Kuna mambo hayaendi sawa bina sawia, hasa baada ya kusoma posts za watu ambao nina amini kwamba wanatoa maelezo ya kina kuhusu hili sakata.
Kwanza nimeshangazwa na jinsi Bunge kama Taasisi jinsi ambavyo linashughulikia hili swala. Kuna mambo mengi sana ya kujiuliza kuhusiana na watendaji wakuu wa Bunge pamoja na wasaidizi wao na watunza usalama wa hilo jengo.
Iwapo camera za usalama za jengo lote zilikuwa zimezimwa, hiyo picha ya Mbunge na Katibu wa Bunge inayowaonyesha wakipita kwenye viti vya waheshimiwa wakimwaga vitu ilitoka kwenye camera ya chombo gani cha habari?
Kwanini kuna contradictions kwenye maelezo yao? Kwamba camera zilikuwa off, mara camera zilikuwa ON na Chenge haonekani? Hapa ninanusa harufu mbaya sana ya ufisadi uliopea. Kuna uwezekano mkubwa sana kwamba Bunge kama Taasisi ilitumiwa na mafisadi ili kufanya hayo waliyoyafanya kwa faida ya mafisadi lakini wameumbuka baada ya picha kutoka nje camera za usalama kumuonyesha Mbunge na Katibu wa Bunge. Kwa hiyo kuna vigogo wa Bunge walijua nini kinafanyika na walitoa baraka zote, may be Sitta na Mama Makinda na some othe Big Shots hawakujua, lakini kuna watu very senior walikuwa involved. Hili swala linahitaji kuwahoji vigogo wote wa Bunge kuanzia Katibu wa Bunge mpaka wanaolinda.
Kuna uzembe fulani katika kushughulikia hili swala. Kwa kawaida mtu akienda kutoa taarifa za mauaji, wizi, na mengineyo huwa anakuwa makini sana kwamba mtu mwingine asiguse chochote ili ushahidi usije ukapotea ama asije akaharibu uchunguzi utakaofanyika. Mfano kuchukua kisu, kushika kitasa cha mlango ama kushika komeo la mlango au zana yoyote iliyotumika kufanya huo uhalifu. Ni polisi ndiyo wanatakiwa kuja kugusa hivyo vitu tena kwa uangalifu na umakini mkubwa ili wasije wakaharibu uchunguzi wao. Swali kwenye hii sakata ni kwamba, je, baada ya kupewa taarifa kwamba kuna madudu yalifanyika kwenye ukumbi kabla ya kikao, walizuia watu wengine kuingia ndani ili kutoharibu uchunguzi? Ni nani alipeleka taarifa za Sitta ama Uongozi wa Bunge kuhusu hilo tukio na je alipeleka kwa wakati muafaka? Na ni hatua zipi zilichukuliwa ili kuzuia kupoteza ushahidi?
Kudai kwamba siku ya pili kulikuwa unga unga kwenye kiti cha Mh. Mwakyembe ina maana kwamba wafagizi hakufuta kiti chake? Ama ina maana usafi haukufanywa? Kama kulikuwa na tukio kama hilo, kwanini Spika hakuahirisha kwa muda kikao hicho ili kupisha uchunguzi wa polisi ili kama kuna sample yoyote ya kuchukua wachukue na kwenda kuifanyia uchunguzi? Ina maana Spika hawezi kuahirisha kikao for a day ili kupisha uchunguzi wa kina ufanyike?
Jengo lile limejaa serikali na wawakilishi wa wananchi kwa hiyo nilitarajia kwamba Usalama wa Taifa hawalali na hawawezi kuwaamini wana usalama wa hapo na inawezekana wafanyakazi wengi wa Bunge kuanzia walinzi mpaka hao wasaidizi ndani ya ukumbi na hata wafagizi ni waajiriwa wa usalama wa Taifa maana humo ndani kuna PM ambaye anatakiwa kulindwa kwa ukaribu sana na pia Ukumbi wa Bunge ni jengo muhimu sana ambalo UWT wanatakiwa kuwa makini nalo masaa 24. Hili linanipeleka kwenye signal nyingine kwamba UWT imetekwa na mafisadi na inafanya kazi zake kwa maslahi ya mafisadi na ndiyo maana kuna mambo mengi sana ambayo hayaendi sawa kwenye uchunguzi wa hili sakata na sijui kama tutapta kitu cha maana kwa kuwa UWT wanaweza kuwa wanahusika na walifanya kwa mahesabu makubwa na kuhakikisha kwamba ushahidi unakuwa mgumu kupatikana.
Kwa mtazamo wangu, ni wakati muafaka kwa JK kubadilisha na kuisafisha UWT vinginevyo nchi hii itaendelea kuwa mikononi mwa mafisadi na iko siku watakuja kufanya mambo makubwa sana. Tukio la hapo Bungeni ni la kiusalama zaidi kuliko kisiasa na hivyo RO alitakiwa awe responsible kwa tukio hilo, maana ni aibu na kama hayo madudu yalifanyika na yeye hakujua basi kuna walakini mkubwa kwamba Idara imepoteza mwelekeo na iko siku tunaweza kusikia Waziri Mkuu ama Jengo zima wamekufa kwa kuvuta hewa ya sumu humo ndani na bado watakaokuwa responsible ni hao hao UWT. Hawa UWT ni wepesi kupenyeza watu wao kwenye vyama vya siasa ili kuvimaliza lakini nitashangaa kama RO atakuwa hana wafagizi, wahudumu, makatibu wa Bunge na wengineo ambao wanahusika moja kwa moja na shughuli za Bunge kila siku kwenye lile jengo. Kama ikiwa hivyo basi ina maana kwamba RO kashindwa kazi au sasa anafanya kazi kisiasa zaidi na siyo usalama wa taifa tena. Kweli nchi imetekwa!