Kutoka Dodoma!

Kutoka Dodoma!

According to the dataz ni kwamba ilifikia mahali wajumbe walitaka kushikana mashati, by kesho Mungu akijalia nitakuwa na exactly nini hasa Mbunge Sendeka alichosema.

Lakini pia aligusia kitendo cha mtoto wa Lowassa, ambaye sio kiongozi wa taifa letu in any capacity, alivyohusishwa na mkataba wa Richimonduli na kufikia kufaidika na hela zetu walipa kodi ambazo sasa amefungua kampuni moja ya Card za Simu, ambayo inampatia hela nyingi sana as a profit, biashara ambayo wananchi wengi walijaribu sana kuiomba kibali serikali wakakataliwa lakini huyu kijana akapewa bila matatizo, biashara ambayo hata mtoto wa Mengi ambaye ni marehemu sasa aliwahi kuiomba serikali akakataliwa.

Kama nilivyoahidi kuwa tunaendelea ku-monitor yanayojiri Dodoma, kwa karibu sana na tutaendelea tu kuhabarishana hapa kwenye uwanja mtukufu wa JF!

Pole na hongera sana Mkuu ESFM, tupo pamoja, tunakuombea Mungu aendelee kukuweka mbali na mikono ya mafisadi
 
Ahsante FMES! Kweli kazi yako ni kubwa!

Hivi hawa wabunge kama Makamba amewapiga chenga si watumie forum yao BUNGE. Wanajuaje muungwana angewasikiliza! Hivi hawaoni muungwana kazidiwa kabisa na kwake yeye nchi inaenda vizuri tu. Ndio maana jana alienda kupata burudani uwanja wa taifa tokea Dodoma!
 
Mkisoma kwa makini ile makala ya Majira na maelezo aliyoyatoa Halisi tayari njama zilishaanza za kuvuruga ushahidi wa sakata hili. Mara wanasema kamera zilikuwa on 24/7 mara kwamba zilizimwa. Hatima yake watasema hakuna ushahidi unaomhusisha Chenge katika sakata hili na mafisadi watakuwa wametufunga tena bao jingine la kisigino.
 
...By the time mnakuja gundua ni spinning tu ya habari, tayari taifa na kikao cha bunge kishapotezwa mwelekeo, ...tuhuma za Richmond, EPA, Kiwira, kujilimbikizia vijisenti, zitakuwa hazina nguvu tena, yale yale kama miaka yote...

Mkuu Heshima yako,

Si kweli kwamba sisi wananchi wote ni wajinga, hapana tupo wenye akili timamu na huko bungeni kuna viongozi wenye akili timamua sana, ndio maana jana kwenye kikao kizito cha siri cha CCM wakadai agenda nzito ambazo hazihusiani na ujinga ujinga wa Chenge.

Everything is under control, sasa hivi inasubiriowa hotuba ya bajeti ya Waziri Mkuu na hotuba ya bajeti nzima kwa ujumla, sisi ni wabongo ninaomba muwe mnakumbuka hilo mnapotoa comments zenu maana wengine manonekana kutojua hilo kuwa bado Tanzania tunafanya mambo yetu ki-Tanzania sio ki-Ulaya Ulaya, mambo yetu ni taratibu sana na kuogopana huku sisi tukiita eti ni heshima, sasa hivi kuna wabunge ambao wamechoka na ujinga na tunawajua kwa majina na tunawaunga mkono, na tunaktaa kabisa maneno ya kuwakatisha tamaaa,

Unaposema maneno ya spinning sielewi unachosema hasa ni nini? Kwamba eti Chenge hakuenda bungeni kuweka ujinga, au kwamba Mwakyembe sasa hayupo Dar kuangaliwa afaya yake na wataalamu? Sasa mkuu kwa maoni yako sisi wananchi tufanye nini tuisongelee yaliyotokea ambayo hatukuyapanga? Enzi zilizopita haya hayaklutokea je tuli-accomplish nini hasa kwa taifa?

Jamani kuweni waangalifu na hizi comments, kwa sababu wengine hili la Tanzania ni taifa letu na tunalipenda na kuliheshimu na pia kuliombea kwa Mungu ili tufanikiwe kusonga mebele angalau kidogo, na hakuna miujiza ni kazi yetu wote wananchi kujihusisha hakuna wa kutufanyia, popote ulipo na chochote unachoweza kutumia do it kwa faida ya taifa letu, taifa ni letu sio lao tena jaribu sana kutumia huu mtandao kuleta mabadiliko sio siri kuwa ujumbe wetu unafika tunapoulenga sasa mkuu wangu can you imagine Rostam akifungua JF nakuona haya maneno yako ya kutukatisha tamaa sisi wananchi walalahoi!
 
Kifupi sasa hivi Chenge na kundi lake wanaogopwa zaidi na wataendelea kutisha bunge zima kwa Uchawi... nasema hakuna Mbongo hata mmoja anayetaka kuwa kafara hata kama haamini Uchawi...
Kifupi sasa hivi kina Mkapa wanacheka sana na kusema mwenye kuona kosa arushe jiwe la kwanza!...
Nasubiri wabunge wenye nguvu zaidi ktk maswala haya ya sayansi ya kiafrika wale ambao kwa kutumia dini zao au mitunga wamejizatiti vya kutosha kuweza kusimama imara...Sii kazi ndogo!
Binafsi nimeshalikubali hili goli la kisigino!....
 
Jamani off line kidogo!!

1. Chenge alimwagia viti vyote "substance"
2. Cha DR Mwakeyebe being one of them.

Swali:

Is there any conection kati ya what is happening kwa Dr Mwakyembe na Substance za Chenge? Fine kama Ni hivyo Why Dr Mwenyewe while alimwaga kw aviti vyote?

Hope ther is conection!
 
Is there any conection kati ya what is happening kwa Dr Mwakyembe na Substance za Chenge? Fine kama Ni hivyo Why Dr Mwenyewe while alimwaga kw aviti vyote?

Mkuu Azimio,

Heshima mbele bro, binafsi ninaichukulia hii ishu ta its face value kwamba:-

1. Fact:- Kwamba Chenge aliingia ndani ya bunge wakati ambao hakutakiwa kuingia mle ndani, na amekamatwa na camera za ndani ya bunge.

2. Fact:-Alipoingia ndani ya bunge, ameonekana kwenye camera za ndani ya bunge, akinyunyizia something katika viti vya baadhi ya wabunge, kiti cha Spika kikiwa ni kimmoja wapo na kiti cha kiti cha Mbunge Mwakyembe.

3. Fact:- Mbunge Mwakyembe sasa hivi kiafya hali yake sio 100%, kama inavyotakiwa kuwa, lakini hatujui chanzo chake ni nini, tukiwa tunasubiri kusikia chanzo chake officially kutoka kwa wataalamu, sisi wananchi ni haki yetu ku-speculate kuwa chanzo chake ni something kilichonyunyiziwa na Chenge kwenye kiti chake, kwa sababu ni fact kuwa Mbunge Mwakyembe alipokwenda bungeni alikuwa mzima 100%.

Binafsi I am not tooo much in to this uchawi thing na wala siuamini, lakini siwezi kusema kuwa haupo wakati Mungu ninayemuamini anasema kwenye kitabu chake yaani Biblia, kuwa upo tena hata nabii Musa alipokwenda kwa Farao na kuonyesha miujiza aliyopewa na Mungu, as a threat ili Farao awaachie watu wake, Farao naye alileta wachawi wake ambao some-how nao waliweza ku-imitate ile miujiza ya Mungu, tena very close, ingwa mwishoni walishindwa, lakini kulikuwa na some struggle hapa kati ya the all Mighty na the most Powerful God, na bina-adam aliowaumba yeye mwenyewe, sasa leo mimi nitakuwa nani kusema kuwa haupo?
 
FMES: You are a star of this forum; shukrani sana.

Lakini mkuu hawa jamaa zako wa CCM mwisho wa siku watakubaliane yaishe kwa "maslahi ya chama". Hope I am wrong!
 
FMES,

..uko wapi ushahidi kwamba Chenge aliingia bungeni na kunyunyuzia "vitu" kwenye vigoda vya wabunge?

..mnadai kuna tapes sasa wananchi tunaomba kuonyeshwa hizo tapes. the jury is on those who accusing Chenge of wrong doing.

..hivyo "vitu" vilinyunyizwa kwenye kiti cha Mwakyembe na wabunge wepi wengine? kwanini hao wabunge wengine hawatajwi ili tukajua wanaendelea vipi kiafya tangu siku ya tukio?
 
Mkuu Azimio,

Heshima mbele bro, binafsi ninaichukulia hii ishu ta its face value kwamba:-

1. Fact:- Kwamba Chenge aliingia ndani ya bunge wakati ambao hakutakiwa kuingia mle ndani, na amekamatwa na camera za ndani ya bunge.

2. Fact:-Alipoingia ndani ya bunge, ameonekana kwenye camera za ndani ya bunge, akinyunyizia something katika viti vya baadhi ya wabunge, kiti cha Spika kikiwa ni kimmoja wapo na kiti cha kiti cha Mbunge Mwakyembe.

3. Fact:- Mbunge Mwakyembe sasa hivi kiafya hali yake sio 100%, kama inavyotakiwa kuwa, lakini hatujui chanzo chake ni nini, tukiwa tunasubiri kusikia chanzo chake officially kutoka kwa wataalamu, sisi wananchi ni haki yetu ku-speculate kuwa chanzo chake ni something kilichonyunyiziwa na Chenge kwenye kiti chake, kwa sababu ni fact kuwa Mbunge Mwakyembe alipokwenda bungeni alikuwa mzima 100%.

Binafsi I am not tooo much in to this uchawi thing na wala siuamini, lakini siwezi kusema kuwa haupo wakati Mungu ninayemuamini anasema kwenye kitabu chake yaani Biblia, kuwa upo tena hata nabii Musa alipokwenda kwa Farao na kuonyesha miujiza aliyopewa na Mungu, as a threat ili Farao awaachie watu wake, Farao naye alileta wachawi wake ambao some-how nao waliweza ku-imitate ile miujiza ya Mungu, tena very close, ingwa mwishoni walishindwa, lakini kulikuwa na some struggle hapa kati ya the all Mighty na the most Powerful God, na bina-adam aliowaumba yeye mwenyewe, sasa leo mimi nitakuwa nani kusema kuwa haupo?

halafu ndo wanataka tuceasefire?
 
FMES,

..uko wapi ushahidi kwamba Chenge aliingia bungeni na kunyunyuzia "vitu" kwenye vigoda vya wabunge?

..mnadai kuna tapes sasa wananchi tunaomba kuonyeshwa hizo tapes. the jury is on those who accusing Chenge of wrong doing.

..hivyo "vitu" vilinyunyizwa kwenye kiti cha Mwakyembe na wabunge wepi wengine? kwanini hao wabunge wengine hawatajwi ili tukajua wanaendelea vipi kiafya tangu siku ya tukio?

This is what I am talking about. Hata hapa JF tumeanza kuuliza mambo ya ushahidi. Kwa hiyo hata Mr Six ni part of the conspiracy za kumchafulia jina bwana Vijisenti? Can you believe this?
 
Hapa tumefungwa goli lingine, hatuongelei tena budget, wabunge wameacha kujiandaa kwa majadiliano makali ya budget na sasa wanaongelea uchawi.

Hakuna adui mkubwa kama hofu, mtu mwenye woga sio huru wala hawezi kuleta uhuru kwa wengine.

Watanzania inaelekea tunawaogopa sana mafisadi, lakini ni kweli wana hizo nguvu? Uwoga wetu ndio unawapa hizo nguvu.

Ili kupambana na mafisadi lazima tuondoe kabisa woga. Pili, kifo kwa mpiganaji yoyote ni jambo la kawaida. Kama wewe ni mpiganaji na unaogopa kifo, basi umeshashindwa mpambano.

Ondoeni woga kabisa, akina Chenge hawana hizo nguvu mnazowapa. Lowassa mwenyewe angelikuwa na nguvu si angejiokoa asiondolewe kuwa PM?
 
Mkuu Heshima yako,

Si kweli kwamba sisi wananchi wote ni wajinga, hapana tupo wenye akili timamu na huko bungeni kuna viongozi wenye akili timamua sana, ndio maana jana kwenye kikao kizito cha siri cha CCM wakadai agenda nzito ambazo hazihusiani na ujinga ujinga wa Chenge...

...Unaposema maneno ya spinning sielewi unachosema hasa ni nini? Kwamba eti Chenge hakuenda bungeni kuweka ujinga, au kwamba Mwakyembe sasa hayupo Dar kuangaliwa afaya yake na wataalamu?

Heshima yako Mkuu,

nakubaliana nawe kwamba si kila mtu mjinga, ila tatizo linakuja pale hii habari inavyopewa hukumu na wengi kwamba CHENGE alikwenda kuweka uchawi, au sumu.

...Spinning namaanisha, linaonekana kama ALIBI;

1.Kufuatana na afisa wa bunge.

2.Star Tv cctv tu, wakati za Bunge zimezimwa! ...

3.muda aliokuwa anautumia kusimama kwenye viti vya hao waheshimiwa.

hivi kweli mnaamini mtu kama CHENGE ambaye ni msomi wa sheria, jambo hili 'linavyojionyesha' ni pre-planned atafanya uharamia huo na kuacha exhibits all over the place kiasi hicho bure bure tu?

naamini huo ni 'usanii', haswa kwa 'watuhumiwa' kutambua society inaathiriwa vipi na 'perception, visual effects and judgments'.

the rest is History!, mwanahabari ana-leak habari kwa wanahabari kisha inakuwa big news!

Anyway, i might be wrong, nilifundishwa na wazee kuwa wengi wape.
Naamini Tanzania tuna Forensic experts wa kutosha, naamini wali cordon 'crime' scene kwa wakati muafaka (bila kuingiza contamination material zozote), na kuchukua sample zote ziwe ni majimaji, unga etc (kama inavyosemwa, alikuwa 'anamwagia'), na wengine watazipitia hizo 'blurred' footage kuhakikisha 'mtuhumiwa' anawajibika kwa vitendo vyake, hata kama ilikuwa ni tisha toto tu!

Mungu ibariki Tanzania.
 
Makosa yote ni ya mtu mmoja na mmoja only :::: JK

Jk ndo yuko hatarini zaidi sababu anakuwa undermined kila kona na yeye hajua kuwa kundi hilo liko powerful mno sababu linahusisha matajiri wa nchi ambao wako tayari kwa gharama yoyote kulinda utajiri.

Jk anadhani Usalama uko under control, that is a fatal assumption.

Issue ni very simple:: BWM, Lowassa, Manji, Rostam, Jeetu, Karamagi na watu wote waliopewa favor under Mkapa wametangaza vita kwa kuundana pamoja.

Advisor wao ni mtu hatari sana ambaye amebobea kwenye issue ya kusolve matatizo kwa elimination, yaani kama X ni tatizo then U eliminate X and the problem is gone.

Sasa hivi problem ni Sitta, na wabunge machachari kwa hiyo tutasikia mengi na kuona vioja vingi tu na mungu apishilie mbali lakini sitashangaa hata baadhi ya mazishi.

Siku wakiconclude JK ni problem, I guess U can see where the movie will end.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Asante kwa data hizi.Nimejiuliza why Rostam anaongea ndani ya vikao vya CCM lakini Bungeni ama hayupo ama anakaa kimya .Kejeli ya JK inaweza ikawa na maana nyingine positive kwao sisi tukadhani ni kejeli lazima kusoma vyema alama za nyakati .

Nime futa safari yangu mbali na sasa natudi Tanzania baada ya kusoma habari hii naona kama Taifa liko njia panda .


Mtani... una mafix wewe...
 
Makosa yote ni ya mtu mmoja na mmoja only :::: JK

Jk ndo yuko hatarini zaidi sababu anakuwa undermined kila kona na yeye hajua kuwa kundi hilo liko powerful mno sababu linahusisha matajiri wa nchi ambao wako tayari kwa gharama yoyote kulinda utajiri.

Jk anadhani Usalama uko under control, that is a fatal assumption.

Issue ni very simple:: BWM, Lowassa, Manji, Rostam, Jeetu, Karamagi na watu wote waliopewa favor under Mkapa wametangaza vita kwa kuundana pamoja.

Advisor wao ni mtu hatari sana ambaye amebobea kwenye issue ya kusolve matatizo kwa elimination, yaani kama X ni tatizo then U eliminate X and the problem is gone.

Sasa hivi problem ni Sitta, na wabunge machachari kwa hiyo tutasikia mengi na kuona vioja vingi tu na mungu apishilie mbali lakini sitashangaa hata baadhi ya mazishi.

Siku wakiconclude JK ni problem, I guess U can see where the movie will end.

Mungu Ibariki Tanzania

...kaka unajua tatizo hapa ni moja...MTANDAO WAMEKOROFISHANA....hili tatizo tuliliona ..maana unapoongelea urais wa kikwete unaongelea KINGMAKERS wake kama ....ROSTAM AZIZ,EDWARD LOWASSA,NAZIR KARAMAGI,BENNARD MEMBE,ZAKIA MEGHJI et al....

hawa watu walifanya mbinu zote safi na nyingi chafu ikiwemo kutumia fedha za BOT,na kampeni za kuchafua wagombea wenzao...

LEO HII MTANDAO HUU HUU UNAMUELEMEA KIKWETE NA SANA SANA AMEBAKIA NA BENNARD MEMBE TU UPANDE WAKE FROM ORIGINAL MEMBERS WA MTANDAWO.......MEMBE OFFCOURSE KABAKI NA KIKWETE KWA SABABU NAYE LENGO LAKE NI KUONEKANA GOOD BOY ILI AWE RAIS 2015.....KIMSINGI MUHESHIMIWA RAIS KAELEMEWA NA KUNDI LAKE MWENYEWE....NA HALI HII HAIASHIRII USALAMA KWETU KAMA TAIFA!!!!

we have one solution in 2010..nayo ni kurudisha ETHICS...na kikwete kama ataendelea asigombee kama mgombea wa mtandao...avue kabisa hilo joho na arudi kwa wanachama...la kama haitawezekana na HII HALI YA RAIS KUKOSA UDHIBITI WA NCHI NA KUKOSA UMOJA CHAMANI ITAENDELEA....ni bora kamati kuu ya CCM ...IAMUE KWA KAULI MOJA KUMPUMZISHA KIKWETE 2010..NA KULETA MGOMBEA MPYA....BILA SHAKA...MIAKA MITANO INAONEKANA NI MINGI MNO KWA KIKWETE!!!!
 
1.
..uko wapi ushahidi kwamba Chenge aliingia bungeni na kunyunyuzia "vitu" kwenye vigoda vya wabunge? ..mnadai kuna tapes sasa wananchi tunaomba kuonyeshwa hizo tapes. the jury is on those who accusing Chenge of wrong doing. ..hivyo "vitu" vilinyunyizwa kwenye kiti cha Mwakyembe na wabunge wepi wengine? kwanini hao wabunge wengine hawatajwi ili tukajua wanaendelea vipi kiafya tangu siku ya tukio?

2.
Uchawi’ bungeni wafika Usalama wa Taifa, Polisi
Stella Nyemenohi, Dodoma
Daily News; Sunday,June 15, 2008 @00:01

Ofisi ya Spika imewasilisha taarifa kwa Polisi na Usalama wa Taifa ili washughulikie madai yaliyojitokeza hivi karibuni kuhusu Mbunge na Ofisa mmoja Mwandamizi wa Bunge kukutwa ndani ya Ukumbi wa Bunge wakifanya vitu vinavyodhaniwa kuwa ni ushirikina. Tukio hilo lililoripotiwa jana na baadhi ya vyombo vya habari, linadaiwa kufanyika Jumatatu wiki iliyopita likimhusisha Mbunge na Ofisa wa Bunge, ambao hata hivyo, hawakutajwa ni akina nani.

Imedaiwa kuwa watu hao walinaswa wakinyunyizia vitu visivyojulikana katika kila kiti cha Mbunge na kuishia cha Spika. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuahirishwa semina ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi mjini hapa, Spika Samuel Sitta alisema Kamanda wa Polisi mkoani hapa na Usalama wameanza kufuatilia zaidi tangu juzi ili kubaini ukweli wa suala hilo .

Ingawa alisema bado suala hilo ni uvumi na kwamba halina budi kusubiri kukamilika uchunguzi wa vyombo hivyo vya usalama , Sitta alisema hata hivyo tahadhari zote zinachukuliwa katika Ukumbi wa Bunge. Hata hivyo, alisema kwa upande mwingine, tahadhari zinaweza kuwa ngumu ikizingatiwa kuwa wanaohusishwa ni watu ambao hawana kipingamizi cha kuingia katika ukumbi huo.

Akizungumzia juu ya tukio hilo , Spika alisema, “Inashangaza. Lakini ni suala la uvumi, linachunguzwa. Tusubiri RPC na Usalama wa Taifa wakamilishe uchunguzi wao…tahadhari zote zinachukuliwa,” alisema. Spika alisema wakati wa tukio hilo, kamera sita zilizokuwa katika ukumbi huo, hazikuwa zimewashwa. Isipokuwa inadaiwa, kamera moja ya studio ndiyo iliyoonyesha watu hao. Hata hivyo, Sitta alisema kamera hiyo ilionyesha picha iliyofifia ambayo ni vigumu kubaini wahusika. Hata hivyo, alisema anaamini kuwa ikifikishwa kwa wataalamu, ndiyo watakaoweza kubaini wahusika
.

Mkuu joka kuu,

Heshima yako bro, unajua zamani nilikuwa ninakuheshimu sana thinking yo are for real, mpaka hapa majuzi nilipokuja kugundua who you are, hapa kwenye forum wengine sisi ni watu wazima ambao tunakuja hapa kwa nia njema na uchungu na taifa letu,

Hayo maswali yako hapo juu, ni nani hasa unayemuuliza hapa JF ambaye amesema kuwa ana tape ya bunge inyomuonyesha Chenge na shughuli yake? Humu kwenye hii topic kuna artcilce ngapi za magazeti yetu bongo ambayo yanasema wazi kuwa yamemuhoji Spika na amethibitisha hayo na yeye Spika ndiye aliyekuwa wa kwanza kusema wazi kuwa kuna Camera moja imenasa yalitokea na kwamba vyote hivi wamepatiwa wana usalama na polisi kwa jili ya uchunguzi ambao tumethibitishiwa na usalama wenyewe na polisi kuwa unaendelea,

sasa wewe unakuja na haya maswali yako ambayo sijui umpelekea nani hasa hapa JF? Mkuu mbona in the real life unaonekana ni mtu mwenye heshima kuiliko mambo unayoyafanya humu forum? Umenga'nga'nia tu kutaka uuuharibu huu mjadala exactly unachotaka nini hasa? Maana huenda una problem hapa tuna watu wa kila aina unaweza kusaidiwa mkuu, kama una maswali ya kutaka tape mpelekee Spika mkuu, hapa tunajaribu kujadili yaliyojiri kwa mapana na marefu na kuna tunaopata elimu kubwa sana bro, please can you understand this once and for all?

Hakuna anyekukataza maswali, lakini yapeleke yanapotakiwa hapa hakuna Spika wala chenge, mkuu mimi sio mtoto mdogo kwamba sijui unayoyafanya hapa ni kwamba unajidanganya sana bro, jaribu kuwa na heshima ili uheshimiwe mkuu!
 
Hii habari iliyofika saa hivi ni kiboko, magazeti yanajitahidi sana kuficha na kutofanya uchunguzi (baadhi) lakini JF siku zote inabaki kuwa sehemu maalum ya ukombozi wa Mtanzania. Kazi nzuri


Kuwa na miguu hakumaanishi kuweza kutembea
 
kaka unajua tatizo hapa ni moja...MTANDAO WAMEKOROFISHANA....hili tatizo tuliliona ..maana unapoongelea urais wa kikwete unaongelea KINGMAKERS wake kama ....ROSTAM AZIZ,EDWARD LOWASSA,NAZIR KARAMAGI,BENNARD MEMBE,ZAKIA MEGHJI et al....

hawa watu walifanya mbinu zote safi na nyingi chafu ikiwemo kutumia fedha za BOT,na kampeni za kuchafua wagombea wenzao...

LEO HII MTANDAO HUU HUU UNAMUELEMEA KIKWETE NA SANA SANA AMEBAKIA NA BENNARD MEMBE TU UPANDE WAKE FROM ORIGINAL MEMBERS WA MTANDAWO.......MEMBE OFFCOURSE KABAKI NA KIKWETE KWA SABABU NAYE LENGO LAKE NI KUONEKANA GOOD BOY ILI AWE RAIS 2015.....KIMSINGI MUHESHIMIWA RAIS KAELEMEWA NA KUNDI LAKE MWENYEWE....NA HALI HII HAIASHIRII USALAMA KWETU KAMA TAIFA!!!!

Mkuu Heshima mbele,

Very strong analysis ya the real ishu, hakuna la kuongeza isipokuwa tu hivi vita vya panzi huenda ikawa furaha yetu sisi dagaa, kwa sababu kama ninawaelewa vizuri wasiokuwa mtandao, wanaona kuna uwezekano mkubwa kwa siku za karibuni taifa letu kuishia kuwa na nothing, sasa dawa ni kuwabana hawa wahuni sasa.
 
1.

2.

Mkuu joka kuu,

Heshima yako bro, unajua zamani nilikuwa ninakuheshimu sana thinking yo are for real, mpaka hapa majuzi nilipokuja kugundua who you are, hapa kwenye forum wengine sisi ni watu wazima ambao tunakuja hapa kwa nia njema na uchungu na taifa letu,

Hayo maswali yako hapo juu, ni nani hasa unayemuuliza hapa JF ambaye amesema kuwa ana tape ya bunge inyomuonyesha Chenge na shughuli yake? Humu kwenye hii topic kuna artcilce ngapi za magazeti yetu bongo ambayo yanasema wazi kuwa yamemuhoji Spika na amethibitisha hayo na yeye Spika ndiye aliyekuwa wa kwanza kusema wazi kuwa kuna Camera moja imenasa yalitokea na kwamba vyote hivi wamepatiwa wana usalama na polisi kwa jili ya uchunguzi ambao tumethibitishiwa na usalama wenyewe na polisi kuwa unaendelea,

sasa wewe unakuja na haya maswali yako ambayo sijui umpelekea nani hasa hapa JF? Mkuu mbona in the real life unaonekana ni mtu mwenye heshima kuiliko mambo unayoyafanya humu forum? Umenga'nga'nia tu kutaka uuuharibu huu mjadala exactly unachotaka nini hasa? Maana huenda una problem hapa tuna watu wa kila aina unaweza kusaidiwa mkuu, kama una maswali ya kutaka tape mpelekee Spika mkuu, hapa tunajaribu kujadili yaliyojiri kwa mapana na marefu na kuna tunaopata elimu kubwa sana bro, please can you understand this once and for all?

Hakuna anyekukataza maswali, lakini yapeleke yanapotakiwa hapa hakuna Spika wala chenge, mkuu mimi sio mtoto mdogo kwamba sijui unayoyafanya hapa ni kwamba unajidanganya sana bro, jaribu kuwa na heshima ili uheshimiwe mkuu!
Umesiliba vizuri nilitaka kumjibu,palipo na maslahi ya taifa unazi na ushabiki woote uwekwe nyuma.sasa hivi nchi hii inakoelea tutakuja kuzipiga kama majirani zetu tusipokuwa macho
 
Back
Top Bottom