Kuna mtu alishawahi kupata hii mikopo ya 10% ya Halmashauri inayotetewa sana na wabunge wa CCM Bungeni?

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,834
18,835
Wakuu niaje, kuna mikopo ambaypo fedha zake hutengwa kwenye asilimia 10 ya mapato ya halmashauri, mikopo hii inaelezwa inatolewa kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

sasa kwenye bajeti ya mwaka huu imependekezwa kwenye huo mkopo badala ya kutolewa asilimia 10 ya mapato, itolewe tu asilimia 5 na hiyo asilimia 5 nyingine itumike kujenga maeneo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo (machinga) kufanyia biashara zao.

lakini hili limekumbana na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wengi wa CCM kuwa hii mikopo inasaidia sana vijana na wanawake na kuiondoa italeta balaa janga kubwa sana.

sasa hii mikopo inatolewa na ina msaada kiasi hicho kweli kama inavyosemwa? maana nilisikia pia kutoka kwa Rais Samia mwenyewe, kuwa hii mikopo inatolewa kwa kujuana na rushwa na inatumika na wabunge kuhonga watu wao ili wawapitishe tena.

je nauliza kuna mtu aliyeweza kupata hii mikopo? au kuna mtu unayemjua aliwahi kupata huu mkopo? ama uliwahi kuomba huu mkopo ukanyimwa na ukapewa sababu gani.
 
Sidhani Kama hiyo mikopo ipo kweli! Lingekuwepo au waombaji wangekuwepo tungeliona huku Jf kwa kusifia au malalamiko.

Hata hao lumumba inawezekana na wao hawapati na Kama wanapata basi watakuwa wameweka utaratibu wa Siri Sana. Hasa hasa madiwani watakuwa wanajuwa hiyo Siri.

Halmashauri wanamambo inawezekana wanawakopesha watoto wao na ndugu zao. Kilichopo tuhamasishe vijana waende watatuletea jibu zinavyotolewa.
 
Wapo walio pata


Ila imeongeza changamoto za maisha ya vijana

Maana kuunda kikundi cha watu wenye utambuzi tofauti tofauti na kuwawapa hela kumeongezea maskini

Vijana wengi hukimbia mahali walipo patia mkopo na kwenda sehemu nyingne

Hapo tayari wanao baki hutakiwa kulipa mkopo huo mpaka uishe

Kingne ni ufinyu mdogo wa masoko ya bidhaa zinazo weza kuzalishwa na hao wanao chukua mkopo

Na Mara nyingi wengi hujikuta wakilazimishwa kuwa na mradi fulan wakati wao wana malengo ya kutanua ofisi zao mwisho wana kikundi hujikuta wakigombana na kuachiana mzigo wa madeni

Kuna haja ya kufanya tathimini upya kama wanaweza kuwakopesha watu kulingana na mwelekeo wao

Na pia kuna sababu ya serikali kuja na mfumo wa vijana wakopesheke na benki wao wakiwa wadhamini ili kuwezesha vijana kupata mitaji sahihi na kwa wakati
 
Wakuu niaje, kuna mikopo ambaypo fedha zake hutengwa kwenye asilimia 10 ya mapato ya halmashauri, mikopo hii inaelezwa inatolewa kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

sasa kwenye bajeti ya mwaka huu imependekezwa kwenye huo mkopo badala ya kutolewa asilimia 10 ya mapato, itolewe tu asilimia 5 na hiyo asilimia 5 nyingine itumike kujenga maeneo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo (machinga) kufanyia biashara zao.

lakini hili limekumbana na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wengi wa CCM kuwa hii mikopo inasaidia sana vijana na wanawake na kuiondoa italeta balaa janga kubwa sana.

sasa hii mikopo inatolewa na ina msaada kiasi hicho kweli kama inavyosemwa? maana nilisikia pia kutoka kwa Rais Samia mwenyewe, kuwa hii mikopo inatolewa kwa kujuana na rushwa na inatumika na wabunge kuhonga watu wao ili wawapitishe tena.

je nauliza kuna mtu aliyeweza kupata hii mikopo? au kuna mtu unayemjua aliwahi kupata huu mkopo? ama uliwahi kuomba huu mkopo ukanyimwa na ukapewa sababu gani.
Binti yangu ameomba mkopa huu yeye na kikundi chake mwaka wanne Sasa hawajibiwi wala hawapewi
Wamekataa kuhonga
 
Wakuu niaje, kuna mikopo ambaypo fedha zake hutengwa kwenye asilimia 10 ya mapato ya halmashauri, mikopo hii inaelezwa inatolewa kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

sasa kwenye bajeti ya mwaka huu imependekezwa kwenye huo mkopo badala ya kutolewa asilimia 10 ya mapato, itolewe tu asilimia 5 na hiyo asilimia 5 nyingine itumike kujenga maeneo maalum kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo (machinga) kufanyia biashara zao.

lakini hili limekumbana na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wengi wa CCM kuwa hii mikopo inasaidia sana vijana na wanawake na kuiondoa italeta balaa janga kubwa sana.

sasa hii mikopo inatolewa na ina msaada kiasi hicho kweli kama inavyosemwa? maana nilisikia pia kutoka kwa Rais Samia mwenyewe, kuwa hii mikopo inatolewa kwa kujuana na rushwa na inatumika na wabunge kuhonga watu wao ili wawapitishe tena.

je nauliza kuna mtu aliyeweza kupata hii mikopo? au kuna mtu unayemjua aliwahi kupata huu mkopo? ama uliwahi kuomba huu mkopo ukanyimwa na ukapewa sababu gani.
 
Temeke : Mwenyekiti wa ccm wa wilaya alipewa mil 300 peke yake ili afanyie kazi zake kinyemela , tabu ikaja baada ya kushindwa kurejesha
 
Hivyo vikundi ni hewa tu.wewe fatilia mtaani kwako uone kama kuna kikundi kimepata.vinakuwa ni vikundi hewa na ata akija waziri au kiongozi wa serikali wataletwa mamluki waonekane ndo wanavikundi kumbe ni vijana tu wa mtaani wanapewa posho baadae wanasepa.
 
Hamlashauri ya Ubungo chini ya CHADEMA angalau tuliona hata Bajaj wamekopeshwa vijana.

Swali, je kuna uwazi kiasi gani kwenye huu mfuko? ni bora yapewe mabenki ndio yafanye hiyo kazi ya kukopesha na kudai
 
vikundi ni hewa tupu,mie kuna ndu yangu alifuatilia WIlaya ya ILala,alikanyagia mpaka basi,baadae wakaambiwa kuwa wanasiasa wanaojiinasibu wanawakilisha wananchi bungeni ndo wamegawana kupitia vikundi hewa,SSH yupo Sahihi huko ni upigaji kwa kwenda mbele kazi ni kuwachosha vijana na akina mama
 
Hizi fedha zinatajwa kwenye majukwaa ya kisiasa tu lkn kiuhalisia huwa hazitolewi.
 
Back
Top Bottom