Kuna ubaya gani kumpa zawadi hii?

Kuna ubaya gani kumpa zawadi hii?

Kamanda hongera sana kwa ujasiri mkubwa wa zawadi nono kwa laaziz wako.Chamsingi muongezee kidereli cha uzi ili awe na full set ya vitendea kazi.
 
Wanawake wanapenda vitu romantic kama perfume, lip-stick,handbag e.t.c,,,,,they have no business mentallity.
 
Ndugu yangu elimu sio kitu tena, wa2 wapokitaa hawana kazi na shahada zao za juu daraja la kwanza. Unaambiwa kazi ni kazi elimu yako unaweka kando unapotafuta maisha. Jamaa kawaza jambo la maana lkn demu anazingua wakati mafundi wanapiga pesa kitaa naelimu zao za std 7.

Tatizo hapo demu anajio matawi ngoja kitaa kitamfunza tuu.
 
Yani kwenye ulimwengu wa teknohama mwendo wa mambo ya kisasa kabisa unawaza cherehani ya kuzungusha na mkono na kunyonga kwa miguu. Ungewaza zaidi ya hapo. Je yeye angekuletea zawadi ya "Tool box" na ngazi, na akaahidi kugharamia mafunzo yako kwa hivyo vifaa,ungejisikiaje?
 
Daaaah! We ni kiboko! Kwa elimu aliyonayo cherehani haina mashiko!! Kama ungelikaa nae ukamuuliza ni zawadi gani alihitaji, au kwakuangalia plan zake na fikra zake ungetambua ni kipi kingemfaa!!
Kweli elimu yote ile akaitundike kabatini na aanze kushona nguo?!?
Hapana, nawajua wahindi kibao wenye CPA wanafanya biashara ya maduka kitumbini!
 
Hapana ndg yangu, 'yale maneno yako na zawadi' yanaonesha una dharau sana na kejeli kwake. Bora ungemrushia pesa ili ajue atafanya nini, bora anunue mwenyewe wewe ungemshauri tu!
 
Kwani amesema anataka kujua kushona? Ilibidi ajue interest za mchumba Wake..ht mi ningenuna!
Hilo Nishamwambia Jamaa Yaan " Amebugi" Zawadi Ni Kucheza Na Hisia Z Mtu, Ukikosea, Umeharibu!!!
 
Chaa loool pesa hailetewagi vikao na maigizo _____ Mtume mtu na baloi wake wakakusanye kago lako hapo umelamba garasha tembea mbele kungali kweupe kabla hali haijaharibika hako ni kasichana ________ Hakakufai
 
kweli zawadi ni chochote na anayepewa zawadi anapaswa kushukuru kwa chochote. Ila fikra zangu zinaninong'oneza kwamba, unapotoa zawadi ni lazima ujue zawadi hiyo itamfaha vipi mpokeaji. Sawa, wewe ulifikiria kuwa ataweza kujiajiri kupitia hiyo cherehani lakini uliwahi kumchunguza ukaona ana interest hata ya kujishonea nguo? Naamini, hata kama amemaliza chuo ila kuna kitu kingine anapendelea kufanya though wewe hukijui. Usinunue zawadi kwasababu wewe unahisi itamsitiri, nunua kwasababu ni kitu ambacho mwenzako anakipendelea na kitakua useful kwake.
 
Cherehani anaweza kuitumia nyumbani pia.sio Kula nguo unapeleka kwa Fundi.HAYA ndio matatizo ya watu waliokosa sayansi kimu ktk elimu zao.
 
hivi ulinunua bei gani?
kama haitaki ailete nimpe pesa yake
.
 
Cherehani anaweza kuitumia nyumbani pia.sio Kula nguo unapeleka kwa Fundi.HAYA ndio matatizo ya watu waliokosa sayansi kimu ktk elimu zao.

Tatizo ni kwamba bidada anajua kuitumia hiyo cherehani? Angempeleka kwanza kozi ya ushonaji
 
Alikwambia anataka kuwa fundi mshoni?

Tena kakuheshimu angekufukuza na cherehani lako.

Punguani wahed.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom