Hii ni summary ya matukio yaliyojitokeza kuhusu Derby ya Kariakoo na Maoni yangu. Nagusia mambo muhimu tu, sitaorodhesha maoni sijui ya wachambuzi maana wengi wapo na bias:
- Inatangazwa tarehe ya Derby ya Kariakoo kama itachezwa tarehe 8 March
- Maandalizi yamepamba moto huku kila pande ikijinasibu kumkanda mwenzake.
- Zinaanza tetesi kuwa Kibu na Mpanzu hawatakuwepo huku wakala wa Mpanzu akidai kumaliziwa kwa deni lake kabla ya siku ya Ijumaa (Wadau wa michezo wanasema minding game lakini kiuhalisia kuna majeruhi halisi wakiwemo Kipa na beki tegemeo)
- Simba wakiwa na escort ya polisi na msafara wa mabasi matatu, wanaenda uwanjani wakitaka kufanya mazoezi ya mwisho kuelekea kwenye mchezo huo.
- Wanaibuka mabaunsa wa kutengeneza wanawauzia Simba wasiingie uwanjani
- Saa saba usiku Simba wanatoa taarifa kwa umma hawatashiriki mechi kwa kuwa wamezuiwa mazoezi ya mwisho (Hakuna Kanuni inayoruhusu timu ngeni kususia mechi, hapa hata wenyewe ukiwauliza wanakujibu wamezoea kutuchezea sasa tumeamua ubaya ubwela)
- Asubuhi Yanga wanasema watapeleka timu uwanjani kwani wanajua mechi ni hiyo siku
- Saa nee Bodi ya ligi inasema mchezo huo upo pale pale hivyo mashabiki muendelee kujiandaa kwenda uwanjani (Binafsi nilikua njiani na basi la asubuhi natokea Iringa kwenda kuangalia Derby, baada ya kuona taarifa ya Simba ile asubuhi ikabidi nishuke Morogoro saa mbili nifanye utaratibu wa kurudi Iringa. Nikapata gari nafika Mikumi kama saa nne naona taarifa ya bodi inasema game ipo. Ikabidi nidrop Mikumi nichukue usafur kurudi tena Dar kuangalia Game. Nafika Chalinze nasikia tena Bodi imeghairisha mchezo huo. Damn!)
- Saa nane Bodi ya ligi inatangaza kuahirishwa kwa mchezo huo
- Saa 11 Yanga inapelekea timu uwanjani
- Yanga wanatangaza hawatashiriki Derby ingine tena msimu huu
- Yanga wanatuma barua kwa bodi ya ligi kuomba wapewe point tatu
- Yanga wanatuma barua kwa bodi ya ligi kuomba warudishiwe gharama zao
- Yanga wanafanya maamuzi kwenda CAS
- Rais wa TFF ansema wanachofanya Yanga ni utoto
- Manara amjibu Rais wa TFF aache dharau
- Mwenyekiti wa bodi ya ligi anaom,ba busara itumike kwenye hilo (Sio kanuni tena bali hekima na busara zitumike)
- Wazee wa Yanga wanatangaza kutoshiriki kwa timu kwenye Derby ingine.
- Kanuni zipitiwe upya, kipengele cha kushushwa daraja kwa timu isipotokea uwanjani kiondolewe, bali kuwe na kipengele cha kuipa pint tatu na magoli matatu timu iliyofika uwanjani (Kipengele hiki ndio kinawapa shidaa bodi ya ligi kwenye kufanya maamuzi)
- Bodi ijiuzulu, tarehe ya derby itangazwe upya na bodi nyngine mpya
- Timu zote zilizop[o ligi kuu zipewe hadhi sawa ndio tutakuwa na ligi yenye ushindani, Marefa na waamuzi wanaofanya maamuzi ya tutat kupendelea timu za Kariakoo wachukuliwe hatua kali ikiwenmo kutojihusisha na mpira milele
- Hakuna kudekeza timu( Ikumbukwe Simba ilishawahi kukataa udhamini wenza wa GSM kwenye ligi yetu wakagoma. Ikabidi GSM ajitoe na kuna baadhi ya timu zikaomba udhamini wa GSM, Simba wanalalamika GSMS kudhamini timu nyingi. Na sasa kagom kucheza Derby Bodi imebeba mzigo wa Simba. Hii hali ikiendelea ipo siku watakataa kucheza na timu Fulani, watakataaa jucheza uwanja Fulani, watakataa refa na mwishowe watakuja kukataa hata baadhi ya wachezaji wa timu pinzani wasiwepo kwenye mechi za Simba. Hii yote ni matokeo ya kudekezwa.
- Mwisho TUKATAE UHUNI WOWOTE UNAOFANYIKA KWENYE LIGI YETU IWE UNANUFAIKA NAO AU HUNUFAIKI KWA SABABU IPO SIKU ITAKUREJEA (KARMA IS A BITCH)