Kuna ubaya gani kumpa zawadi hii?

Mbwa dume

JF-Expert Member
Jan 15, 2014
5,530
9,062
Nina girlfriend wangu ambaye tumedumu miezi kadhaa na tumepanga kuoana pindi uchaguzi utakapomalizika!

Amehitimu chuo cha biashara tangu mwaka Jana na mpaka sasa hajafanikiwa kupata ajira!

Nafahamika kwa wazazi wake nae anajulikana kwetu.

Sasa jana alisherehekea siku yake ya kuzaliwa
sherehe ilifanyika nyumbani kwao mida ya saa 1 jioni.

Wiki moja kabla ya sherehe hiyo nilikuwa safarini nikamuahidi kumnunulia zawadi nzuri kwa ajili ya birthday yake.

Sasa hiyo jana alikuwa na shauku ya kutaka kujua nimemletea zawadi gani !

Mda ulipowadia nilienda taratibu kumkumbatia kipenzi changu na kumzawadia cherehani mpya aina ya butterfly pamoja na kuahidi mbele ya umati kuwa nitatoa gharama zote za mafunzo ya kozi ya miezi mitatu ya ushonaji ili baada ya kumaliza mafunzo aweze kujiajiri.

Lakini cha ajabu mpenzi wangu alionyesha hakufurahishwa na zawadi hiyo!

Jana usiku kanisms kwamba "umenichukuliaje mimi lakn?"

Nikampigia akasema eti alitegemea ningemnunulia zawadi ya maana kumbe hovyo!

Leo nimemtumia ujumbe tuonane hakunijibu nimejaribu kumpigia mda wote hapokei simu yangu!

Naomba mnishauri eti hiyo zawadi ina ubaya gani au ningemnunulia nini ikiwa sina uwezo wa kununua gari?!
 
Huyo sio wife material

Nimesema hivo kwa sababu kama kweli anakupenda kwa dhati.hata ungempelekea mchanga Wa pwani angefurahia .
Zawadi ni chochote we pokea tu.

Kimbia fasta mzee waibiwa.ukilegea utakaa uchi nzi watakung'ong'a.
 
Daaaah! We ni kiboko! Kwa elimu aliyonayo cherehani haina mashiko!! Kama ungelikaa nae ukamuuliza ni zawadi gani alihitaji, au kwakuangalia plan zake na fikra zake ungetambua ni kipi kingemfaa!!
Kweli elimu yote ile akaitundike kabatini na aanze kushona nguo?!?

ninachokiangalia hapa ni namna ya kumsaidia aweze kujiajiri!
sasa kumnunulia cherehani ni kosa?
au ningemnunulia mzani wa kupimia uzito
awe anazunguka nao mitaani?
vinginevyo asubiri mwakani nikipata hela nianzishe mradi wa choo cha kulipia halafu awe anasimamia huo mradi.
siku zote biashara mnazozidharau ndio watu wanatajirikia!
 
binadamu tunatofautiana sana cherehani haina maana awe fundi nguo no, atakapokuwa nafamilia aweze hata kuripea nguo zikitatuka hata kuchanika, apinde kanga vitenge, ashone nguo zakushindia wanae. mf, mimi mamangu alinitunuku cherehani siku ya send off akanihusia, nanukuu "mwanangu nimekuandalia zawadi hii ikusaidie kwenye familia yako, enzi zetu tulitumia sindano yamkono kuripea nguo ila teknolojia imewarahisishia sana hivyo itumie vizuri silazima kwenda kwa fundi kama tatizo unaweza litatua" ndo nikajua kumbe hata mi na degree yangu ya sheria bado natakiwa kuwa fundi? duh! today 7yrs bado natumia cherehani yamama yangu, kwa matumizi yafamilia
 
ninachokiangalia hapa ni namna ya kumsaidia aweze kujiajiri!
sasa kumnunulia cherehani ni kosa?
au ningemnunulia mzani wa kupimia uzito
awe anazunguka nao mitaani?
vinginevyo asubiri mwakani nikipata hela nianzishe mradi wa choo cha kulipia halafu awe anasimamia huo mradi.
siku zote biashara mnazozidharau ndio watu wanatajirikia!
Teh teh..We jamaa hauko serious hata kidogo
 
Wala hujakosea kiongozi....

Hawa mabint wanadhani kuajitiwa ndio big deal sana wakati hakuna maana yoyote...

Unakuta mtu kamaliza chuo na haamini kama aanafanya kazi hadi aajiriwe....

Tumeaminishwa ujinga sana....
 
Ni mcharuko huyo binti, anaamini kuwa fundi nguo ni kukosa elimu ? Lakini kwa ujuha anapoteza Muda kwenye maboutique kutafuta mavazi yaliyoshonwa na mafundi nguo.
Mpige shule huyo hana mpango wowote kichwani zaidi ya kuja kutegemea pay yako kwa kila kitu, kama ana mapause tupa kule...
 
Alitegemea labda utampa ka ufunguo ka vitz. wewe unaleta cherehani duu nomaaaa....wakati mwenzio anawaza kutembea akiwa amekaa! kajipange upya
 
Upeo wake mdogo,kaa nae chini umjuze vizuri,
Yawezekana wewe kwake ni boy wa kupita so hana mpango wa kuwa mke wako.
Ila kama unampango wa kumuoa,cha msingi mwambie aitunze Cherehani yaweza kuwa ni mwanzo wa kiwanda cha kushona covers za viti vya harusi na mikutano,au yaweza kuwa mwanzo wa kiwanda cha overalls na uniform za viwandani.
Hana upeo ,muelimishe akiwa mzito Hafai kuoelewa ni kula nae bata ukiwa nazo kama huna unawapisha wenye visu wale nae bata
 
hahahaha... pole sana ndugu. sasa naona jipange mnunulie Eicher au dcm abebe abiria mjini. maana hakuna namna anabagua ajira.
 
ninachokiangalia hapa ni namna ya kumsaidia aweze kujiajiri!
sasa kumnunulia cherehani ni kosa?
au ningemnunulia mzani wa kupimia uzito
awe anazunguka nao mitaani?
vinginevyo asubiri mwakani nikipata hela nianzishe mradi wa choo cha kulipia halafu awe anasimamia huo mradi.
siku zote biashara mnazozidharau ndio watu wanatajirikia!

Kweli wewe ni mbwa dume nimecheka sanaaa hiyo zawadi ya mizani kupima uzito lazima angekutukana. Kwa staili yako ya kutoa zawadi kweli we ni great thinker
 
Jifunze kusoma alama za nyakati mbaba. Kwani alikwambia anataka kuwa fundi cherehan? Jiongeze wakati mwingine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom