Kuna ubaya gani kumpa zawadi hii?

Kuna ubaya gani kumpa zawadi hii?

nawe tumiaga akili pia....ungemuuliza...side b ni kuwa saafi umejua kuwa si wife material kama vp kula bati nawewe
 
Hiyo Stori Isikutishe, Jamaa Mwenywe Ajui Interest Ya Mtu Wake, Yaan " Amebugii" Tuu,, Heaven Sent Kma Mambo Ya Lishe Anayakubali, Mzawadie Tuu...Si Unajua Vitu Vingine Usimfosi Mtu Afanye Ilihali Apendi..Usije Ukanuniwa Na Ww Kma Jamaa.

Mimi napenda mtu ajiajiri!
mbona hata Mimi nna elimu ya form 4 nlipomaliza nlijiunga JKT miaka 2
baada ya kumaliza nilikosa ajira kabisa nikaamua kukomaa nlipopata pesa kidogo nikanunua bunduki aina ya gobore na sasa nimejiajiri ni mlinzi wa kukodiwa!
na ninapata pesa inayoniwezesha kusukuma maisha hata yeye anajua!
 
hahahahaha! thread zngne bhanaaah ,unamnunulia dada duu chereani?? hahahaha! umebugi ,ila tatz umedate nae muda mfyupi sanah umeshndwa kujua anapenda k2 gan ,trust me hata kama ungemnunulia hata kamdoli angeridhka kuliko huo mcherehani.
 
Card nitakuletea Au nitamkabidhi rubii Akuletee lakini nimeimis ile kisawasawa

Umemiss nini? Niletee mwenyewe au mpe wifi Apologise lady aniletee maana wewe unaweza ukatokomea kama ulivyotokomea na zile hela zangu
 
Last edited by a moderator:
Umemiss nini? Niletee mwenyewe au mpe wifi Apologise lady aniletee maana wewe unaweza ukatokomea kama ulivyotokomea na zile hela zangu
Nimemic kale kakinanda kako kenye lafudhi ya Kimasai.. nitampa dada lakini kuwa makini nae kwani hata yeye ni mpenda pesa kupindukia
 
Last edited by a moderator:
Nimemic kale kakinanda kako kenye lafudhi ya Kimasai.. nitampa dada lakini kuwa makini nae kwani hata yeye ni mpenda pesa kupindukia

Kwani kuna asopenda pesa dunia hii? Wacha weeee!!
 
Nina girlfriend wangu ambaye tumedumu miezi kadhaa na tumepanga kuoana pindi uchaguzi utakapomalizika!

Amehitimu chuo cha biashara tangu mwaka Jana na mpaka sasa hajafanikiwa kupata ajira!

Nafahamika kwa wazazi wake nae anajulikana kwetu.

Sasa jana alisherehekea siku yake ya kuzaliwa
sherehe ilifanyika nyumbani kwao mida ya saa 1 jioni.

Wiki moja kabla ya sherehe hiyo nilikuwa safarini nikamuahidi kumnunulia zawadi nzuri kwa ajili ya birthday yake.

Sasa hiyo jana alikuwa na shauku ya kutaka kujua nimemletea zawadi gani !

Mda ulipowadia nilienda taratibu kumkumbatia kipenzi changu na kumzawadia cherehani mpya aina ya butterfly pamoja na kuahidi mbele ya umati kuwa nitatoa gharama zote za mafunzo ya kozi ya miezi mitatu ya ushonaji ili baada ya kumaliza mafunzo aweze kujiajiri.

Lakini cha ajabu mpenzi wangu alionyesha hakufurahishwa na zawadi hiyo!

Jana usiku kanisms kwamba "umenichukuliaje mimi lakn?"

Nikampigia akasema eti alitegemea ningemnunulia zawadi ya maana kumbe hovyo!

Leo nimemtumia ujumbe tuonane hakunijibu nimejaribu kumpigia mda wote hapokei simu yangu!

Naomba mnishauri eti hiyo zawadi ina ubaya gani au ningemnunulia nini ikiwa sina uwezo wa kununua gari?!

Mshamba huyooo na anamawazo mgando..... inipe mimi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom