Kumekucha TTCL wateja sasa bwerere!

Kumekucha TTCL wateja sasa bwerere!

Kwamba wewe unajitoa hauhusiki kwenye kuchagua viongozi?

Hili la TTCL sio la Magufuli, hili ni suala la nchi kupenda kutumia vyakwetu kuliko vya nje.

Mi sijaona kosa hapo. (Ni mtazamo wangu)
umenena vyema ni mtazamo wako.

kuna mtazamo wa sheri,FAIR COMPETITION ACT, NA MAHAKAMA YAKE IPO UBUNGO PLAZA, FAIR COMPETITION TRIBUNAL, ni kosa, na haikubaliki.

mwishowe mtaaambiwa kila mtu anunue bidhaa kwa mjumbe wa CCM
 
Nashauri serikali imkate kila mtumishi Tsh 6000 kila mwezi kisha imuingizie kama vocha kupitia hiyo line ya TTCL atakayosajiliwa!Hii itawaondoa wale ambao wana mpango wa kusajili na kuweka kabatini hizo line,hahahahaaa,TTCL oyeeeeeee,watumishi Oyeeeeeee!!!!
Wakatwe elfu 15 ya vocha ,wawe wanaingiziwa kila mwezi ,Ari Mpya Nguvu Mpya na Kasi Mpya Pongezi kwa Jakaya kwa Kuleta CHUMA,na sasa tunaona mabadiliko WaTZ tuko Nyuma yako,Tulishazoea kuitwa kichwa cha mwendawazimu.....Dr Levy
 
Sijui na mikataba yao nayo itabadilishwa kuongeza kipengele cha umiliki wa kadi ya simu ya TTCL?
IMG-20190530-WA0001.jpeg
IMG-20190530-WA0001.jpeg
 

Attachments

  • IMG-20190530-WA0000.jpeg
    IMG-20190530-WA0000.jpeg
    43.1 KB · Views: 13
HATIMAYE SAUTI YENYE MAMLAKA IMEWARUDISHA NYUMBANI!!
RUDI NYUMBANI KUMENOGA PENDA CHAKO.
 
Watanzania wenye simu za mkononi wanafikia 43,621,000 na kati ya hao TTCL ina subscribers 711,411 (1.6%). Serikali ina jumla ya wfanyakazi 800,000. Hata kama wote hawa waki-subscribe kwa TTCL watafikia 1,511,411 (3.4%). TTCL isitegemee itatoboa kwa kubebwa bebwa. Badala yake iandae marketing strategy itakayowawezesha kuongeza market share ili angalau ifikie 20% ndani ya miaka 3 ijayo.
...kati ya hao wafanyakazi 800000 mimi simo hivo wamebaki 799999
 
Watumishi wa mma hamfiki 1,000,000 mkianza kujibagua na kuwa na mtandao wenu wenyewe sijui mitaani mtaonekanaje maana sasa hivi kupigiana simu ni Mtandao mmoja kwemye Mtandao huo huo sasa nyie milioni 1,000,000 mkiwa mtandao wenue na sisi 19,000,000 tukiwa mitandaoni hii mingine hamwone kwamba hawa 19,000,000 ndio watatoa biashara kubwa zaidi ya hao 1,000,000?

Kampuni binafsi za simu zinaweza jiunga zikaisusia TTCL ikafa kifo cha mchana kweupe!

Wanaweza ichapa kwenye calls interconnection tu!

Au wakiamua kukata mobile money interconnection yaani TTCL wajitegemee wao kama wao bila uhusiano wowote na makampuni binafsi!

My friend,TTCL will find hell on earth!

Serikali hua inaniboa sana wanaponifanya wao wana upper hand on everything!

Delusional motherfvckers!
 
Kwa nini Mfanyakazi wa TiGo kuwa na line ya tiGo, Vodacom kuwa na laini ya Vodacom, AirTel kuwa na line ya Airtele , Zantel kuwa na line ya Zantel (mwajiri) , nk siyo issue, ila Mfanya kazi wa Serikali kuwa na line ya mwajiri (Shirika la Mawasiliano la Taifa (TTCL) inaonekana ni issue?! Naomba kujua.
..hoja yako Dhaifu kwani wafanyakazi wote wa serikari wanafanya kazi TTCL?,..Pia mbona wakiomba kuongezewa mshahara wanakataliwa,..so kutumia line za TTCL iwe hiari
 
Hivi unsjua kwamba TTCL iki-perform vizuri itatoa gawio kubwa serikalini,gawio ambalo litasaidia kukulipa hata wewe mshahara?Usione kama TTCL ni kitu cha mbaali,no it is so close to you.
...gawio litaenda kwenye miundo mbinu siyo mishahara..
 
Kwa mtandao husika . Mfano tigo pesa iko Kila kona ya nchi.Nikitaka vocha nina uhuru nikitaka ya kukwangua napata .Nikitaka ya kununua tigopesa naweka pesa mfano elfu Moja kwa wakawa wa tigo pesa nanunua vocha ya elfu Moja exactly.Tuje upande wa TTCL vocha zao kupata shida , TTCL pesa shida sehemu nyingi za nchi hazipo kabisa ikiwemo Dar es salaam.Unachoongea wewe unakijua mwenyewe .Hiyo TTCL vocha ukinunua kwa kutumia tigopesa,mpesa,airtel money,simbanking kuna extra charge unayochajiwa kama service fee . Wakati nikinunua mfano nina line ya Tigo nikinunua vocha ya kampuni yao ya Tigo sichajiwi extra charge ya service fee.Hivi kwa akili yako unategemea Mimi mitume mtandao wa TTCL unaoniongezea gharama kwa matumizi ya simu kwa hizo extra charges Kila ninunuapo vocha? Mitaani wengi hawatumii TTCL line si kwa sababu hawaitaki bali vocha hamna na hizo TTCL pesa hamna!!!!! TTCL kiukweli biashara ya simu za mkononi wako zero sio siri.
...umesahau pia mawasiliano yako kudukuliwa mkuu...
 
Serikali imeshatoa tamko TTCL lazima kwa viongozi wabaojaziwa vocha na mwajiri.Sio wafanyakazi wote wa Serikali.Msemaji wa serikali katoa tamko.Kwa wengine karibuni TTCL kwa hiari yenu
 
hao wa nje wakipenda kutumia ya kwao kuliko vya nje mtauza nini? acha ubinafsi na utapia mlo wa akili, duania ni free market, unaleta hadhidhi za protectionism, haifanikiwi hata siku moja, kuna baraza la ushindani, ni kosa kulazimisha watu watumie bidhaa fulani na kuacha nyingine, kwahiyo wiki ijayo watumishi wote wataambiwa waangalie TBC na vingamuzi vya star times, baada ya mwezi watumishi wote wanaambiwa wahamie nyumba za NHC wakapange huko, then wataambiwa hata kuoa waoane kwanza wao kwa wao, idiot
..😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Serikali imeshatoa tamko TTCL lazima kwa viongozi wabaojaziwa vocha na mwajiri.Sio wafanyakazi wote wa Serikali.Msemaji wa serikali katoa tamko.Kwa wengine karibuni TTCL kwa hiari yenu
Wewe kama ni mfanyakazi wa umma nakupa pole
 
Back
Top Bottom