Kumekucha TTCL wateja sasa bwerere!

Kumekucha TTCL wateja sasa bwerere!

hao wa nje wakipenda kutumia ya kwao kuliko vya nje mtauza nini? acha ubinafsi na utapia mlo wa akili, duania ni free market, unaleta hadhidhi za protectionism, haifanikiwi hata siku moja, kuna baraza la ushindani, ni kosa kulazimisha watu watumie bidhaa fulani na kuacha nyingine, kwahiyo wiki ijayo watumishi wote wataambiwa waangalie TBC na vingamuzi vya star times, baada ya mwezi watumishi wote wanaambiwa wahamie nyumba za NHC wakapange huko, then wataambiwa hata kuoa waoane kwanza wao kwa wao, idiot
Akiwamaliza wapinzani atawarudia. . . .
Nisuala la muda tuu. Akiona inazingua atafanya kama la kukokotoo atajifanya hahusiki tutamsifia huku stress na hasira zikiwa zinatumaliza kidogokidogo
 
Huduma zimeboreka kwa kiwango kikubwa mno. Hivi sasa TTCL inapatikana nchi nzima kwa bei nafuu
TTCL ya sasa ni tofauti ya miaka mitano iliyopita.
Shida inaanzia kwa aliyetangaza maana watu tumehamia kumpinga kuliko kutafakari uhalisia wa huduma za TTCL kwa sasa. Watu tunapinga Magufuli, tunapinga Serikali kwahiyo hata aliposema suala la kuhimiza viongozi wa serikali kutumia TTCL imeleta tabu kweli kweli yaani kila sehemu watu wanakosoa tu.

Ila ukiangalia kwa uhalisia watu wa rank za juu serikalini wanaolipiwa muda wa mawasiliano wana sababu gani ya kutokutumia TTCL?

Tutumie TTCL ni yetu wenyewe na pia hatujakazwa kutumia mitandao mingine kwahiyo ni ruksa kuwa na laini nyingi na TTCL ikiwemo
 
Aiseee!!!

Hizi ni dalili za kufikia nchi ya uchumi wa kati!!!!

Hakika Mkulu ni mbinufu na anaweza!

Private sector mpo?

Alafu hapa naomba kuuliza,kutatungwa sheria ya kulazimisha watumishi kuweka muda wa maongezi kwenye hizo line?!!!

Na je,watakuwa wanafuatilia kujua kila mtumishi kaongea jambo gani ili kujua kama katumia line sahihi au laa?

Na je,sheria za nchi zinaruhusu hii kitu?

Na mtumishi ambae atatumia line ya simu za makampuni binafsi kufanya mawasiliano ya simu kwa shughuli za kiserikali, atakuwa amevunja sheria gani ya nchi au taratibu ipi ya utumishi wa umma?
Kilichobaki ni watumishi kusema hawana simu za matumizi ya kazi za serikali, unless wapewe bure na serikali na wawekewe airtime kama mashirika ya kimataifa yanavyofanya.
 
Watu wazima wasomi na raia huru kuanza kulazimishana mpka kwenye matumizi ya simu naona kuna ukakasi hapo
 
Watu wazima wasomi na raia huru kuanza kulazimishana mpka kwenye matumizi ya simu naona kuna ukakasi hapo
Hakuna aliyelazimishwa watu wamehimizwa kuikumbuka kampuni ya nyumbani.

Ila wale top officials wa serikali ni lazima maana utakuta hata hela za mawasiliano wanapewa sasa kwanini wazipeleke voda, airtel au tigo ilihali kuna TTCL?

Ukitaka kujua thamani ya kutumia vya nyumbani angalia USA anavyominyana na Mchina, USA alianza kuunda zengwe kwamba Huawei wanauza simu zilizofungwa program za kidukuzi baada ya kuona Huawei ameizidi Apple kwenye mauzo.
 
Ninayo mkuu sio utani pia ninazo laini zingine.
Kwanza TTCL iko cheap sana upande wa dakika na data sasa naanzaje kuikosa
Kuitumia TTCL kwa hiari yako ni vizuri sana ila tatizo nipale unapolazimishwa kuitumia. Wangewalazumisha wale wanaowalipia muda wa maongezi na simu zote za ofisi za serikali ziwe za TTCL ila sisi wengine watushawishi tuache tuone sababu sio amri tuu
 
Kuitumia TTCL kwa hiari yako ni vizuri sana ila tatizo nipale unapolazimishwa kuitumia. Wangewalazumisha wale wanaowalipia muda wa maongezi na simu zote za ofisi za serikali ziwe za TTCL ila sisi wengine watushawishi tuache tuone sababu sio amri tuu
Na Magufuli alisema viongozi wa serikali sidhani kama alisema watumishi wa kawaida ambao hata posho za mawasiliano hawapati.

Sema huku chini LGAs utakuta mkurugenzi naye anakomaa na walimu wake
 
Hakuna aliyelazimishwa watu wamehimizwa kuikumbuka kampuni ya nyumbani.

Ila wale top officials wa serikali ni lazima maana utakuta hata hela za mawasiliano wanapewa sasa kwanini wazipeleke voda, airtel au tigo ilihali kuna TTCL?

Ukitaka kujua thamani ya kutumia vya nyumbani angalia USA anavyominyana na Mchina, USA alianza kuunda zengwe kwamba Huawei wanauza simu zilizofungwa program za kidukuzi baada ya kuona Huawei ameizidi Apple kwenye mauzo.
Mkuu hueleweki! Umesema hakuna alolazimishwa na pia unasema top officers ni lazima watumie!!

Afu pia kutoa mfano wa Apple na Huawei bado umechemka sana tu.
Kwan makampuni binafs sio ya nyumbani?
Kuna maelf ya watanzania wameajiriwa huko so kuua sekta binafs ni kuua wananchi wako mwenyewe!
Kama nchi ni ya wanyonge na Serikali inajali wanyonge ingeimarisha sana sekta binafs ambako wanyonge wengi ndo wanakopumulia!!
 
Mkuu hueleweki! Umesema hakuna alolazimishwa na pia unasema top officers ni lazima watumie!!

Afu pia kutoa mfano wa Apple na Huawei bado umechemka sana tu.
Kwan makampuni binafs sio ya nyumbani?
Kuna maelf ya watanzania wameajiriwa huko so kuua sekta binafs ni kuua wananchi wako mwenyewe!
Kama nchi ni ya wanyonge na Serikali inajali wanyonge ingeimarisha sana sekta binafs ambako wanyonge wengi ndo wanakopumulia!!
Top officials wamelazimishwa maana wanapata posho ya mawasiliano, sisi kada za chini hakuna aliyelazimishwa na Rais.
Kampuni kama Airtel unaweza kusema ni ya nyumbani lakini tazama inamilikiwa na nani kwa maana ya hisa (wahindi wale).

Kidoogo sasahivi ndo serikali yetu imepata hisa nyingi
Screenshot_20190530-094829_Chrome.jpeg
 
Unamuogopa nani?
Sheria ya ajira na mahusiano kazini wapi imetaja lazima uwe na line ya TTCL?
Barua yako ya ajira inahicho kipengele?
Nani kakudanganya Magufuli anafuata sheria? kuna sheria ya kusimamisha increment ya mfanyakazi? kuna sheria inaruhusu KUTUMBULIWA MFANYAKAZI KIHOLELA? Agizo la Magufuli ndio sheria. waulize wakazi wa kimara waliokwena mahakamani kupinga kubomolewa nyumba zao na mahakama ikawapa ushindi, waulize kililchowakuta
 
Aiseee!!!

Hizi ni dalili za kufikia nchi ya uchumi wa kati!!!!

Hakika Mkulu ni mbinufu na anaweza!

Private sector mpo?

Alafu hapa naomba kuuliza,kutatungwa sheria ya kulazimisha watumishi kuweka muda wa maongezi kwenye hizo line?!!!

Na je,watakuwa wanafuatilia kujua kila mtumishi kaongea jambo gani ili kujua kama katumia line sahihi au laa?

Na je,sheria za nchi zinaruhusu hii kitu?

Na mtumishi ambae atatumia line ya simu za makampuni binafsi kufanya mawasiliano ya simu kwa shughuli za kiserikali, atakuwa amevunja sheria gani ya nchi au taratibu ipi ya utumishi wa umma?
Utata pia uko hapa, "....... kwa shughuli za kiserikali" kwani wananiwekea salio? Kama wanataka watoe ofa mtaalam kwa simu za watumishi. Kinyume na hapo kwa kulazimishwa zitasajiliwa halafu unatia chooni!
 
Back
Top Bottom