu mno na hata hao tunaoweza kuwaita kwamba ni watetezi wa wananchi, ukiwakaribia kwa karibu unagundua wameoza tu, labda wanasema kwasababu hawakukatiwa kiti.

Mimi naombea Tanzania tufanye mabadiliko ya nguvu ya kuing'oa CCM madarakani ili kuachana na huu ujinga wote.

Wengine tunaombea waruhusu wagombea huru maana kuna kundi kubwa la watu ambalo halioni nafasi ndani ya CCM na pia hata huko upinzani.
 
Lunyungu,
Nime futa safari yangu mbali na sasa natudi Tanzania baada ya kusoma habari hii naona kama Taifa liko njia panda

Maneno haya kweli au ndio ktk kamba!..
 
this can olny happen in TZ, mtu mjinga mjinga anasumbua taifa anachekewa, mtu anasema amesahau kitu halafu anaenda mpaka pale mbele kwenye kiti cha spika, hapo ndo alipoacha vitu vyake.... hii tayari haijakaa sana na ni sbb tosha ya kubanwa lkn analindwa lindwa tuu.. hii nchi si muda mrefu italipuka vibaya sana kama hatua za kuliokoa taifa hazita chukuliwa

FMES mwaga vitu kijana
 
..............mimi Kejeli Ya Kikwete Kwa Rostam Naichukulia Kama Kichekesho......in Reality Uchafu Wote Aliofanya Rostam Epa ..kikwete Alikuwa Na Taarifa Nao...sasa Tatizo Kubwa Linakuja Wanapogeukana Leo....jk Knows Where The Money Came From....

..kuhusu Kuwa Uchumi Na Reserve Wakati Wa Mkapa Ulikuwa Juu..hilo Halina Ubishi....ukiacha Hili Suala La Ufisadi..mkapa Perfomance Was Brilliant!!!

..hadi Dakika Hii Zaidi Ya Mkingamo Isiyokuwa Na Uamuzi ..jk Hajafanya Lolote La Maendeleo La Kukumbukwa..hilo Alijue Na Ajitahidi!!!....pia Udhibiti Wa Kikwete Kwa Dola Ni Mdogo Kwa Viwango Vya Kawaida!!!
 
mkuu mkjj ulipomuhoji muheshimiwa aliposingiziwa kunywa sumu alijibu kuwa anatoka ahera anaelekea duniani


huenda kweli alitoka kuzimu huko alipewa unabii wa ushirikina na sasa yuko bungeni kutangaza unabii wake
 

Asante Mkuu wa dataz, endelea. lakini ebu tupashe angalau kiduchu, Sendeka alilonga nini kiasi cha kuamsha mjadala mzito?
 

Sijui lakini unaweza kutumia jina lolote ilimradi unaamini litaweza kuleta ushindi. Mimi nimeamua kutumia jina kubwa kama hilo sijui wewe utatumia lipi mkuu. Cha muhimu ni ushindi mkuu.
 
hivi jamani bado tu amjakubali kuwa serika yetu imekwenda likizo.yaani imeshindwa hata hesabu ndogo ya mbili kujumlisha mbil ni nne.
 
..kuhusu Kuwa Uchumi Na Reserve Wakati Wa Mkapa Ulikuwa Juu..hilo Halina Ubishi....ukiacha Hili Suala La Ufisadi..mkapa Perfomance Was Brilliant!!!

Mmmmmmhhhhh!!!! Labda sielewi maana ya neno brilliant! kule kwetu kijijini sikuona maendeleo yoyote ya wananchi tofauti na mwaka 1995, kwa tathmini yangu ya haraka haraka, watu wanazidi kuwa maskini kuliko walivyokuwa 1995.

Mkapa ameuza mashirika yote hayo ya umma, ni obvious alikuwa na pesa nyingi za kutumia kuliko viongozi waliotangulia. Pia kwa kuuza mashirika ambalo lilikuwa jambo jema hata kama
ubinafishaji ulikuwa na kasoro kibao, tayari alikuwa amepunguza matumizi ya serikali kwenye kusaidia hayo mashirika ambayo yalikuwa yanaingiza hasara.

Sawa alijitahidi kwenye uchumi lakini sio kwa kiwango hicho cha kusema performance yake ilikuwa brilliant.
 
Asante sana kwa data, ila mimi siwaamini CCM, watajifanya wanagombana lakini lao moja tu. Dawa ya kukomesha ufisadi Tanzania ni kuwang'oa CCM kwanza, wakae nje, waone wenzao wanavyofanya changes za kweli kweli.

Mkuu Mtanzania,

1. Ninakusikia sana, katika huu mkutano ninaongea na wabunge wote wa pande mbili kwa nyakati tofauti, never before nhimewahi kuwa moved emotional kama safari hii, I mean what is this Mwakyembe's thing? Mkuu si unakumbuka juzi tu nilisema kuwa wa-Tanzania huwa hatujifunzi kabisa, ya Balali hayajaisha here we are about to commit another big mistake,

2. I do not care what, Chenge to me is a thug na wenziwe wote, ni wahuni tena ni vibaka wasiokuwa na class kabisa kama bin-adam wengine wote, mkuu kwenye hili sakata la Richomonduli kina Mwakyembe walishawishiwa kupewa hela nyingi sana, lakini wakagoma kabisaa kwa hiyo na ushahidi upo wazi, kwa hiyo angalia tena hiyo statement yako, kuna wabunge wengi waliopewa millions of shilllngs ili waikatae ripoti ya Mwakyembe pale bungeni ushahidi upo mkuu maana haya yalikuwa aykifanya wazi wazi!

3. Taifa letu linakuwaje na viongozi wapuuzi kama Chenge? Tunakuwaje na viongozi wajinga wajinga kama Lowassa? Jana usiku for about six hours nilikuwa na mkutano wa siri na mmoja wa watuhumiwa wa mkataba Richimonduli, I mean kuna wakati machozi yalikuwa yananitoka jinsi alivyokuwa akinielezea aliyoyaona kwa macho yake mwenyewe na sio kuhadithiwa na mtu au kusoma ripoti yoyote, huyu ni mmoja wa walioona the whole thing, I mean it a shame huyu alenda Europe kukagua hizo machine, alienda Malasyia na Kolimba, lakini walipotaka kwenda Houston kukagua ofisi na machine za Richimond kama sheria za serikali na jamhuri yetu inavyosema, na kutaka Msabaha kwa makusudi mazima ya ufisadi akawakataza kwenda huko huku akiwashambulia kuwa wanapenda sana safari ili wale hela za wananchi huku hakuna cha maana wanachokifanya, akitamba kwamba yeye anaijua sana Richmond ni kampuni safi hawahitaji kwenda huko, sasa najiuliza kwa nini hakuwazuia kwenda ile miji mingine? Na kwa nini aliwazuia kwenda Houston ambako ndio makao makuu ya Richmond? Na ilikuwaje Hosea akawasafisha kundi zima la Richimonduli!

Wakuu tunahitaji kuwa macho sana na taifa letu, na hasa kujua nani yuko na sisi wananchi na nani yuko uapnde wa pili, katika kuongea tu na hawa viongozi binafsi ninaweza kutenganisha nani yupo na sisi na nani hayupo pia, tufike mahali tumuombe Mungu atusaidei tulipite hili janga la taifa letu kuhujumiwa na hawa viongozi wachache ambao mimi ninasema kuwa ni sawa na wanyama, yes I said it this guys are pure animals, unfit licha tu ya kutuongoza bali hata kuruhusiwa kusihi na binadamu wengine,

dawa ni kuwakamata na kuwalazimisha wao na familia zao walipie risasi za kuwatwanga mbele ya public, tena ikiwezekana pale Sanamu Monument, yes piga risasi tu, kwa sababu look what they are doing to us now? tumeacha kuongelea a strong an big agenda za taifa kama EPA na Kiwira, lakini sasa tunaongelea uchawi na ujinga wa a Harvad man Chenge, yaani the Harvads, kina Obama wanakaribia kuwa marais wa kwanza weusi huko USA, hili lijinga ndoo kwanza linaenda ku-promote uchawi nationally!

Halafu kumbuka kuwa akiwa Mwanasheria mkuu ameshiriki kwenye kuwafunga wananchi wangapi wasiokuwa na makosa kisheria, ingekuwa nchi za majuu sasa hivi kungekuwa na kesi kibao na lawsuits against serikali yetu kwa sababu ya Chenge, kwamba hana intelligent judgement au uwezo wa kutosha kufikiri kama binadam kamili, kwa hiyo wote alioshiriki kuwafunga kisheria wanahitaki kuachiwa, na mikataba yote iliyosainiwa china yake akiwa Mwanasheria mkuu itenguliwe mara moja!

Binafsi, sioni siasa ya chama hapa, ninachooona ni taifa kwanza hapa kuna wabunge am,bao wamepania na wako intact, kuna CCM na wa upinzani pia wanashirikiana ingawa kwa siri, kuweka agenda za wananchi kwa manufaa ya taifa, na ninawaombea Mungu awabariki na wafanikiwe!
 
lakini ebu tupashe angalau kiduchu, Sendeka alilonga nini kiasi cha kuamsha mjadala mzito?

According to the dataz ni kwamba ilifikia mahali wajumbe walitaka kushikana mashati, by kesho Mungu akijalia nitakuwa na exactly nini hasa Mbunge Sendeka alichosema.

Lakini pia aligusia kitendo cha mtoto wa Lowassa, ambaye sio kiongozi wa taifa letu in any capacity, alivyohusishwa na mkataba wa Richimonduli na kufikia kufaidika na hela zetu walipa kodi ambazo sasa amefungua kampuni moja ya Card za Simu, ambayo inampatia hela nyingi sana as a profit, biashara ambayo wananchi wengi walijaribu sana kuiomba kibali serikali wakakataliwa lakini huyu kijana akapewa bila matatizo, biashara ambayo hata mtoto wa Mengi ambaye ni marehemu sasa aliwahi kuiomba serikali akakataliwa.

Kama nilivyoahidi kuwa tunaendelea ku-monitor yanayojiri Dodoma, kwa karibu sana na tutaendelea tu kuhabarishana hapa kwenye uwanja mtukufu wa JF!
 
Mtanzania,
hapo ndipo napokoma na Wadanganyika... ati brilliant!... wakati taifa limedidimia zaidi ktk miundombinu wakati wa Mkapa. Wewe umeona wapi mji kama Dar pekee ambao hesabu ya wakazi wake walizidi kwa asilimi 100 lakini nguvu ya umeme ni ile ile nguvu ya maji ni ileiule toka 1978, elimu chini, kilimo chini, Afya na meningine kibao. Haya hizo fedha walizokusanya ni kutoka kwa walipa kodi wananchi wasiokuwa na kitu wakiibiwa ktk kodi za asilimia 40 hadi 60, mwenkeshaji toka nje zero! Fedha tunazojivunia zilikuwa mikopo ambayo leo tunakuja fahamu zilitumika vibaya,,, huu uchumi wanaozungumzia ni upi? haswa kwa mzalendo mlalahoi kama mimi.
jamani jamani tuwe wakweli na kutomwenea mtu aibu kwani sidhani kama kuna mtu hapa anaweza kutoa maelezo ya maendeleo hayo zaidi ya Takwimu, takwimu ambazo leo kwa Kiktwete wanasema zimetengenezwa!.. iweje Kikwete atengeneze takwimu lakini sio wakati wa Mkapa..besides kwa nini serikali ilikataa kabisa uchunguzi wa BoT (EPA) usiende nyuma ya mwaka 2005 ikiwa kweli tulitaka kuufahamu ukweli.

Hata hivyo hoja hii haihusiani na mada hii lakini wakuu tusijaribu kabisa kuunda timu hapa.. Huyo RA alikuwa bwana fedha wa chama CCM chini ya Mkapa unaweza kuelewa kilitembea kitu gani ikiwa wahalifu wote ni wajukuu wa Mkapa. Hayakuanza jana haya jamani!
 




...Told you so!,

SPIN DOCTORS wapo kazini, nyie mmekazana na dhana za uchawi!

...mbele mwangaza nyuma kivuli, ni hiari yako kufikiri hicho kivuli ni cha umbile lako au ni jini-mapembe linakufuata!

...By the time mnakuja gundua ni spinning tu ya habari, tayari taifa na kikao cha bunge kishapotezwa mwelekeo, ...tuhuma za Richmond, EPA, Kiwira, kujilimbikizia vijisenti, zitakuwa hazina nguvu tena, yale yale kama miaka yote...

Oh my God, Only in Tanzania!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…