Kuna Mchezo Unachezwa!

Kuna Mchezo Unachezwa!

Mchezo wenyewe wanataka kuuchezea kwenye juke box ya tune waipendao wao ilihali wachezaji ni sisi ndo tunaotakiwa kuicheza, najiuli swali moja hawa watu kwa nini wanataka kutuwekea santuri ambayo hatujakubaliana nao, lakini ni kwa nini ni wagumu kuelewa hawa?

Tulishawaeleza tangu mapema walipoweka ile santuri ya kwanza tulitoikataa kuwa hatutakuwa tayari kuicheza santuri ambayo sisi hatuichagua iwe kwenye background ya huyu dj ambaye hata uwezo na kazi yake tunahofu naye. Natoa angalizo huku kucheza kwetu bila kuangaliana mwisho tutaishia kukanyagana halafu mwisho wa ngoma tusione na laha ya mchezo tuliokuwa tunacheza
 
Kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Mchezo unaochezwa na wenye kucheza hucheza. Mchezo huo huchezwa na wale wenye kuupenda mchezo huo. Ukikaa pembeni wanakushangaa kwanini hutaki kucheza na ukiingia kucheza utakavyo watakuuliza 'mbona huchezi kama sisi'? Ukiwaambia mchezo wenu haufuati kanuni wala mlio wa muziki watakuambia haijalishi wewe cheza tu alimradi uonekane unacheza. kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Ukialikwa kucheza utacheza au utabakia kutazama? Au utajaribu kutaka mchezo ubadilishwe ili wengi waufurahie kwa kufuata kanuni, na mirindimo yenye kuendana na uzuri wa mchezo wenyewe?

Ndugu zangu, kuna mchezo unachezwa, na wapo wenye kupenda kucheza mchezo huo!



MMM
MMJ kwa kweli wewe ni mchonga maneno!
Lakini unasababisha watu kufikiri.

Mchezo hata uwe mzuri namna gani kama wengi wana njaa na magonjwa hawawezi cheza!
Muziki wake hata ungepigwa na Luambo Luanzo makiadi, kama uko ICU mmmmh!
Kama hujaelimika wala hutajua kinachoendelea, utakuwa wajipakulia mziki kwa masikio tu lakini unabakia msindikizaji tu yaani kama zuzu!
Na ni kama ulivyoainisha, hata muziki unapokaribia na utakapoisha kabisa, wengine watabakia wanakata viuno, sasa huo ni mchezo unaofaa kweli?
Heri nisiucheze, nitapigania uanzishwe mchezo mzuri ambao wengi zaidi wataucheza na kadri idadi ya wachezaji itakavyoongezeka, basi na furaha yake hata Mungu ataisikia na kujibu na baraka zake!
Kinyume chake ni balaa tupu!
 
Kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Mchezo unaochezwa na wenye kucheza hucheza. Mchezo huo huchezwa na wale wenye kuupenda mchezo huo. Ukikaa pembeni wanakushangaa kwanini hutaki kucheza na ukiingia kucheza utakavyo watakuuliza 'mbona huchezi kama sisi'? Ukiwaambia mchezo wenu haufuati kanuni wala mlio wa muziki watakuambia haijalishi wewe cheza tu alimradi uonekane unacheza. kuna mchezo unachezwa na wapo wanaopenda kucheza mchezo huo. Ukialikwa kucheza utacheza au utabakia kutazama? Au utajaribu kutaka mchezo ubadilishwe ili wengi waufurahie kwa kufuata kanuni, na mirindimo yenye kuendana na uzuri wa mchezo wenyewe?

Ndugu zangu, kuna mchezo unachezwa, na wapo wenye kupenda kucheza mchezo huo!

MMM
Mzee Mwanakijiji, with due respect, we all know politics is a dirty game, and we all knows the games people play!.

Kabla ya mchezo wowote, rules of the game zinakuwa put forward, timu zote ninakubali kuwa zita play by the rules, on the middle of the game, unakuta rafu za ajabu na refa anazifungia macho ili game iendelee wewe ushindwe. Kwenye rules of the game, pia wamekuwekea provision kama utayaona hayo unayoyaona, unatakiwa ufanye nini within the rules ili kuusimamisha mchezo na wewe kutendewa haki, haki yako ni kusimama kucheza na kubaki uwanjani kushinikiza fair play vinginevyo pambano livunjike.

No matter how bad your situation is, don't loose your temper, you can make it worse!. Hata kama mnajua refa hawatetei haki, bado ni lazima kupeleka timu uwanjani na kutumia kanuni kumlazimisha refa kutenda haki, na sio ku play no show, wenzenu watajipatia ushindi wa mezani!.

Isome kwa makini kanuni ya 86, kwa nini Chadema hawakuitumia kuusimamisha muswada huo?. Hivi unajua kuwa hotuba ya kambi ya upinzani ni pre-requisite ili muswada wa serikali usonge mbele?. Kwanini Mhe. Lissu hakuitumia kanuni hiyo ya 86 kutosoma hotuba ya kambi ya upinzani, hivyo muswada lazima ungekwama kuwasilishwa kwa mara ya pili na ungelazimika kurudishwa kwenye kamati?!.

Kwa vile Chadema had a chance, but lost the chances they've been given tena kwa kuwafungulia mlango wa kuendelea na safari, huko kususia wataachieve nini?.

Kwenye mapambano yoyote, au vitani, kuna ile strategy ya "no retreat, no surender", hapa ni kupigana mpaka risasi ya mwisho, na tone la mwisho la damu linamwagika, at the end of the day, unakuwa umekufa kishujaa kama Ghadafi!.

Stategy nyingine ni ile ya "if you can't beat them, join them", ili ujijenge upya na kuja ku fight them from within. Hii ni strategy ya compromise, "if you can get what you want, take what you get" ili safari iendelee na sio kuisusa safari jumla, wakati wenzako wanaendelea, mwisho wa siku, watakaofanikisha safari, ni wale tuu waliofika mwisho wa safari no matter how rough the road was!.
 
MM usinambie sasa umehamia ktk kutunga Tungo za Bongo fleva...Anyway najua mtu mzima kama wewe ukisema kitu kina mantiki ndani yake..we just need to figure out unamaanisha nini
 
Kifupi ni kwamba 2015 itafika bila katiba mpya MUITAKAYO - na sababu zitakuwa hizi hizi za kucheza mchezo ule ule unaojulikana.. Ngoma zizimwe tusikie muimbaji mmoja akimba lilotakiwa kuimbwa, kisha sote tuimbe Mungu ibariki Tanzania kwa furaha zote!
 
Mie nahisi mchezo huu utakuwa unachezwa na Magamba, labda Mwanakijiji atatufafanulia zaidi kuhusu mchezo huu unaochezwa.
 
Dah mbona bado niko kizani
Washeni hata disco light kwa dk chache hata ambao hatuchezi tuonekane tunacheza. Bado niko salenda briji . Nasubiri kuona au kujua huo mchezo
 
Isome kwa makini kanuni ya 86, kwa nini Chadema hawakuitumia kuusimamisha muswada huo?. Hivi unajua kuwa hotuba ya kambi ya upinzani ni pre-requisite ili muswada wa serikali usonge mbele?. Kwanini Mhe. Lissu hakuitumia kanuni hiyo ya 86 kutosoma hotuba ya kambi ya upinzani, hivyo muswada lazima ungekwama kuwasilishwa kwa mara ya pili na ungelazimika kurudishwa kwenye kamati?!.

Kwa vile Chadema had a chance, but lost the chances they've been given tena kwa kuwafungulia mlango wa kuendelea na safari, huko kususia wataachieve nini?.

Ni miongoni mwa 'tactics' za mchezo unaochezwa! Just for ur info
 
Kifupi ni kwamba 2015 itafika bila katiba mpya MUITAKAYO - na sababu zitakuwa hizi hizi za kucheza mchezo ule ule unaojulikana.. Ngoma zizimwe tusikie muimbaji mmoja akimba lilotakiwa kuimbwa, kisha sote tuimbe Mungu ibariki Tanzania kwa furaha zote!

sasa mlitegemea katiba mpya italetwa na vilaza na wajinga wale wale? Tz bwana...kila siku tunaimba ngonjera zile zile. Lakini mwisho wa siku mchawi wetu tunamjua. CCM ndio mchawi. Tatizo kuna wapumbavu wengi ambao hawataki kuona tunaendelea. Ondoa hilo litakataka, nchi iendelee. Kweli ningekuwa mwanasiasa hata kukaa meza moja na ccm nisingeweza. Maana ni sawa na Mungu na shetani kukaa meza moja.
 
Mchezo wanaocheza wao sio mchezo bali wanachezeana.mchezo mchezo kesho ni mauti kwao.na hapo ndio mwisho wa mchezo.
 
Yes mchezo wenyewe ni katiba. Kila mtu anaitaka lakini wananchi walio wengi including wapinzani wamegoma kucheza mpaka kanuni zifuatwe. CCM wanatulazimisha tuingie tucheze lakini bila kanuni hamna raha ya mchezo. Ni wazi upinzani wamekataa kabisa kuingia kucheza; wamekaa pembeni, sijajua wanachi wameamu nini hasa. Je wamekaa pembeni tu au wanampango wakuingia na kuvuruga mchezo mzima ili tuanze upya kwa taratibu/kufuata kanuni? Au watakubali kucheza kama wanavyoshauriwa na CCM bila kufuata kanuni?

yah hii ndio maana ya msg ya MMJ, ongezea na hii kama alivyosema Mwanakijiji muziki utakwisha wao watendelea kucheza kama viziwi!!! namanisha wabunge especially wa ccm wanaopiga makofi bungeni kwa kushabikia kitu wasichokuwa na upeo wa kukifikiria (mazuzu) watakujastuka walikuwa wanacheza mchezo wasio ujua na usio na kanuni!!!
 
Well inaonekana wengine hata mlikuwa hamjui kuna mchezo unachezwa.. well lets see tutaona muziki utakapoisha na kukuta watu wanaendelea kucheza... kumbe walikuwa viziwi!

Ni kweli kabisa mkuu, mtu kama Mh. Lusinde (kiziwi) anamtukana Mh.Lissu eti anakosea step za muziki wakati yeye ndo hazisikii beats! ha ha haaaa nimecheka sana leo!
 
only wise can dance the melody of life,
I'm wise enough to dance this melody.
 
wengine tumwpitia St. KAYUMBA hatukuweza kudadavuliwa hao akina Malenga Wapya wala Shaaban Robert. Sasa tuweke wazi tuujue mchezo huo
 
He who pays the piper chooses the tune........................
Nawasilisha.
Mungu Ibariki Tanzania!
 
Back
Top Bottom